Sudysoko
JF-Expert Member
- Aug 19, 2015
- 449
- 180
Yaliyoandikwa na Abdul Kambaya aliyekuwa naibu mkurugenzi wa Habari na Uenezi cuf leo mtandaoni(FB)
"SIJAMBO GENI, HATA FIRAUN ALIPOSHINDWA KUJIBU HOJA ZA MUSSA ALITUMIA JESHI
Nimekua napigiwa simu nyingi toka kwa Wanachama wenzangu na Waandishi wa habari kuhusu Taarifa zilizozagaa kwenye Mitandao. Majibu yangu ya awali Kuhusu Taarifa hizo ni
1 Moja Baraza Kuu lina Mamlaka ya kufanya hivyo kwa mujibu wa Katiba na kwa kwa kufuata Katiba jinsi inavyoeleza kwenye hizo taratibu za kuchukua hatua za Kinidhamu.
2 Mimi na wenzangu tunaotajwa kwenye kadhia hiyo ikiwa ni Pamoja na Wabunge wa Mtwara Mjini (Maftaha Nachuma) na Magdalena Sakaya Mbunge wa Jimbo la Kaliua na Diwani wa Kata ya Misima Wilayani Handeni,pamoja na wale ambao sikuwataja hatukuwepo wakati hukumu hiyo inatolewa na Baraza Kuu lilofanyika jana Mjini Unguja katika Visiwa vya Zanzibar.
3 Baada ya kuahirishwa kwa Mkutano Mkuu uliofanyika pale Ubungo Plaza Tarehe 21 /08 /2016 kutokana na Wajumbe 324 kutoridhishwa na ukiukwaji wa Katiba ya Chama chetu ikiwa ni pamoja na kuingizwa kwa Wajumbe wasio halali kwenye Mkutano Mkuu, mimi ni miongoni mwa Wajumbe tuliojiorodhesha na kuandika barua ya Malalamiko na kupeleka Ofisi ya Msajili wa Vyama.
Kutokana na Mambo hayo Matatu, nawaomba Wanacuf msifadhahike na wala msihuzunike waliotufukuza kabla hata ya kutoa majibu ya hoja zetu tulizowasilisha kwa Msajili, bila shaka hawana Majibu ya sahihi ya hoja zetu. Na jambo hili sio geni kwa hapa Duaniani, Firaun aliposhindwa kuthibitisha kua yeye ndie Mungu, alitumia Jeshi lake (Baraza Kuu) kutaka kumuangamiza Mussa na Wafuasi wake waliokua wanaamini katika Haki na Mungu wa kweli.
Kilichoendelea Zanzibar ni Mfano wa Firaun na Jeshi lake dhidi ya Mussa na Wafuasi wake.
Kauli yangu ya Mwisho ni kwamba hatoki mtu kwenye Cuf hii kwakua sio ya Mtu bali ni ya watu, sijambo jema kujifananisha na Firaun, jibu hoja usitumie Jeshi kujibu hoja. Hakuna kukataa Tamaa wala kukimbia Cuf. Harakati za kutafuta Uhuru ndani ya Cuf kwa Watanganyika ndio kwanza umezifungulia Geti, sasa ni hoja za Makabwela dhidi ya Vibaraka wa Mabepari wa Tanganyika."
Je?Kama Mussa ni Prof. Lipumba na Firauni ni Nani!
'Hakika Mfa Maji Aishi Kutapatapa......'
"SIJAMBO GENI, HATA FIRAUN ALIPOSHINDWA KUJIBU HOJA ZA MUSSA ALITUMIA JESHI
Nimekua napigiwa simu nyingi toka kwa Wanachama wenzangu na Waandishi wa habari kuhusu Taarifa zilizozagaa kwenye Mitandao. Majibu yangu ya awali Kuhusu Taarifa hizo ni
1 Moja Baraza Kuu lina Mamlaka ya kufanya hivyo kwa mujibu wa Katiba na kwa kwa kufuata Katiba jinsi inavyoeleza kwenye hizo taratibu za kuchukua hatua za Kinidhamu.
2 Mimi na wenzangu tunaotajwa kwenye kadhia hiyo ikiwa ni Pamoja na Wabunge wa Mtwara Mjini (Maftaha Nachuma) na Magdalena Sakaya Mbunge wa Jimbo la Kaliua na Diwani wa Kata ya Misima Wilayani Handeni,pamoja na wale ambao sikuwataja hatukuwepo wakati hukumu hiyo inatolewa na Baraza Kuu lilofanyika jana Mjini Unguja katika Visiwa vya Zanzibar.
3 Baada ya kuahirishwa kwa Mkutano Mkuu uliofanyika pale Ubungo Plaza Tarehe 21 /08 /2016 kutokana na Wajumbe 324 kutoridhishwa na ukiukwaji wa Katiba ya Chama chetu ikiwa ni pamoja na kuingizwa kwa Wajumbe wasio halali kwenye Mkutano Mkuu, mimi ni miongoni mwa Wajumbe tuliojiorodhesha na kuandika barua ya Malalamiko na kupeleka Ofisi ya Msajili wa Vyama.
Kutokana na Mambo hayo Matatu, nawaomba Wanacuf msifadhahike na wala msihuzunike waliotufukuza kabla hata ya kutoa majibu ya hoja zetu tulizowasilisha kwa Msajili, bila shaka hawana Majibu ya sahihi ya hoja zetu. Na jambo hili sio geni kwa hapa Duaniani, Firaun aliposhindwa kuthibitisha kua yeye ndie Mungu, alitumia Jeshi lake (Baraza Kuu) kutaka kumuangamiza Mussa na Wafuasi wake waliokua wanaamini katika Haki na Mungu wa kweli.
Kilichoendelea Zanzibar ni Mfano wa Firaun na Jeshi lake dhidi ya Mussa na Wafuasi wake.
Kauli yangu ya Mwisho ni kwamba hatoki mtu kwenye Cuf hii kwakua sio ya Mtu bali ni ya watu, sijambo jema kujifananisha na Firaun, jibu hoja usitumie Jeshi kujibu hoja. Hakuna kukataa Tamaa wala kukimbia Cuf. Harakati za kutafuta Uhuru ndani ya Cuf kwa Watanganyika ndio kwanza umezifungulia Geti, sasa ni hoja za Makabwela dhidi ya Vibaraka wa Mabepari wa Tanganyika."
Je?Kama Mussa ni Prof. Lipumba na Firauni ni Nani!
'Hakika Mfa Maji Aishi Kutapatapa......'
