Mapenzi yamesababisha urafiki wetu uvunjike

Hiyo paragraph ya mwisho sijui umetunga hukutunga ila mie nna ushauri kwa huyu jamaa...mkuu John huyu poyoyo ikitokea akataka kuja kwako akiwa na huyo malaya mwenzake sijui Anna sijui takataka gani ita kelele za mwizi waambie jirani zako waite polisi kamata wote sema umeibiwa hela zako 10mill ulizotoa bank jana ambazo ulipanga ukanunulie kiwanja na wezi wako ndio hao ambapo huyo mwanamke mlishawahi kuwa wapenzi mkaachana so alichonga funguo kwa siri ndo unashangaa umewakuta ndani mwako.
 
Dah kaka ulichofanya jamaa lazime akasirike mana umemzunguka mpaka unampa demu mimba ulichokifanya unakijua na matokeo unayajua pia ila kwangu sitaki nikukatishe tamaa endelea kumwmba msamaha sema kua makini kama mwenzako kafanyiwa hvyo ikaja kwako its pocbo pia ukaja fanyiwa wewe pia yote kwa yote jiridhishe kama mambo yapo sawa kila la kheri katika maisha yako.
 
Wadau ni matumaini yangu kuwa wote ni wazima

Nikiwa na huzuni kubwa naandika uzi huu kwa lengo la kumuomba msamaha rafiki yangu wa utotoni na wa muda mrefu John (Ni jina lake halisi) kwa yote yaliyotokea kati yetu, kwa kauli yako ya mwisho wakati tunaongea kwenye simu ulisema hutokaa unisamehe maisha yako yote, kwa kile unachodai kuwa nimekunyang'anya mwanamke wa maisha yako, lakini kauli yako hiyo bado hainifanyi mm nisiendelee kukuomba msamaha.

Kila nikifanya Juhudi za kuonana na wewe ili tuzungumze face to face umekuwa ukikataa kuonana na mm. Najua hupo humu Jf na ukipata muda naomba soma uzi huu ili uelewe kilichotokea kati yangu na shemeji (Demu wako)

Unakumbuka mwanzoni mwa mwaka jana nilivyokuja kukusalimia ulipokuwa unaishi mwanzo Mbezi Kimara, Nilipofika kwako, baada ya stori za hapa na pale ukapendekeza tutoke home kwako twende bar moja hivi, kwa jina nimeisahau ila haikuwa mbali sana na mahali ulipokuwa unaishi.

Tukiwa njian tunaelekea kwenye ile Bar.. Ulimpigia simu shemeji ili nae aje kuungana na sisi. Kwa wasiojua ni kuwa John na Shemeji yangu walikuwa wakiishi mtaa mmoja.

Nakumbuka Baada ya kama dk 30 hivi toka tufike pale bar, shem aliwasili. Ulinitambulisha kwa shemeji, kuwa anaitwa Anna. kisha vinywaji vikaendelea. Wewe ulikuwa unakunywa Safari. Mm na Shem tukinywa Soda.

John usichokijua ni kuwa sekeseke lilianza baada ya wewe kutoka pale mezani kwenda Chooni. Tukiwa tumebaki wenyewe mezani mm na shemeji. Shemeji alivunja ukimywa kwa kuanza kunisifia kuwa kati ya rafiki zako wote uliowai kumtambulishwa, mm tu ndo ambae ameona sinywi pombe.

Aliendelea kusema naonekana mpole na mtaratibu, mwisho shemeji aliniomba namba yangu ya simu ila alinisihi sana kuwa nisikwambie ww.

So i want to make a record clear that, mm sio wa kwanza kumuomba Anna namba. Yeye ndo alianza.

Nilimpa Anna namba yangu ya simu huku nikiwa na maswali kadhaa kichwani..Kwa nn alisubiri mpaka ww uondoke mezani ndo aniombe namba? Alishindwa nn kuniomba mbele yako? Kwa nn hataki ww hujue? Lakini sikujali sana nikampa namba.

Baada ya muda kidogo ulirudi mezani na kutukuta kimya kabisa kila mtu yuko busy na simu yake kana kwamba toka uende chooni hakuna mazungumzo yoyote yaliyofanyika kati yangu na Anna.

Ulivyorudi stori zikaendelea mpaka mida ya saa tatu usiku nilipoamua kuwaaga na kuanza safari ya kurudi kwangu Kigamboni. Nilichogundua wakati wote tukiwa pale Bar, Anna alikuwa mtu wa kuniangalia sana.

