Long'ututi
Member
- Dec 5, 2010
- 41
- 4
Ndugu zangu,naombeni ushauri,kweli nakiri nimekosea. Suala langu lipo hivi,mimi nilizaa na mwanamke mmoja japo sikumpenda kwani nilijipa moyo nampenda kumbe ilikuwa si kweli kwani nilikutana naye nikiwa na wawazo mengi kutokana na kuachana na mpenzi wangu wa kabla yake,niliyezaa naye huyu tuna uhusiano wa mwaka na zaidi hivi,akiwa mjamzito nikapata mwanamke niliyempenda kwa dhati,kutokana na ujana nikamvisha pete ya uchumba, naye nipo naye kwenye uhusiano yapata miezi tisa sasa,wote wanajuana na hakuna anayekubali kuachana nami,mwenye mtoto hakubali na mwenye pete anasema hawezi kubaki na pete,ndugu zake na jamaa washajua namuoa. Wote wanataka kutumia nguvu hadi za jadi nisimwache hata mmoja na najua ipo siku mambo yatakuwa makubwa sana na wote wanipenda kwa dhati japo mimi toka moyoni nampenda niliyemvisha pete ila mara zote namfikiria mwanangu ataishije bila baba? naombeni ushauri,mimi ni mkristo siwezi kuoa wake wawili,nipo tayari kurudi kwa mwenye mtoto ili niilee familia yangu ila mwenye pete naye hakubali,nifanyeje ndugu zangu?