Mapenzi yamenifikisha hapa

Mapenzi yamenifikisha hapa

ChizzoDrama

JF-Expert Member
Joined
Sep 29, 2019
Posts
1,317
Reaction score
1,235
Mambo zenu,

Nimeona tu-share experience.

Kiukweli nimelelewa katika maadili mazuri na wazazi wangu pia wakubwa wangu katika familia yetu ni watu ambao ni mifano ya kuigwa.

Ni kweli nina heshima sana kwa watu wa rika zote na ninaonekana kijana smart na miongoni mwa vijana tunaojielewa sana hapa mtaani, lakini wengi wananitizama hivyo kwakuwa nimesoma kidogo lakini sina makundi kama vijana wengine.

Mwaka 2016 niliachana na mpenzi wangu ambaye kiuhalisia ni msichana ninaye mpenda tangu utoto wangu, na hii ilikuwa baada ya yeye kwenda chuo huko mkoani Arusha ndipo ikaanza (LONG DISTANCE RELATIONSHIP). Tulienda na hiyo lakini ikafika time mapenzi yakakosa mvuto kutokana na yeye kutotaka kurudi pale alipopata likizo.

Nakumbuka nilianza kuona mabadiliko ya kimawasiliano hivyo nikaanza kujitoa taratibu ili kuepuka maumivu makali siku akiniacha. Basi nakumbuka siku moja mishale ya saa 2 usiku iliingia message ikisomeka hivi: "NAOMBA USINITAFUTE, NIPO KWENYE MAHUSIANO SERIOUS". Nilikuwa barabarani na nakumbuka niliwaza hata kujirusha ili nigongwe na gari lakini nashukuru Muumba aliniepusha na hili.

Pia nakumbuka ndiyo ilikuwa siku yangu ya kwanza kuvuta bangi. Nakumbuka machozi yalikuwa yakinitoka taratibu nikiwa njiani nikaghairi kurudi nyumbani nikaenda katika bar moja, nikaagiza vinywaji vikali kisha nilipomaliza hapo nijaenda katika vijiwe vya bhangi ambavyo obvious vinafahamika na kila mwana mtaa.

Nakumbuka nilivuta sana kisha nikarudi zangu home baada ya hapo niliamua kuishi pekee, bila ya marafiki wengi na wanawake kabisa.

Basi nikaanza tabia ya kila jioni lazima nijisogeze kwenye bar za uchochoroni kupata moja mbili, na nilikuwa naingia bar zilizojficha ili kukwepa watu wanao niona kama mtu wa maana kumbe wakati huo mimi najiona mtu nisiye na maana.

Ikawa hivyo sasa, malaya wengi wakawa katika mzunguko wangu, muda mwingi nikajikuta nalala nao hovyo hovyo. Na ama ujuavyo malaya hawanaga nongwa, leo unalala na huyu, kesho yule, mchana huyu, usiku yule. Siyo siri, watoto wanayaweza sanaa pia wanajiachia mpaka raha.

Sasa imefika wakati ngono imekuwa kama kilevi kwangu, yaani karibu kila siku lazima nifanye ngono na malaya tofauti.
Imefika wakati napenda bangi na pombe zaidi ya sana, na msimamo wangu umebaki ule ule, sihitaji marafiki.

Kiukweli stress zimenitoka kabisa siku hizi. Hata juzi kati nimekutana na huyo msichana aliyeniacha nikakuta hata sishtuki, nikampungia mkono tu kisha nikaendelea na safari zangu.

Kwa nilivyo muona, alikuwa ni mtu aliyehitaji nimpe hata dakika 5 za mazungumzo lakini haikuwa hivyo. Nilikuwa sizioni status zake za WhatsApp kwa miaka kama mitatu ila kwa kuwa mimi sikufuta namba yake najikuta nimeanza kuziona inamaanisha amei-save tena namba yangu ila angejua hata mpango wa kuwa kwenye mahusiano sina.

Pombe, ngono na bangi ni wamekuwa washkaji zangu sana. Ukiwaona hao ujue na mimi nipo.

Life Goes On by 2Pac is my one of my favorite songs ever.
Bury me smiling with Gs in my pocket
Let every rapper rock at my funeral
Let those hoes I used to know from way before
Kiss from head to my toes


Karibuni K-VANT pembeni tonic na limao, sina muda.
 
Mkuu ondoa hayo madude yote uliyoshikamana nayo..Baki na Bangi tu!
Ila usiitumie kama sehemu ya kuondolea stress bali kama dawa!

Huu ushauri unaonekana umetoka kwa mtumiaji nguli kabisa.
 
Sasa hvyo ndio vya muhimu, umechelewa sana kuvipata.

Kama kijana nakuambia shikilia hapo hapo maisha ndio haya haya tu, kikubwa tafuta mmoja akufyatulie mtoto basi.
 
Sasa hvyo ndio vya muhimu..umechelewa sana kuvipata.

Kama kijana nakuambia shikilia hapo hapo maisha ndio haya haya tu,kikubwa tafuta malaya mmoja akufyatulie mtoto basi
nimelipoke hili mkuu japo najua itakuwa ngumu ila nitajiajiri
 
Mkuu ondoa hayo madude yote uliyoshikamana nayo..Baki na Bangi tu!
Ila usiitumie kama sehemu ya kuondolea stress bali kama dawa!
duuh ! Niombee tu maana sina wazo bado
 
Yaani mkuu mdada mmoja tu kakuvuruga umetoka kabisa kwenye rait traki ya maisha, kaka?

Sasa unasema kwa jinsi ulivyomuona bidada ni kama alihitaji dakika 5 mzungumze kidogo, nahisi ungempa tu. Kwa hali ilivyo, wewe ndio unahitaji msaada zaidi wa kisaikolojia mkuu.

Maisha ya bangi, pombe na malaya ni combination mbaya mkuu. Hiyo combination itakuletea shida mwisho wa siku.
 
Yaani mkuu mdada mmoja Tu kakuvuruga umetoka kabisa kwenye'lait traki' ya maisha Kaka?

Sasa unasema Kwa jinsi ulivyomuona bidada ni Kama alihitaji dakika 5 mzungumze kidogo, nahisi ungempa Tu. Kwa Hali ilivyo wewe ndio unahitaji msaada zaidi wa kisaikolojia mkuu.

Maisha ya bangi, pombe na Malaya ni combination mbaya mkuu. Hiyo combination itakuletea shida mwisho wa siku.
Mkuu nadhàni MOYO ungekuwa transparent tusinge umizana, yule binti nilimpenda isivyo kawaida ila nadhani kuna kitu alihitaji zaidi ya nilivyo muhitaji.

Maisha ikabidi yaendelee tu.
 
Mzae hii noma kunywa pombe acha na wasupa wako infected kunywa pombe kiasi tafuta demu fvcke mate mukulane poa achana hizo prostitute
 
Okkk....maisha ni kuchagua....na iko wazi matokea ya kila kitu yanajulikana.
Kwahiyo kama unaona hiyo tabia ndo solution ya kuachwa basi ujiandae na matokeo yake.
 
Moja ndo inakufanya hvyo duuh we jamaa unapenda vibaya.
Anyway karibu ulevini
 
Kuachwa na demu mmoja tu ndio umepaniki hivyo mkuu?

Ukiona wengine tuna demu zaidi ya mmoja ujue ni sababu ya kukwepa kadhia kama yako, ukiachwa na mmoja yupo mwingine anakushikilia.
 
Maisha ni kuchagua, unapochagua hakikisha mbeleni huna majuto.
 
Back
Top Bottom