Mapenzi yamesababisha urafiki wetu uvunjike

Umemchukua mpenzi wang,umemzalisha na bado uko nae?lengo lako nini?unaniomba msamaha ili iweje?au unataka unizoee tena na huyu niliye nae umchukue?unadhan nitakapoona ww pamoja na Anna nitajisikiaje?siwez kukusamehe,siwez kukuamin.unazid kunipa uchungu.msijaribu kunitafuta nitawatafuna masikio yenu(in john voice)
 
Nashukuru mkuu umeelewa lengo langu ni kuomba msamaha.
Mimi sikulaumu kwa ulichofanya lakini there is no point ya kuomba msamaha.... Hapo ni kama unamkoga tu John. Potezea endeleeni na maisha yenu na Anna maana nyote wawili John hakuwa moyoni mwenu otherwise msingefanya mliofanya.
 
Nina mashaka makubwa sana na muendelezo wa maisha yenu ww na huyo Anna wakuiba huyo
 
It's not fair kwa mlichokifanya kwa nafas ya kwanza, lkn pia kwa sehemu nyingine kosa kubwa zaid ni kwa mwanamke, hakuwa wazi kwa mpenzi wake kwani inaonekana hakuwa anapenda pombe, yote kwa yote maji yamemwagika hayazoleki, tumieni marafiki zenu na wazazi au wazee kama mnao kupatana na kurejesha urafiki wenu maana maisha lazima yaendelee, muombe pia Mungu amsaidie mwenzenu apate aliyeumbiwa na Mungu kwani huyu ni wazi hakuwa wakwake japo ukweli huu kwa sasa ni mchungu kwake, mpeni muda pia kwani bado ni mapema, litakwisha.
 
Huu uzi unatia hasira,bora ungekaa kimya tu hapa umekuja washa moto uliokwisha zimika bila busara za hali ya juu hautauzima
 
mbona sijaona shida katika hili, wala john hana haja ya kunoa kisu sijui shoka ye atulie atawalipa kwa staili sawa na wao.

ilinitokea mwanamke wangu akachukuliwa na rafiki na kuzaa nae kama ivi ivi sikuwahi sema chochote huku huyu rafiki akijitetea kwamba yeye ndo alianza kumtongoza.

nikaingia kazini na mimi, nikamtongoza mdogo wa rafiki aliemtia mimba demu wangu nikamtia mimba na mimi.sikuishia hapo nikamtafuta dada wa demu wangu nae nikatia mimba, watajua wataitanaje hao watoto.

hapa niko taratibu nanyatia siku za hatari yele x wangu nae nimtie mimba.(mechi za mchangani zinaendelea)

john fanya kulipa kisasi wote tu shee maumivu,maana nakumbuka baada ya mdg wa mdogo wa rafiki yangu kujifungua na kuambiwa mtoto wangu alilalamika sana hadi kunitumia meseji (hatukuwahi kuwasilina 2yrs) akilaumu

kisasi ni lazima mambo ya kusamehe ni utoto
 
Hili jambo limewahi kunipata kwa rafiki yangu tangu tuko darasa la 3, akaja kuuvunja urafiki(undugu i can saying) rasmi mwaka 2013. Jamaa ulichomfanyia rafiki yako ningekushauri tu usije ukakaa nae karibu, muache tu na maisha yake
 
daaah demu wko kuliwa na rafiki yko inaumaa sana tena sana na kusahau ni ngumu me ilishanitokea inaelekea mwaka wa 4 sijasahau yale maumivu
 
Pole sana uliyechukuliwa mpenz,hii ni kawaida sana nafikiri haikupangwa muishi pamoja.Kwa aliyechukua mpenzi wako Anna hongera maisha lazima yaendelee ni kawaida kabisa marafiki kuchukuliana mpenzi lakini sio mke.
 
mbona sijaona shida katika hili, wala john hana haja ya kunoa kisu sijui shoka ye atulie atawalipa kwa staili sawa na wao.

ilinitokea mwanamke wangu akachukuliwa na rafiki na kuzaa nae kama ivi ivi sikuwahi sema chochote huku huyu rafiki akijitetea kwamba yeye ndo alianza kumtongoza.

nikaingia kazini na mimi, nikamtongoza mdogo wa rafiki aliemtia mimba demu wangu nikamtia mimba na mimi.sikuishia hapo nikamtafuta dada wa demu wangu nae nikatia mimba, watajua wataitanaje hao watoto.

