Kazitunayo
JF-Expert Member
- Mar 30, 2013
- 3,784
- 3,205
Marais hawa wastaafu hawajaonekana katika tukio hili la kiistoria pamoja na waziri mkuu mstaafu Sumaye pia hajaonekana Dodoma..
Hii ni kusema hawajaridhika na mchakato ulivyopelekwa au wapo nje ya nchi?
============
Hii ni kusema hawajaridhika na mchakato ulivyopelekwa au wapo nje ya nchi?
============
CHANZO: Mtanzania
![]()
Benjamin Mkapa
NA JONAS MUSHI, DAR ES SALAAM
RAIS mstaafu wa awamu ya tatu, Benjamin Mkapa na Rais mstaafu wa Zanzibar, Aman Abeid Karume hawakuonekana katika sherehe za makabidhiano ya Katiba inayopendekezwa zilizofanyika jana mjini Dodoma.
Kutokuwapo kwao katika sherehe hizo, kunakwenda tofauti na tangazo lililotolewa na Mkuu wa Mkoa wa Dodoma, Dk. Rehema Nchimbi aliyesema viongozi wote wastaafu wamealikwa na watakuwapo.
Pamoja na kutokuwapo kwa viongozi hao, haikutolewa taarifa yoyote hadi mwisho wa shughuli hizo.
Mbali na Mkapa na Karume, pia wajumbe wote wa iliyokuwa Tume ya Mabadiliko ya Katiba pamoja na Mwenyekiti wake Jaji Joseph Warioba hawakuwapo katika sherehe hizo.
Kutokana na hali hiyo pia Makamu wa Kwanza wa Rais wa Serikali ya Umoja wa Kitaifa ya Zanzibar, Maalim Seif Sharif Hamad, naye kuwepo katika sherehe hizo.
Kutoonekana kwa vigogo hao huenda kukaibua mjadala mzito kwa wananchi kutokana na uzito wa tukio la jana la kukabidhiwa Katiba inayopendekezwa kwa Rais Jakaya Kikwete na Rais wa Zanzibar, Dk. Ali Mohamed Shein.