Marealle afungua kesi kutaka bibi yake afukuliwe mahala alipoishi miaka 80

Jaji Mfawidhi

JF-Expert Member
Feb 20, 2016
14,047
20,411
0000.jpeg

Mahakama Kuu Kanda ya Moshi, Mkoani Kilimanjaro,imeliamuru baraza la Ardhi wilaya ya Moshi Mkoani Kilimanjaro,kurejea upya mgogoro wa Ardhi wa familia maarufu ya chifu Marealle kwa kutembelea eneo linalobishaniwa na wanandugu hao na kurekodi upya mipaka na kisha kutoa maamuzi chini ya mwenyekiti mwingine wa baraza hilo

Jaji kuu,Lilian Mongella katika kesi namba 51/2023 ya mrufani Frank Mareale dhidi ya Ackley Mareale ambao wote ni wanandugu, Jaji Mongella alisema mahakama imepitia ushahidi na maamuzi ya Baraza la Nyumba na Makazi la Mji wa Moshi chini ya Uenyekiti wa Reginald Mtei yaliyotolewa mei 5 mwaka huu na kusema kuwa maamuzi hayo yalikuwa na kasoro za kisheria.

"Nimeamua kesi hii ya wanafamilia wa Mareale isikilizwe upya kwa sababu Baraza la Ardhi lilikosea kisheria kwa kushindwa kuonyesha mipaka ya ekari mbili inayogombaniwa"

Katika kesi ya awali iliyofunguliwa na Frank Mareale katika Baraza la Ardhi Nyumba na Makazi katika Mji wa Moshi, alikuwa na madai matatu moja wapo ni ombi la Baraza hilo litamke kuwa eneo la ekari mbili yeye ni mmiliki halali, Pili Baraza litoe amri ya kufukuliwa kwa mwili wa mama yake mdogo marehemu Veronica Mareale aliyeishi katika eneo hilo miaka 80 na kufariki mwaka 2020 na pia alitaka alipwe gharama za kesi.

Akizungumza nje ya Mahakama,Wakili wa Ackley Mareale,Julius Semali alisema kuwa hana pingamizi na uamuzi wa Mahakama kwani ana uhakika kuwa mteja wake ni mmiliki halali wa eneo hilo kwa kuwa mama yake alipata kihalali na alizikwa katika eneo lake.

Naye Wakili wa frank Mareale,Modest Njau aliishukuru Mahakama Kuu kwa uamuzi wake wa kuiagiza Baraza la Ardhi Nyumba na MakaziMoshi kusikiliza upya kesi hiyo na aliamuru Mwenyekiti wa Baraza na wajumbe wake wabadilishwe.

Njau alidai Mahakama Kuu iliona jinsi haki ilivyokuwa ikitaka kuchezewa katika usikilizwaji wa awali nayeye na mteja wake wameridhika na maamuzi hayo

Mei 5 mwaka huu chini ya mwenyekiti wa Baraza hilo la Ardhi Nyumba na Makazi ,Reginald Mtei lilitupilia mbali madai hayo ya Frank Mareale na kusema kuwa Ackley Mareale ni mmiliki halali wa eneo hilo na sio vinginevyo
.
 
Sidhani kama ni mali ila ni ardhi, wana utajiri uliopindukia ila wanalinda ardhi ya familia iliyopo kijijini.
Huwa ninawashangaa hawa ndugu zangu ni kipi haswa kinawafanya kuzozania vipande vidogo vya ardhi ya Kilimanjaro wakati nchi yetu ina maeneo mengi yasiyotumika.

Kilimanjaro pamejaa na ni eneo lenye population pressure kwa sasa.
 
Huwa ninawashangaa hawa ndugu zangu ni kipi haswa kinawafanya kuzozania vipande vidogo vya ardhi ya Kilimanjaro wakati nchi yetu ina maeneo mengi yasiyotumika.

Kilimanjaro pamejaa na ni eneo lenye population pressure kwa sasa.
Population pressure ya kilimanjaro unapima kwa vigezo gani?
Unafahamu half of the region wala hakuna aliyehamia?
Unajua kwamba mkoa unapoona kumejaa ni kwa wachaga wa Marangu?
Kuanzia Njia panda ya himo mpaka -Mwanga-Same- Hedaru na Mazinde kule umeona watu ?

Toka Same mpaka Hedaru unaendesha gari kilometa 40 bila kukuta nyumba wala kamji, wewe upo nyuma ya keyboard unaamini kilimanjaro imejaa?
 
Population pressure ya kilimanjaro unapima kwa vigezo gani?
Unafahamu half of the region wala hakuna aliyehamia?
Unajua kwamba mkoa unapoona kumejaa ni kwa wachaga wa Marangu?
Kuanzia Njia panda ya himo mpaka -Mwanga-Same- Hedaru na Mazinde kule umeona watu ?

Toka Same mpaka Hedaru unaendesha gari kilometa 40 bila kukuta nyumba wala kamji, wewe upo nyuma ya keyboard unaamini kilimanjaro imejaa?
Sikumaanisha Same na Mwanga. Nilimaanisha Wilaya ya Moshi huko maana ndipo kwetu na ndipo kwenye population pressure
 
Back
Top Bottom