hapa niko taratibu nanyatia siku za hatari yele x wangu nae nimtie mimba.(mechi za mchangani zinaendelea)

john fanya kulipa kisasi wote tu shee maumivu,maana nakumbuka baada ya mdg wa mdogo wa rafiki yangu kujifungua na kuambiwa mtoto wangu alilalamika sana hadi kunitumia meseji (hatukuwahi kuwasilina 2yrs) akilaumu

kisasi ni lazima mambo ya kusamehe ni utoto
Mkuu naona utaki kuruka ata jino moja
 
Wadau ni matumaini yangu kuwa wote ni wazima

Nikiwa na huzuni kubwa naandika uzi huu kwa lengo la kumuomba msamaha rafiki yangu wa utotoni na wa muda mrefu John (Ni jina lake halisi) kwa yote yaliyotokea kati yetu, kwa kauli yako ya mwisho wakati tunaongea kwenye simu ulisema hutokaa unisamehe maisha yako yote, kwa kile unachodai kuwa nimekunyang'anya mwanamke wa maisha yako, lakini kauli yako hiyo bado hainifanyi mm nisiendelee kukuomba msamaha.

Kila nikifanya Juhudi za kuonana na wewe ili tuzungumze face to face umekuwa ukikataa kuonana na mm. Najua hupo humu Jf na ukipata muda naomba soma uzi huu ili uelewe kilichotokea kati yangu na shemeji (Demu wako)

Unakumbuka mwanzoni mwa mwaka jana nilivyokuja kukusalimia ulipokuwa unaishi mwanzo Mbezi Kimara, Nilipofika kwako, baada ya stori za hapa na pale ukapendekeza tutoke home kwako twende bar moja hivi, kwa jina nimeisahau ila haikuwa mbali sana na mahali ulipokuwa unaishi.

Tukiwa njian tunaelekea kwenye ile Bar.. Ulimpigia simu shemeji ili nae aje kuungana na sisi. Kwa wasiojua ni kuwa John na Shemeji yangu walikuwa wakiishi mtaa mmoja.

Nakumbuka Baada ya kama dk 30 hivi toka tufike pale bar, shem aliwasili. Ulinitambulisha kwa shemeji, kuwa anaitwa Anna. kisha vinywaji vikaendelea. Wewe ulikuwa unakunywa Safari. Mm na Shem tukinywa Soda.

John usichokijua ni kuwa sekeseke lilianza baada ya wewe kutoka pale mezani kwenda Chooni. Tukiwa tumebaki wenyewe mezani mm na shemeji. Shemeji alivunja ukimywa kwa kuanza kunisifia kuwa kati ya rafiki zako wote uliowai kumtambulishwa, mm tu ndo ambae ameona sinywi pombe.

Aliendelea kusema naonekana mpole na mtaratibu, mwisho shemeji aliniomba namba yangu ya simu ila alinisihi sana kuwa nisikwambie ww.

So i want to make a record clear that, mm sio wa kwanza kumuomba Anna namba. Yeye ndo alianza.

Nilimpa Anna namba yangu ya simu huku nikiwa na maswali kadhaa kichwani..Kwa nn alisubiri mpaka ww uondoke mezani ndo aniombe namba? Alishindwa nn kuniomba mbele yako? Kwa nn hataki ww hujue? Lakini sikujali sana nikampa namba.

Baada ya muda kidogo ulirudi mezani na kutukuta kimya kabisa kila mtu yuko busy na simu yake kana kwamba toka uende chooni hakuna mazungumzo yoyote yaliyofanyika kati yangu na Anna.

Ulivyorudi stori zikaendelea mpaka mida ya saa tatu usiku nilipoamua kuwaaga na kuanza safari ya kurudi kwangu Kigamboni. Nilichogundua wakati wote tukiwa pale Bar, Anna alikuwa mtu wa kuniangalia sana.

Nikiwa naendesha gari narudi nyumbn.. niliwaza vitu vingi sana.. Vipi endapo ww utagundua kuwa shem ana namba yangu? Kuna wakati niliwaza nikwambie kuwa shem aliniomba namba yangu ya simu ila nikawaza utachukuliaje? Sitawagombanisha kweli?

Kwa kifupi maswali yangu yote kwa wakt ule yalikosa majibu. Nilibaki kujiambia tu moyoni ngoja nione lengo la Shemeji kuomba namba yangu kwa kificho. Nilijipa moyo wenda hana nia mbaya. Na hapo ndo nilipokosea, bora ningekwambia ukweli kuwa shem kachukua namba yangu ulivyokwenda chooni ili kama kugombana mngegombana au kama ungechukulia kawaida sawa.

Nikiwa bado nipo njiani, sms iliingia kwenye simu yangu. Kucheki ni Anna. Sms ilikuwa inasema 'it was nice meetin u shem'.. i just replied 'Thank you'.

