Melki the Storyteller
JF-Expert Member
- May 3, 2022
- 5,700
- 9,778
"Ndio maana ikatokea huko kwenye mahusiano na mwanaume, halafu ukampigia simu akutumie hata elfu kumi, utamsikia akisema, njoo nyumbani kwangu uchukue",alisikika mwanadada mmoja akizungumza kwa hisia kali!
Aliendelea kuzungumza," hata utakapoamua kwenda kwake ataishia kukushawishi mfanye mapenzi ndipo akupatie hiyo pesa! Wanaume wamefanya wanawake tukariri kuwa kwa sasa hakuna mahusiano ya kimapenzi, kupendana kama ilivyokuwa zamani, badala yake tunafanya biashara ya ngono japo iliyostaarabika!"
Alitazama chini kwa muda wa nusu dakika kisha aliendelea kusema, "kwa sasa wanaume mmekuwa vitega uchumi vyetu! pale tutakapokuwa na shida na pesa, simu zitakuwa nyingi!
Na ndiyo maana baada ya tendo tutakaa mkao wa ngoja nione leo ntaondoka na kiasi gani! Wanaume wale wa nitumie pesa akakuuliza nikutumie kwa namba hii au, hawapo tena! Kama mtu ungelibahatisha mtu kama huyo, hata kama angelikuhitaji, ukaenda na asikupatie pesa siku hiyo, usingelahum, kwa sababu ni mtoaji! Mapenzi ya sasa hakuna kutongozana tena kwa maneno, bali pesa inaongea tu!
Wingi wa pesa ndio unaharakisha zoezi zima la kufanya mapenzi! Waoaji hawapo siku hizi, bali kuna wabebeshaji mimba! Hapo kuna mawili, mimba hiyo ailee ama aikimbie! Wanaume waaminifu wamekwisha, siku hizi hakuna ndoa, bali kuna njoo tuishi pamoja kwa muda!"
Alifuta machozi, akaendelea kusema,"Hakuna mwanaume wa mwanamke mmoja kwa sasa, hilo wanawake wote tunalitambua, lakini mada inakuja ni jinsi gani mwanaume huyo ana behave mbele yako? Mwanaume wa kibongo atakapopata hawala, ataanzisha dharau ndani ya nyumba! Ni bora mwanaume utafute michepuko mingi kadri uwezavyo, lakini heshima ndani ya nyumba iwemo! Itapendeza zaidi kama utaweka akili yako sawa kujua mimi ni nani na nina nafasi gani katika maisha yako"
Mazungumzo yake yalimalizikia pale huku yakisindikizwa na machozi yaliyoambatana na kwikwi! Ndipo nikachukua wasaa wa kutubu na kujutia makosa yangu pasi na kujibiwa neno lolote! Nikaishia kumkumbatia na kushtuka usingizini!
Aliendelea kuzungumza," hata utakapoamua kwenda kwake ataishia kukushawishi mfanye mapenzi ndipo akupatie hiyo pesa! Wanaume wamefanya wanawake tukariri kuwa kwa sasa hakuna mahusiano ya kimapenzi, kupendana kama ilivyokuwa zamani, badala yake tunafanya biashara ya ngono japo iliyostaarabika!"
Alitazama chini kwa muda wa nusu dakika kisha aliendelea kusema, "kwa sasa wanaume mmekuwa vitega uchumi vyetu! pale tutakapokuwa na shida na pesa, simu zitakuwa nyingi!
Na ndiyo maana baada ya tendo tutakaa mkao wa ngoja nione leo ntaondoka na kiasi gani! Wanaume wale wa nitumie pesa akakuuliza nikutumie kwa namba hii au, hawapo tena! Kama mtu ungelibahatisha mtu kama huyo, hata kama angelikuhitaji, ukaenda na asikupatie pesa siku hiyo, usingelahum, kwa sababu ni mtoaji! Mapenzi ya sasa hakuna kutongozana tena kwa maneno, bali pesa inaongea tu!
Wingi wa pesa ndio unaharakisha zoezi zima la kufanya mapenzi! Waoaji hawapo siku hizi, bali kuna wabebeshaji mimba! Hapo kuna mawili, mimba hiyo ailee ama aikimbie! Wanaume waaminifu wamekwisha, siku hizi hakuna ndoa, bali kuna njoo tuishi pamoja kwa muda!"
Alifuta machozi, akaendelea kusema,"Hakuna mwanaume wa mwanamke mmoja kwa sasa, hilo wanawake wote tunalitambua, lakini mada inakuja ni jinsi gani mwanaume huyo ana behave mbele yako? Mwanaume wa kibongo atakapopata hawala, ataanzisha dharau ndani ya nyumba! Ni bora mwanaume utafute michepuko mingi kadri uwezavyo, lakini heshima ndani ya nyumba iwemo! Itapendeza zaidi kama utaweka akili yako sawa kujua mimi ni nani na nina nafasi gani katika maisha yako"
Mazungumzo yake yalimalizikia pale huku yakisindikizwa na machozi yaliyoambatana na kwikwi! Ndipo nikachukua wasaa wa kutubu na kujutia makosa yangu pasi na kujibiwa neno lolote! Nikaishia kumkumbatia na kushtuka usingizini!