Nikiwa naendesha gari narudi nyumbn.. niliwaza vitu vingi sana.. Vipi endapo ww utagundua kuwa shem ana namba yangu? Kuna wakati niliwaza nikwambie kuwa shem aliniomba namba yangu ya simu ila nikawaza utachukuliaje? Sitawagombanisha kweli?

Kwa kifupi maswali yangu yote kwa wakt ule yalikosa majibu. Nilibaki kujiambia tu moyoni ngoja nione lengo la Shemeji kuomba namba yangu kwa kificho. Nilijipa moyo wenda hana nia mbaya. Na hapo ndo nilipokosea, bora ningekwambia ukweli kuwa shem kachukua namba yangu ulivyokwenda chooni ili kama kugombana mngegombana au kama ungechukulia kawaida sawa.

Nikiwa bado nipo njiani, sms iliingia kwenye simu yangu. Kucheki ni Anna. Sms ilikuwa inasema 'it was nice meetin u shem'.. i just replied 'Thank you'.

And she was like 'Hope to see u again shem' Nikamjibu 'Wornot shem'

Siku iliyofuata nakumbuka ilikuwa Jumatatu.. Tuliendelea kuwasiliana na shem, mawasiliano yaliendelea kuimarika hadi kufikia hatua tukawa hatuwezi kulala bila kuwasiliana.

Na kwa kuwa wote, mm na Anna tulikuwa tukifanya kazi Posta tulipata muda mwingi wa kuonana. Hilo ni kosa jengine ambalo niliruhusu, lakini wakati mwengine najiambia sikuwa na kosa sababu Anna alilazimisha sana kuonana na mm. Nadhani kwa wiki nilipata muda mwingi wa kuonana nae kuliko wewe.

Kuna wakati ulimpigia simu akiwa na mm alikuwa hapokei. Nilimuuliza kwa nn hapokei simu zako hakuwa na jibu la kuridhisha alilonipa.

Sisi tukaendelea kuwasiliana asubuhi, mchna na usiku, Lakini wakati wote huu wa mawasiliano yetu, Anna alisisita sana usijue.

Ukweli kama binadamu taratibu nilijikuta naanza kumzoea Anna. Ilifika hatua Anna alikuwa hataki kuonana na ww, nilikuwa najua hilo na nilimsisitiza asifanye ivo lakini hakuwa tayari tena kuwa na ww.

Taratibu mm na Anna tukawa wapenzi.Ushemeji tukauweka pembeni.hata ile siku ambayo mligombana sana kwa sababu ulitaka akupe Password ya simu yake lakini hakufanya ivo. Anna alinieleza kila kitu. Baada ya ugomvi alikutumia sms kuomba muachane.

Nakumbuka ulinipigia simu mm na kunieleza kuwa Anna amebadilika sana na ukanitumia namba yake ukaniomba niwapatanishe. Nilikujibu kuwa 'Sawa nitafanya ivo'

Ukweli hakuna nilichoongea nae Anna. Kwa upande wetu mapenzi yalipamba moto, hadi kufikia hatua Anna akitoka kazin straight kwangu, hata kwake alikopanga mbezi alikuwa haend tena, alisema mbezi mbali na kazini kwake. Ni kama alihamia kwangu kiaina maana hata nusu ya nguo zake zilikuwa kwangu.

Kama utakumbuka, ndo mana kila ulivyokuwa ukitaka kuja kwangu nilikuwa sihishi sababu, nakujibu sipo, mara nakwambia nimesafiri kikazi.

Mapenzi yalinizidi..Mara na Anna tumekwenda Bagamoyo, Mara Mikumi, mara Movie mlimani city, mara Shopping Mkuki House. Na mambo mengine mengi.

Hatimae Anna akanitambulisha kwa mama yake. Kwa dada zake, kwa kaka zake, kwa rafiki zake.
Nakumbuka mwaka jana mwezi wa sita, Anna alishika ujauzito wangu na mwaka huu mwezi wa Pili mungu ametupatia kijana niliyempatia jina la Marehemu Baba yangu, Denis.

Kwa kipindi chote hiki nimekua mtu wa kukukimbia na kukuhepuka sio kwa sababu sitaki kuonana na ww ila kwa sababu sura yangu itashindwa kukuangalia usoni.

Juzi ulivyonipigia simu na kuanza kunitukana na kuniita msaliti na kunitishia maisha wala sikushangaaa sana, najua wapi ulipopata habari.

Juzi Anna alivyoweka picha yetu Dp whatsapp na kupost facebook, tukiwa tumembeba mtoto, nilimwambia kuwa umefanya makosa. Anna alichonijibu ni kuwa tutakuficha mpaka lini.

