comrade_kipepe
JF-Expert Member
- Jun 25, 2019
- 6,465
- 11,535
Kuna namna wanafanya vitu kwa mihemko, kuna watu kabisa wanaonekana hawakua na kesi lakini wakawapa kesi ya uhaini bila kujua hao watu ndio wanawatengeneza kua wapinzani wao.
Mtu wanajua kabisa hana kesi na hana madhara, yanini kumpaisha na kumbrand maana mwisho wa siku atatoka maana kesi hamna na akitoka anakua washamtengeneza kua mpinzani wao.
Mfano huyu jamaa Mika Chavala wengi tulikuwa hatumjui lakini CCM ndio wametulazimisha tumjue, jamaa umaarufu wake umeongezeka maradufu akiwa nyuma ya nondo! Kajiongezea kijiji kirahisi sana, kaonekana shujaa wakati hata haikutakiwa iwe hivyo.
Mi naona kabisa CCM inajitengenezea maadui na wakosoaji kila kukicha, kuna waliokua hawampendi lisu, lakini wanapompitisha lissu anazidi kujipatia wafuasi, wengine wanakua wafuasi wake kwasababu tu ya kumuhurumia anayopitia.
Yani mipango ya ccm mara nyingine siielewi kabisa.
Mtu wanajua kabisa hana kesi na hana madhara, yanini kumpaisha na kumbrand maana mwisho wa siku atatoka maana kesi hamna na akitoka anakua washamtengeneza kua mpinzani wao.
Mfano huyu jamaa Mika Chavala wengi tulikuwa hatumjui lakini CCM ndio wametulazimisha tumjue, jamaa umaarufu wake umeongezeka maradufu akiwa nyuma ya nondo! Kajiongezea kijiji kirahisi sana, kaonekana shujaa wakati hata haikutakiwa iwe hivyo.
Mi naona kabisa CCM inajitengenezea maadui na wakosoaji kila kukicha, kuna waliokua hawampendi lisu, lakini wanapompitisha lissu anazidi kujipatia wafuasi, wengine wanakua wafuasi wake kwasababu tu ya kumuhurumia anayopitia.
Yani mipango ya ccm mara nyingine siielewi kabisa.