Mapishi ya kisamvu

m.agape

Senior Member
Dec 7, 2012
141
79
attachment.php

Habari wana jukwaa.

Najitokeza kwenu kuomba mafunzo ya upishi wa kisamvu.
Nimekula kisamvu kwenye sherehe kitamu sana
Nifunzeni nipate kukipika mwenyewe nyumbani.
Asanteni

Recipe ya mama yangu.

Mahitaji

1: kisamvu kilichotwangwa na vitunguu saum, (waweza blend kama huna kinu) vikombe 2
2: vitunguu maji viwili vikubwa.
3: mafuta kidogo
4: karanga zilizosiginwa (sagwa na kulainika) 3/4 kikombe.
5: chumvi kwa ladha.

Hatua

1: chemsha kisamvu kwa maji mengi mpaka kiive (mara nyingi utahitaji kuongeza maji maana kisamvu kina sumu ambayo huondoshwa kwa joto)

2. Chukua sifuria nyingine, weka mafuta na kaanga vitunguu vyako mpaka vilainike na kuanza kubadili rangi.

3: Weka kisamvu kwenye vitunguu, kaanga kwa dakika 3-5.

4: Weka karanga na changanya kama unasonga ugali vile mpaka ichanganyikane vizuri ongeza na chumvi kwa ladha.

NB:
Waweza weka nyanya wakati unakaanga vitunguu.

Kisamvu cha Kinyamwezi hakina mchuzi hivyo hakikisha maji yamepungua au kukauka wakati unaweka kwenye vitunguu vyako.
Karanga nyingi ni siri ya kisamvu cha kinyamwezi

Ngoja watumia nazi waje watoe namna yao.
 

Attachments

  • kisamvu.JPG
    kisamvu.JPG
    25.8 KB · Views: 2,880
Recipe ya mama yangu.
Mahitaji
1: kisamvu kilichotwangwa na vitunguu thoum, (waweza blend kama huna kinu) vikombe 2
2: vitunguu maji viwili vikubwa.
3: mafuta kidogo
4: karanga zilizosiginwa (sagwa na kulainika) 3/4 kikombe.
5: chumvi kwa ladha.

Hatua.
1: chemsha kisamvu kwa maji mengi mpaka kiive (mara nyingi utahitaji kuongeza maji maana kisamvu kina sumu ambayo huondoshwa kwa joto)
2. Chukua sifuria nyingine, weka mafuta na kaanga vitunguu vyako mpaka vilainike na kuanza kubadili rangi.
3: weka kisamvu kwenye vitunguu, kaanga kwa dakika 3-5.
4: weka karanga na changanya kama unasonga ugali vile mpaka ichanganyikane vizuri ongeza na chumvi kwa ladha.
NB:
Waweza weka nyanya wakati unakaanga vitunguu.
Kisamvu cha kinyamwezi hakina mchuzi hivyo hakikisha maji yamepungua au kukauka wakati unaweka kwenye vitunguu vyako.
Karanga nyingi ni siri ya kisamvu cha kinyamwezi

Ngoja watumia nazi waje watoe namna yao.
 
Ira ukiweka na ka piripiri na ka iliki kwa bari kananogaga? Au kwenye unyamwezi hamwekagi? Waarike na wa samli baada ya wenye nazi.



Recipe ya mama yangu.
Mahitaji
1: kisamvu kilichotwangwa na vitunguu thoum, (waweza blend kama huna kinu) vikombe 2
2: vitunguu maji viwili vikubwa.
3: mafuta kidogo
4: karanga zilizosiginwa (sagwa na kulainika) 3/4 kikombe.
5: chumvi kwa ladha.

Hatua.
1: chemsha kisamvu kwa maji mengi mpaka kiive (mara nyingi utahitaji kuongeza maji maana kisamvu kina sumu ambayo huondoshwa kwa joto)
2. Chukua sifuria nyingine, weka mafuta na kaanga vitunguu vyako mpaka vilainike na kuanza kubadili rangi.
3: weka kisamvu kwenye vitunguu, kaanga kwa dakika 3-5.
4: weka karanga na changanya kama unasonga ugali vile mpaka ichanganyikane vizuri ongeza na chumvi kwa ladha.
NB:
Waweza weka nyanya wakati unakaanga vitunguu.
Kisamvu cha kinyamwezi hakina mchuzi hivyo hakikisha maji yamepungua au kukauka wakati unaweka kwenye vitunguu vyako.
Karanga nyingi ni siri ya kisamvu cha kinyamwezi

Ngoja watumia nazi waje watoe namna yao.
 