Kwa hiyo nataka uelewe kuwa , uhusiano wangu na Anna ulianza siku ile pale bar na sio kama unavyodhani ww kuwa, ulivyonitumia namba yake ili niwasuruhishe ndo nikamtongoza Anna. Sio hivyo hata kidogo.

Lakini yote ya yote ni kuwa makosa yalishafanyika na nakuomba msamaha. Mpaka naandika hapa tulishajadiliana na Anna na wote wawili tunakuomba msamaha na tumepanga kuja kwako kukuomba msamaha zaidi.

Ni Mm RTM

HAPA NDO UMEHARIBU KABISA, KWA NINI:

- Umemkosea sana Anna mkeo, umempa lawama zote na kuongeza uadui kati ya rafiki yako na Anna.
- Kama mwanaume ulipaswa kukabili na kupokea lawama bila kumuhusisha Anna.
- Wewe ni mbinafsi kabisa, haya alipaswa kuyajua toka zamani kabisa.
- Kuomba msamaha ndo umeharibu kabisa, there is no way nyie mtakuwa marafiki tena.
- Mind your own business!!!!
 
Yaan, we cjui niaje rafik yako kabisa ata angekuwa msela ucingefanya ivo bado tu unataka kwenda nyumban kwake kuomba msamaha, jiandae kuzinguliwa maana ulichokifanya hakisamehek ata ningekuwa mimi
 
Kiongoz nimekusoma vizuri,( ila mile sio Jon,msinitolee macho),Kiongoz ulichofanya kinaitwa double impact,yaan umepiga rungu 2 kwa mkupuo,nachomaanisha uyo jamaa yako wewe umebetray na girlfriend wake pia,aliposoma izo picha fb alijua wewe ndo mwenye makosa ilimuuma sana,ila akisoma jumbe ii atagundua girlfriend wake pia ameusika,Kiongoz stay away from that guy,wewe una roho kama ya mtu mmoja anitwa Adolf Hitler, unaua uku unaangalia usoni,..yan nimejaribu kuvaa VIATU vya mshikaj yaan bora mkae mbali tu we na mkeo,asiwajue kabisaa,stay away from that guy Mr. Coldhearted,ahsante
 
Kama unataka msamaha kwa Jonh achana na huyo mwanamke hata kama mmezaa wote. Jonh hatovumilia kamwe kuendelea kuona unaendelea kuishi na msaliti wake hata kama unamwomba msamaha. Yaani uniibie fedha zangu, umetumia zilipoisha ndo unajileta kuomba msamaha ni ngumu kukusamehe.
 
Hiyo paragraph ya mwisho sijui umetunga hukutunga ila mie nna ushauri kwa huyu jamaa...mkuu John huyu poyoyo ikitokea akataka kuja kwako akiwa na huyo malaya mwenzake sijui Anna sijui takataka gani ita kelele za mwizi waambie jirani zako waite polisi kamata wote sema umeibiwa hela zako 10mill ulizotoa bank jana ambazo ulipanga ukanunulie kiwanja na wezi wako ndio hao ambapo huyo mwanamke mlishawahi kuwa wapenzi mkaachana so alichonga funguo kwa siri ndo unashangaa umewakuta ndani mwako.
hili halitakaa vyema mkuu..kwani akisingizia wizi huenda akaulizwa kutoa ushahidi zaidi..bora aondokane na wanafiki hao vya kabisa na nyumba lake walione paa hao wanafiki
 
Kama kamsaliti John hawezi shindwa kukusaliti na wewe.

Pamoja na hayo yote, wewe makosa yako ni kuzini na sio kumsaliti rafiki yako, maana hakua mke wake huyo.

Pamoja na hayo endelea kula maisha kijana huo ndio uanaume
 
Ni zaidi ya upupu mkuu hii nikuchanganya pumba na mashudu dadekiii
Ndio umemwandikia upupwu wote wa nini, natumaini hatakusoma umetaka tu kumuumiza zaidi mwenzako. Una roho ngumu ya chuma wewe.

Na mkienda kwake awapige vibao tu na mateke kabisa.

Wewe sio mwanaume wala hufai kuwa rafiki, sasa subiri uje uyaonje wewe.

Kaa mbali naye hamna haja ya kwenda kwake wala kumtafuta ungethamini urafiki wako na yeye husingefanya yote... namba moja kuchukua simu ya wake na kunyamaza. Unaroho mbaya na tamaa ya wivu umekujaaaa.

Na akikusoma ndio akufute kabisa maishani mwake, unatia aibu.
 
Back
Top Bottom