Mapenzi yananitesa, naombeni ushauri

Dada yangu ulikuwa naye hali ukijua ana mtu mwingine nimefurahi kuwa uko tayari kumlea mwanao wala usihangaike kutoa hiyo mimba ni dhambi kubwa inayoweza kukusumbua for the rest of your life,na unajuaje kama huyo si mtoto pekee Mungu aliyekupangia chini ya jua?wala asikupe tabu lea mimba muda ukifika ukajifungua salama tunza mwanao atakupa faraja ya ajabu,fikiria kama mama yako angekutoa ungekuwa wapi?Kila mtoto anayekuja Mungu ana kusudi lake haijalishi amepatikana kwa njia gani.Blessings
 
zaa mtoto wako mwambie haya iyo mimba si yake.ili akuache kwa amani maana hakupendi hata kidogo
na kwanini umnganganie mtu jamani? wanaume waliisha au huuziki wewe?
mtu kakuambia hakutaki wewe unamganda kaa kupe,ona sasa.wanaume mbona wengi tu jamani? ushaniharibia siku wallah.ungekuwa karibu ningekuzaba kibao
Hahaha!Nitakusetia mashavu yake kabisa mkuu!Umenikosha!
 
Chukulia kama hilo ulilofanya la kumpenda asiyependeka ni kosa, lakini pia likupe funzo.
Sasa cha kufanya ni kujiamulia wewe mwenyewe. Ikiwa umeshaamua kutunza mimba na kulea mwanao, fanya hivyo. Huyo jamaa achana naye, hana haki yoyote kwa mtoto huyo na jidai kuwa huyo mtoto ni wako peke yako.... kujikwaa si kuanguka...endelea na maisha yako.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom