LOTH HEMA
JF-Expert Member
- Dec 6, 2015
- 26,826
- 41,352
Awali kabisa sikujua chakula kinachoitwa biriani ila nilikuwa nasikia tu kuna chakula kinaitwa biriani. Kumbe nikaja kuambiwa kuwa nilishawahi kula kwenye sherehe na mikutano ya kiofisi. Nikaambiwa ni wali uliotiwa rangi rangi una nyama ya kuku na viungo fulanifulani hivi. Hotelini ni bei ghali kupata biriani na ni mara chache huandaliwa kwa wiki sio kila siku na mchele wake ni maalumu. Sasa nataka nijue maandilzi na mahitaji ya kupika biriani yanaandaliwa vipi. Wapishi wapevu naombeni maarifa yenu namna ya kupika biriani