Mapenzi ya kweli yapo jamani

Mapenzi ya kweli yapo jamani

prettydiva

Senior Member
Joined
Feb 19, 2014
Posts
101
Reaction score
39
Habari wana jamvi...kuna siku niliwah kupost kuhusu kuwa na jamaa ambaye nlmpenda lakin yeye hakuwa na mapenzi ya kweli kwangu.Leo nmekuja kwenu kuwashuhudia kuwa wapo wanaume wenye mapenzi ya kweli na wenye kujua thamani ya mwanamke,kuna kijana nipo nae kwa sasa ambaye alionyesha kunipenda toka tuko wote chuo kikuu japo tulikuwa kozi tofauti hakuonyesha kuchoka kunipenda n hata nlipokuwa naumizwa na maisha yeye alikuwa nami kwa zaidi ya miaka miwili alinivumilia,hakupenda aone machozi yangu lakini mimi sikuwa tayari kumpa moyo wangu.Toka nimpe moyo wangu amekuwa furaha kwangu,yan ananijali hadi nashangaa nlkuwa wapi siku zote,ananipa chochote hata bila kuomba nami zawadi kubwa ni kumpa penzi la dhati na la kweli. USHAURI: Wasichana mnaotendwa kwenye mapenzi msife moyo ipo siku mtakutana na wanaume sahihi kwa maisha yenu,endeleeni kuomba Mungu.
 
Hongera, mpe akugegede vya kutosha akikuchoka usije ukatulilia

Habari wana jamvi...kuna siku niliwah kupost kuhusu kuwa na jamaa ambaye nlmpenda lakin yeye hakuwa na mapenzi ya kweli kwangu.Leo nmekuja kwenu kuwashuhudia kuwa wapo wanaume wenye mapenzi ya kweli na wenye kujua thamani ya mwanamke,kuna kijana nipo nae kwa sasa ambaye alionyesha kunipenda toka tuko wote chuo kikuu japo tulikuwa kozi tofauti hakuonyesha kuchoka kunipenda n hata nlipokuwa naumizwa na maisha yeye alikuwa nami kwa zaidi ya miaka miwili alinivumilia,hakupenda aone machozi yangu lakini mimi sikuwa tayari kumpa moyo wangu.Toka nimpe moyo wangu amekuwa furaha kwangu,yan ananijali hadi nashangaa nlkuwa wapi siku zote,ananipa chochote hata bila kuomba nami zawadi kubwa ni kumpa penzi la dhati na la kweli. USHAURI: Wasichana mnaotendwa kwenye mapenzi msife moyo ipo siku mtakutana na wanaume sahihi kwa maisha yenu,endeleeni kuomba Mungu.
 
^^
May be its a Perfect Match- Congrats lady
^^
 
Kwa sasa furahia mamy,upepo ukigeuka vumilia maana!!!!
Wanaume wengi ni Simba wanajua wanachowinda!
 
Mwanzoni mapenzi huwa matamu hivyo hivyo na asilimia kubwa huwa tunajiuliza kwanini hatukukutana mapema
 
Kupenda unakokuzungumzia wewe ni kupi?

Kupenda hakuwezi kupimwa kwa wiki moja au mbili au mwaka au miaka

Kipimo cha kupenda ni hadi pale utakapokuja kufa

Lakini sio kufa tu bali kujua kama alikupenda kwa maana ya kupenda

Kupenda kuna maana ya kuheshimiana

Kuheshimiana kunakuja pamoja na kuthaminiana

Yote hayo hayapimwi kwa kupewa gari au kurudi nyumbani mapema

Kipimo cha hayo ni maisha yenu yote!
 
Yote kwa yote endelea kumuomba mungu mnavoishi ss muishi ivo ad kifo kiwatenganishe.
 
Homa ya penzi jipya dada hilo bado hujajua kama unampenda au laa, mim huwa naiogopa sana homa hiyo manaake hufanya wapenzi wawe kama watoto, sasa ukija kupona homa hiyo ndio utajua kama umempenda
 
prettydiva mapenzi ya kweli yapoje?? Je mko in relation kwa miaka mingapi?
 
Last edited by a moderator:
Toba weeee ushapenda Mara hii tna jaman mmmmh

Tulia mdogo wangu ungechukua holiday na kutokuwa na mpenz kwa mda

Mapenz mapya lazima yawe matamu....
Wewe una moyo wa maumivu ndo mana unaona huyu ndo rty person...
 
Umeandika kama teen anayeingia katika ulimwengu wa mapenzi... Ngoja atafune hiyo cookie akinai, tunasubiria mrejesho!!!
 
hivi wanaume huwajui eeeh! utashangaa siku ya siku anakuwa kama nyati!
 
Back
Top Bottom