Zitto
Former MP Kigoma Urban
- Mar 2, 2007
- 1,562
- 10,879
HOFU ya CCM ya Magufuli ni Hatari kwa Nchi yetu
Kwa wiki moja sasa kumekuwa na mjadala mkali nchini kuhusu Tamko lililotolewa na Makatibu Wakuu wastaafu wa CCM Kanali Abdulrahman Kinana na Luteni Yusuf Makamba kuhusu mtu anayeitwa Cyprian Musiba. Wana CCM hao wameandika malalamiko yao kwa Baraza la Wazee wa Chama chao ili hatua zichukuliwe. Katika hali ya kawaida hili lilipaswa kuwa jambo la CCM na kushughulikiwa na chama hicho wenyewe. Hata hivyo jambo hilo limechukua mkondo wa kitaifa na haswa usalama wa watu na usalama wa Taifa.
Tamko la Kanali Kinana na Luteni Makamba limeujulisha Umma mipango dhalimu ya kubumba kesi za uhaini kwa Wanasiasa waandamizi nchini kutoka Chama Tawala na Vyama vya Upinzani. Pia baadhi ya wana harakati ambao Bwana Musiba amekuwa akiwataja kuwa ni watu hatari kwa nchi ni miongoni mwa wahanga wa mipango hiyo. Kina Kinana wametibua mpango huo ndio maana wafuasi au wanaojiita wanaomwunga mkono Rais Magufuli wametaharuki na wanajaribu sana mipango yao iendelee. Shabaha ya kesi ya uhaini ni kuhakikisha ama mwaka 2020 hapatakuwa na uchaguzi au uchaguzi ufanyike wakati wanasiasa wote waandamizi nchini wakiwa magerezani au wasiwepo kabisa.
Baadhi ya wanasiasa wameanza kujiokoa kwa kujiegemeza upande wa wenye mamlaka. Hata wale ambao kwa muda sasa wamekuwa ni tumaini la Wananchi kwa kuwa wakosoaji wakuu wa Serikali wamerudi nyuma na kutoa kauli za kujikosha . Kwa mfano mtu ambaye amekuwa akikosoa vikali Serikali kule mwanzo nia ilikuwa ni kumnyima uhalali Rais Magufuli ? Mbona wakati wa Uongozi wa Rais Jakaya Kikwete alikuwa anashambuliwa sana na Wazee kama vile Mzee Butiku, Warioba nk lakini hatukusikia haya? Kitu gani ‘special’ wakati huu? Nadhani huu Ni wakati kwa wapenda demokrasia wote kutoogopa na kuwa pamoja.
Sisi wengine tunajua kitambo kuwa CCM imeshafika mwisho wake. Bahati mbaya sana CCM ya Magufuli inataka kuondoka na nchi yetu. Tusikubali. Tumesoma kuwa kabla ya Wazee hao wastaafu wa CCM kuandika, waliomba ushauri na Mzee Pius Msekwa akawaambia ‘jibuni Mapigo’. Ina maana Msekwa naye anataka kuua Chama chao? CCM ianguke yenyewe na ituachie nchi yetu.
Hofu ya Watawala kuhusu 2020 isihatarishe nchi yetu. Mipango ya Kesi ya Uhaini iachwe mara moja. Ukosoaji ndani au nje ya vyama vya Siasa kamwe haiwezi kuwa uhaini. Acha demokrasia ishamiri
Zitto Kabwe
18/7/2019
Kwa wiki moja sasa kumekuwa na mjadala mkali nchini kuhusu Tamko lililotolewa na Makatibu Wakuu wastaafu wa CCM Kanali Abdulrahman Kinana na Luteni Yusuf Makamba kuhusu mtu anayeitwa Cyprian Musiba. Wana CCM hao wameandika malalamiko yao kwa Baraza la Wazee wa Chama chao ili hatua zichukuliwe. Katika hali ya kawaida hili lilipaswa kuwa jambo la CCM na kushughulikiwa na chama hicho wenyewe. Hata hivyo jambo hilo limechukua mkondo wa kitaifa na haswa usalama wa watu na usalama wa Taifa.
Tamko la Kanali Kinana na Luteni Makamba limeujulisha Umma mipango dhalimu ya kubumba kesi za uhaini kwa Wanasiasa waandamizi nchini kutoka Chama Tawala na Vyama vya Upinzani. Pia baadhi ya wana harakati ambao Bwana Musiba amekuwa akiwataja kuwa ni watu hatari kwa nchi ni miongoni mwa wahanga wa mipango hiyo. Kina Kinana wametibua mpango huo ndio maana wafuasi au wanaojiita wanaomwunga mkono Rais Magufuli wametaharuki na wanajaribu sana mipango yao iendelee. Shabaha ya kesi ya uhaini ni kuhakikisha ama mwaka 2020 hapatakuwa na uchaguzi au uchaguzi ufanyike wakati wanasiasa wote waandamizi nchini wakiwa magerezani au wasiwepo kabisa.
Baadhi ya wanasiasa wameanza kujiokoa kwa kujiegemeza upande wa wenye mamlaka. Hata wale ambao kwa muda sasa wamekuwa ni tumaini la Wananchi kwa kuwa wakosoaji wakuu wa Serikali wamerudi nyuma na kutoa kauli za kujikosha . Kwa mfano mtu ambaye amekuwa akikosoa vikali Serikali kule mwanzo nia ilikuwa ni kumnyima uhalali Rais Magufuli ? Mbona wakati wa Uongozi wa Rais Jakaya Kikwete alikuwa anashambuliwa sana na Wazee kama vile Mzee Butiku, Warioba nk lakini hatukusikia haya? Kitu gani ‘special’ wakati huu? Nadhani huu Ni wakati kwa wapenda demokrasia wote kutoogopa na kuwa pamoja.
Sisi wengine tunajua kitambo kuwa CCM imeshafika mwisho wake. Bahati mbaya sana CCM ya Magufuli inataka kuondoka na nchi yetu. Tusikubali. Tumesoma kuwa kabla ya Wazee hao wastaafu wa CCM kuandika, waliomba ushauri na Mzee Pius Msekwa akawaambia ‘jibuni Mapigo’. Ina maana Msekwa naye anataka kuua Chama chao? CCM ianguke yenyewe na ituachie nchi yetu.
Hofu ya Watawala kuhusu 2020 isihatarishe nchi yetu. Mipango ya Kesi ya Uhaini iachwe mara moja. Ukosoaji ndani au nje ya vyama vya Siasa kamwe haiwezi kuwa uhaini. Acha demokrasia ishamiri
Zitto Kabwe
18/7/2019