And she was like 'Hope to see u again shem' Nikamjibu 'Wornot shem'

Siku iliyofuata nakumbuka ilikuwa Jumatatu.. Tuliendelea kuwasiliana na shem, mawasiliano yaliendelea kuimarika hadi kufikia hatua tukawa hatuwezi kulala bila kuwasiliana.

Na kwa kuwa wote, mm na Anna tulikuwa tukifanya kazi Posta tulipata muda mwingi wa kuonana. Hilo ni kosa jengine ambalo niliruhusu, lakini wakati mwengine najiambia sikuwa na kosa sababu Anna alilazimisha sana kuonana na mm. Nadhani kwa wiki nilipata muda mwingi wa kuonana nae kuliko wewe.

Kuna wakati ulimpigia simu akiwa na mm alikuwa hapokei. Nilimuuliza kwa nn hapokei simu zako hakuwa na jibu la kuridhisha alilonipa.

Sisi tukaendelea kuwasiliana asubuhi, mchna na usiku, Lakini wakati wote huu wa mawasiliano yetu, Anna alisisita sana usijue.

Ukweli kama binadamu taratibu nilijikuta naanza kumzoea Anna. Ilifika hatua Anna alikuwa hataki kuonana na ww, nilikuwa najua hilo na nilimsisitiza asifanye ivo lakini hakuwa tayari tena kuwa na ww.

Taratibu mm na Anna tukawa wapenzi.Ushemeji tukauweka pembeni.hata ile siku ambayo mligombana sana kwa sababu ulitaka akupe Password ya simu yake lakini hakufanya ivo. Anna alinieleza kila kitu. Baada ya ugomvi alikutumia sms kuomba muachane.

Nakumbuka ulinipigia simu mm na kunieleza kuwa Anna amebadilika sana na ukanitumia namba yake ukaniomba niwapatanishe. Nilikujibu kuwa 'Sawa nitafanya ivo'

Ukweli hakuna nilichoongea nae Anna. Kwa upande wetu mapenzi yalipamba moto, hadi kufikia hatua Anna akitoka kazin straight kwangu, hata kwake alikopanga mbezi alikuwa haend tena, alisema mbezi mbali na kazini kwake. Ni kama alihamia kwangu kiaina maana hata nusu ya nguo zake zilikuwa kwangu.

Kama utakumbuka, ndo mana kila ulivyokuwa ukitaka kuja kwangu nilikuwa sihishi sababu, nakujibu sipo, mara nakwambia nimesafiri kikazi.

Mapenzi yalinizidi..Mara na Anna tumekwenda Bagamoyo, Mara Mikumi, mara Movie mlimani city, mara Shopping Mkuki House. Na mambo mengine mengi.

Hatimae Anna akanitambulisha kwa mama yake. Kwa dada zake, kwa kaka zake, kwa rafiki zake.
Nakumbuka mwaka jana mwezi wa sita, Anna alishika ujauzito wangu na mwaka huu mwezi wa Pili mungu ametupatia kijana niliyempatia jina la Marehemu Baba yangu, Denis.

Kwa kipindi chote hiki nimekua mtu wa kukukimbia na kukuhepuka sio kwa sababu sitaki kuonana na ww ila kwa sababu sura yangu itashindwa kukuangalia usoni.

Juzi ulivyonipigia simu na kuanza kunitukana na kuniita msaliti na kunitishia maisha wala sikushangaaa sana, najua wapi ulipopata habari.

Juzi Anna alivyoweka picha yetu Dp whatsapp na kupost facebook, tukiwa tumembeba mtoto, nilimwambia kuwa umefanya makosa. Anna alichonijibu ni kuwa tutakuficha mpaka lini.

Kwa hiyo nataka uelewe kuwa , uhusiano wangu na Anna ulianza siku ile pale bar na sio kama unavyodhani ww kuwa, ulivyonitumia namba yake ili niwasuruhishe ndo nikamtongoza Anna. Sio hivyo hata kidogo.

Lakini yote ya yote ni kuwa makosa yalishafanyika na nakuomba msamaha. Mpaka naandika hapa tulishajadiliana na Anna na wote wawili tunakuomba msamaha na tumepanga kuja kwako kukuomba msamaha zaidi.

Ni Mm RTM
We jamaa una upungufu kichwani siyo bure aisee alaf naona wanawake umewajulia ukubwani, ur not gentleman
 
Mapenzi ni kama mpira wa miguu, usipopigiwa pasi, unaenda mwenyewe kunyang'anya mpira... Ukizembea kila siku atakuwa anashangiliwa Ronaldo tu... Hongera kwa kupata mpenzi... Mapenzi ni uselfish...
 
Back
Top Bottom