Ira ukiweka na ka piripiri na ka iliki kwa bari kananogaga? Au kwenye unyamwezi hamwekagi? Waarike na wa samli baada ya wenye nazi.

Pilipili tunaweka, ila kama ni mlo wa familia unaishia kuchemshia tu kapilipili mbuzi kako.

Hiliki mama haweki, ila nitajaribu. Asante.
 
Recipe ya mama yangu.
Mahitaji
1: kisamvu kilichotwangwa na vitunguu thoum, (waweza blend kama huna kinu) vikombe 2
2: vitunguu maji viwili vikubwa.
3: mafuta kidogo
4: karanga zilizosiginwa (sagwa na kulainika) 3/4 kikombe.
5: chumvi kwa ladha.

Hatua.
1: chemsha kisamvu kwa maji mengi mpaka kiive (mara nyingi utahitaji kuongeza maji maana kisamvu kina sumu ambayo huondoshwa kwa joto)
2. Chukua sifuria nyingine, weka mafuta na kaanga vitunguu vyako mpaka vilainike na kuanza kubadili rangi.
3: weka kisamvu kwenye vitunguu, kaanga kwa dakika 3-5.
4: weka karanga na changanya kama unasonga ugali vile mpaka ichanganyikane vizuri ongeza na chumvi kwa ladha.
NB:
Waweza weka nyanya wakati unakaanga vitunguu.
Kisamvu cha kinyamwezi hakina mchuzi hivyo hakikisha maji yamepungua au kukauka wakati unaweka kwenye vitunguu vyako.
Karanga nyingi ni siri ya kisamvu cha kinyamwezi

Ngoja watumia nazi waje watoe namna yao.

Loh!! Hapa umenikumbusha mbali sana
 
Asanteni kwa somo zuri, naomba na wapishi wa nazi mnifunze tafadhal.

Mapishi hayatofautiani na wa karanga sema tu nazi unakamua tui mbili la kwanza liwe zitooo kabisa na la pili zito kidogo afu hapo unaanza kuweka tui la pili linachemka kidogo na kukauka unaweka lile zito unageuza geuza ili tui lifike kote! Unageuza geuza ili tui lianze kuchemka lisije likakatika likichanganya kuchemka unaacha dakika2-3 unaepua tayari kwa matumizi! Viungo vingine unaweza kukatia karoti kama una kunde pia zinazoga sana ukizipika pamoja na kisamvu! Maana kisamvu pekeyake hakinogi kinakuwa kama kinyesi cha ng'ombe!
 
Recipe ya mama yangu.
Mahitaji
1: kisamvu kilichotwangwa na vitunguu thoum, (waweza blend kama huna kinu) vikombe 2
2: vitunguu maji viwili vikubwa.
3: mafuta kidogo
4: karanga zilizosiginwa (sagwa na kulainika) 3/4 kikombe.
5: chumvi kwa ladha.

Hatua.
1: chemsha kisamvu kwa maji mengi mpaka kiive (mara nyingi utahitaji kuongeza maji maana kisamvu kina sumu ambayo huondoshwa kwa joto)
2. Chukua sifuria nyingine, weka mafuta na kaanga vitunguu vyako mpaka vilainike na kuanza kubadili rangi.
3: weka kisamvu kwenye vitunguu, kaanga kwa dakika 3-5.
4: weka karanga na changanya kama unasonga ugali vile mpaka ichanganyikane vizuri ongeza na chumvi kwa ladha.
NB:
Waweza weka nyanya wakati unakaanga vitunguu.
Kisamvu cha kinyamwezi hakina mchuzi hivyo hakikisha maji yamepungua au kukauka wakati unaweka kwenye vitunguu vyako.
Karanga nyingi ni siri ya kisamvu cha kinyamwezi

Ngoja watumia nazi waje watoe namna yao.

Mnyamwezi halisi Kaunga nakumbukuka kipindi tunakua kwa mama hii ilikuwa ndo mboga ya wageni, kinapendeza kuliwa na wali kwa mkono, halafu kikilala ladha inaongezeka sana.
 
Last edited by a moderator:
Kaunga, recipe nzuri. Halafu umewahi kula kile kisamvu cha wanyarwanda? wanaita Isombe. Mie kinachonishinda wanaweka na samaki samaki aliyekaushwa (rafiki yangu huwa anamkatakata samaki).. Ila wenyewe wanaipenda sanaaa hiyo Isombe.
 
Last edited by a moderator:
Kaunga, recipe nzuri. Halafu umewahi kula kile kisamvu cha wanyarwanda? wanaita Isombe. Mie kinachonishinda wanaweka na samaki samaki aliyekaushwa (rafiki yangu huwa anamkatakata samaki).. Ila wenyewe wanaipenda sanaaa hiyo Isombe.

Mie nilikipenda sana nilikula kule 'Rubavu' boda ya Rwanda na DRc wanapika vizuri sana. Lusaka niliona wanaweka maziwa kitamu kweli ha ha mapishi haya si mchezo....

Upo mrembo??? Missing u so much.....
 
Last edited by a moderator:
Mie nilikipenda sana nilikula kule 'Rubavu' boda ya Rwanda na DRc wanapika vizuri sana. Lusaka niliona wanaweka maziwa kitamu kweli ha ha mapishi haya si mchezo....

Upo mrembo??? Missing u so much.....

Usiniambie umekipenda hicho kisamvu..safi sana!
Nipo mamito, majukumu yametinga mumie..miss you too, nawe umepotea kiaina. Sijui umefichwa wapi?
 
Napenda sana kisamvu u will never miss it kwa fridge yangu. Mapishi yangu ni kama ya Kaunga sema mie napenda kurahisisha mambo nikishaweka jikoni na kukichemsha kwa muda naweka kitunguu kabsa na chumvi na mafuta kidogo sana cz hata karanga zina mafuta.
Then natengeneza tui la karanga zito sana naweka thn nakoroga mpaka kiwe kizito...!!!!
Napenda kula na wali wa nazi...!!!!
 
Last edited by a moderator:
viola richard

. . .Kwanza kabisa unakichemsha kwa chumvi kidogo,maji na pilipili kidogo kama unapenda, mpaka kialainike. Kati ya saa 1 - 2 kutegemea na moto wako (aina ya jiko). Uwe unaangalia maji mara kwa mara ili kisiungue.
. . .#2 Kaanga vitunguu, vikiiva weka kisamvu chako kikiwa kikavu (kama kuna mchuzi uache kwanza).
. . .#3 Weka ule mchuzi ukifuatiwa na nazi au karanga (zilizosagwa) kuendana na matakwa yako. Punguza moto na acha ulichoweka (karanga/nazi) kiivie vizuri. Usiache kuangalia na kukoroga mara kwa mara ili kisiungue.

Ngoja wakina farkhina , King'asti , Kaunga na wengine waje kukupa maujanja zaidi maana nasikiaga wengine wanaweka mpaka nyama na vikorokoro vingine vingine. Mi naishiaga kwenye pilipili na nazi/karanga tu.
 
Last edited by a moderator:
Wifi kwa mapishi huwa nakuaminia. Hapo labda nitaongeza vitunguu swaumu tu. Halafu kuna mtu kaniambia chungu kinafaa kupikia kwenye jiko la gas, manake kisamvu kikipikwa na chungu kinakuwa extra special na hakiungui chini.
viola richard

. . .Kwanza kabisa unakichemsha kwa chumvi kidogo,maji na pilipili kidogo kama unapenda, mpaka kialainike. Kati ya saa 1 - 2 kutegemea na moto wako (aina ya jiko). Uwe unaangalia maji mara kwa mara ili kisiungue.
. . .#2 Kaanga vitunguu, vikiiva weka kisamvu chako kikiwa kikavu (kama kuna mchuzi uache kwanza).
. . .#3 Weka ule mchuzi ukifuatiwa na nazi au karanga (zilizosagwa) kuendana na matakwa yako. Punguza moto na acha ulichoweka (karanga/nazi) kiivie vizuri. Usiache kuangalia na kukoroga mara kwa mara ili kisiungue.

Ngoja wakina farkhina , King'asti , Kaunga na wengine waje kukupa maujanja zaidi maana nasikiaga wengine wanaweka mpaka nyama na vikorokoro vingine vingine. Mi naishiaga kwenye pilipili na nazi/karanga tu.
 
Hata nazi pia ni swaafi kabisa. Issue ya nazi huwa ni kwenye kuchuja. Unatakiwa kuchuja na maji kidogo sana ya uvuguvugu mkali (warm, not lukewarm). Kwa hiyo uchuje kama mara tatu, na ukiweka tui shurti ulikoroge lisikatike. Nazi haidanganyi atii!
Hiki kisamvu kwa karanga ndio noma ila nazi hamna kitu..
 
Mi huwa napenda kupika kisamvu cha Nazi mixer Na Utumbo Na kapilipili mbuzi kinanogaje!!!
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom