Marafiki wa Lowassa waja na staili mpya

Marafiki wa Lowassa waja na staili mpya

Lowassa ni mgonjwa sana, tusitake kuingia gharama ya kuchagua Rais mara 2
 
Moshi. Mbunge wa Moshi Vijijini na Mjumbe wa Nec ya CCM, Dk Cyrill Chami, amewaomba walimu zaidi ya 2,700 wamuombee Waziri mkuu mstaafu, Edward Lowassa, ili ‘ndoto’ yake iweze kutimia.

Wakati Dk. Chami akiwaomba walimu hao, mtandao wa marafiki wa Lowassa Kanda ya Kaskazini, juzi walikuja na staili mpya ya kumshawishi Mbunge huyo wa Monduli agombee nafasi ya Urais.

Staili hiyo mpya imekuja wakati CCM ikiwa imempiga ‘stopu’ kuendelea na utaratibu wake wa kupokea makundi ya watu wanaomshawishi kugombea urais na yeye (Lowassa) kuridhia na kuwaomba wananchi wasubiri maelekezo ya CCM.

Marafiki hao ambao ni wanafunzi wa vyuo vikuu mkoani Kilimanjaro, walikwenda kitengo cha damu salama Kanda ya Kaskazini kuchangia damu kama njia ya kutambua na kuenzi upendo wa Lowassa.

Tukio hilo la wanafunzi hao kwenda katika kitengo hicho, kilitanguliwa na tukio la mkutano mkuu wa Chama cha Akiba na Mikopo (Saccos) ya Walimu Moshi Vijijini kufanya mkutano wao mkuu. Katika mkutano huo, Dk Chami aliyekuwa mgeni rasmi, aliwaambia amekwenda pale akiwa na salamu kutoka kwa Lowassa kwamba anawapenda sana walimu. “Anasema anawapenda na anawakumbuka sana na anawaomba mmuombee ili ndoto yake na ile safari yake (bila kuitaja) itimie,” alisema Dk Chami na walimu hao kulipuka kwa vigelegele.

Katika tukio la uchangiaji wa damu, wanafunzi zaidi ya 100 wa vyuo vikuu mkoani Kilimanjaro, walitumia tukio hilo kumuunga mkono Lowassa wakimsihi atangaze nia ya kuwania Urais 2015.

Mratibu wa marafiki wa Lowassa, Noel Nnko, alisema wanafunzi hao wameamua kuchangia damu kumuunga mkono kada huyo kwa vile wao hawana uwezo wa kutoa fedha za kuchangia fomu.

Chanzo:
Mwananchi

Tumechoka sasa, kila siku Lowassa, hivi nyie mwanachi news paper hakuna habari zingine, kila siku ni Lowassa tu???? Au na nyie mmehongwa??? Hebu tuondoleeni upuuzi...!
 
Lowassa anashawishiwa kwa lipi, wakati inajulikana wazi kwamba Urais anautaka kwa udi na uvumba, tangu mwaka 1995? Maigizo mengine bhanaaaaa!!!!!!

Hii ndiyo ajabu. This is a misuse of the word ' Shawishi'. Kuna wakati aliwahi kusema hataki urais hata ashawishiwe? Akili za watu kama akina Chami zina kasoro kubwa na hasa tangu alipoondolewa kwenye uwaziri amekuwa off point mara nyingi akitawaliwa na jazba kuliko kutumia logic.
 
Moshi. Mbunge wa Moshi Vijijini na Mjumbe wa Nec ya CCM, Dk Cyrill Chami, amewaomba walimu zaidi ya 2,700 wamuombee Waziri mkuu mstaafu, Edward Lowassa, ili ‘ndoto’ yake iweze kutimia.

Wakati Dk. Chami akiwaomba walimu hao, mtandao wa marafiki wa Lowassa Kanda ya Kaskazini, juzi walikuja na staili mpya ya kumshawishi Mbunge huyo wa Monduli agombee nafasi ya Urais.

Staili hiyo mpya imekuja wakati CCM ikiwa imempiga ‘stopu’ kuendelea na utaratibu wake wa kupokea makundi ya watu wanaomshawishi kugombea urais na yeye (Lowassa) kuridhia na kuwaomba wananchi wasubiri maelekezo ya CCM.

Marafiki hao ambao ni wanafunzi wa vyuo vikuu mkoani Kilimanjaro, walikwenda kitengo cha damu salama Kanda ya Kaskazini kuchangia damu kama njia ya kutambua na kuenzi upendo wa Lowassa.

Tukio hilo la wanafunzi hao kwenda katika kitengo hicho, kilitanguliwa na tukio la mkutano mkuu wa Chama cha Akiba na Mikopo (Saccos) ya Walimu Moshi Vijijini kufanya mkutano wao mkuu. Katika mkutano huo, Dk Chami aliyekuwa mgeni rasmi, aliwaambia amekwenda pale akiwa na salamu kutoka kwa Lowassa kwamba anawapenda sana walimu. “Anasema anawapenda na anawakumbuka sana na anawaomba mmuombee ili ndoto yake na ile safari yake (bila kuitaja) itimie,” alisema Dk Chami na walimu hao kulipuka kwa vigelegele.

Katika tukio la uchangiaji wa damu, wanafunzi zaidi ya 100 wa vyuo vikuu mkoani Kilimanjaro, walitumia tukio hilo kumuunga mkono Lowassa wakimsihi atangaze nia ya kuwania Urais 2015.

Mratibu wa marafiki wa Lowassa, Noel Nnko, alisema wanafunzi hao wameamua kuchangia damu kumuunga mkono kada huyo kwa vile wao hawana uwezo wa kutoa fedha za kuchangia fomu.

Chanzo:
Mwananchi

Wana Jf naomba niwashawishi pia tumwombee Chami arudi katika ndoa yake.
 
CCM watakua na kichaa yaani wao ndio wamuondoe uwaziri mkuu leo wampe urais bwiiii
 
Rais alisema watu waweza shawishiwa kugombea urais 2015 so Lowasa anaendelea kushawishiwa na wadau mbali mbali. Lowasa is NON STOP kwa presidency contest this year.
 
Ndoto aote lowasa walimu ndio wamuombe ili hiyo ndoto iweze kutimia!!!

Ujinga mwingine unalemea sana.

Hivi ni mema gani yanayotambuliwa na makundi tuu ambayo ni rafiki zake ila wengine hatujui? Huu uraisi utatutokea puani
 
Rais alisema watu waweza shawishiwa kugombea urais 2015 so Lowasa anaendelea kushawishiwa na wadau mbali mbali. Lowasa is NON STOP kwa presidency contest this year.

Aandae tu mabingwa wa magonjwa ya moyo
 
Kama afai toeni mbadala wake basi sio kukosoa tu sijui mmekula vyakula gn nyie....
 
Lowassa ni Fisadi mkuu nchi hii ndiyo maana alijiuzulu, Hivyo ufisadi ni ugonjwa mbaya sana kuliko hata huo alionao wa Kutetemeka. Aachane na mambo ya urais kwani bado ni mchafu sana, Nchi yetu itakuwa rehani tukiendelea ku entertain haya maigizo ya Lowassa
Mi nadhani kwa CCM ndo jembe la ng'ombe kwani kigezo no 1 ni kuwa joka kuu la makengeza. Sasa katika mafisadi mbadhani nani mbabe. Ngoja na Chenge aibuke siku ya kuchukua fomu
 
Lowassa ni mgonjwa sana, tusitake kuingia gharama ya kuchagua Rais mara 2
Hata Kikwete 2005 tuliambiwa ni mgonjwa sana, hayo ni magonjwa ya kupakaziwa tu. Wewe unaweza kutueleza ugonjwa wa Lowasa?!
 
Hata Kikwete 2005 tuliambiwa ni mgonjwa sana, hayo ni magonjwa ya kupakaziwa tu. Wewe unaweza kutueleza ugonjwa wa Lowasa?!

Parkinson syndrome imekula upande wa kulia. Angalia jicho lake, vile vile akitembea na mkono wa kulia hawezi hata kushika microphone
 
Acha nianze kwa kutamka wazi kabisa; Mimi siipendi ccm kabisaa na hata wakimchagua nani kwangu hainiumizi kichwa ila, kwa kuwa ccm lazima ishinde kwa mbinde zao, nchi hii ikimpata EL, hakika kitaeleweka. Kinyume cha hapo, hakuna anayefaa katika wote wanao gombea gombea kutoka ccm.
EL ndiye mwenyewe pale lumumba wala hakuna wa kumfikia, hivyo maccm wamchague huyo tu akifurumue hicho chama mfu.
 
Lowassa katu hawezi kuwa rahisi wa nchi hii, ikitokea ivyo nitakuwa sina sababu ya kuishi tena kwenye nchi kama hii nitafungasha vilivyo vyangu mimi na familia yangu haoooo tunayeyaa zetu Mogadishu....ni afadhali nikaishi kwenye nchi yenye misukosuko kama Somalia kuliko kuishi kwenye nchi inayoongozwa na Lowassa...!!
 
Lakin ole wetu tukijvuruga kumpa huyu Mzeeee huo uraisi anao uhtaji kwa njia ovu hv anampango wakutufanyaje? Kama kweli tunamuenzi muasisi Wa Taifa hili basis tumkatae maana hana cfa alizo zsema mwalimu
 
Back
Top Bottom