Mapenzi na uungwana..................wanaume tuonyeshe mfano.

The Boss

JF-Expert Member
Aug 18, 2009
49,110
115,885
Mimi nafikiri wakati mwingine ni bora
kila mtu kabla hujaanza kuingia kwenye mapenzi
na mtu ni bora kujua kwamba,
masuala ya kugombana na kupata maudhi kwenye mapenzi
ni mambo ya kutegemea na kutarajia......kilicho cha maana
ni wewe mwenyewe kujifunza namna ya ku deal na ugomvi
na maudhi yanayokuja na mapenzi.....it is part of any relationship.....

Sasa basi cha kushangaza ni kuwa wapo watu wakiwa na ugomvi
kidogo na wapenzi wao ni aibu tupu......
Yaaani aibu mpaka kwa majirani au wapita njia.........
Wengine ugomvi mpaka watu wanajaa kuwasikiliza na ukikuta
yanayozungumzwa ni aibu ,aibu aibu........

Pamoja na yote mimi naamini mwanaume ukiwa na msimamo na unajua
kum handle mwenzio tangu mwanzo mambo mengi yasio faa yanaweza ku epukwa.....
Hivi ni lazima watu wazima mfokeane mbele ya watoto????
Au ugomvi mpaka majirani wanakuja kuwaamua??????
Utakuta mtu anajaribu kumtukana mpenzi wake mbele ya watu as if
na yeye hajitukani kwa ujinga wake.....

Mimi huwa naona watu kama mmechokana ni bora kuachana kwa heri bila ugomvi
na sio unakuta watu wazima,shule wameenda,pesa wanayo lakini
ikifika jioni ni ugomvi,ugomvi mpaka wapita njia wanasimama kufaidi sinema ya bure...

Ni kweli wanawake wana maudhi sana.but mwanaume ukiwa mstaarabu
matatizo mengine yanaepukika........
Tusisahau nobody is perfect...........................................
 
Kugombana ni part and parcel ya wapendanao lakini kugombana mbele ya kadamnasi ni aibu tupu hata kama hamtukanani matusi ya nguoni. Hata siku moja sitapoteza muda wangu wa kujibizana na nimpendaye kama hatuwezi kuongea kiustaarabu ili kumaliza matatizo yaliyokuwepo basi nitaingia mitini maana mtu anayebwata kwa sauti kubwa mpaka utui wa mdomo unamtoka na hakupi nafasi hata ya kutia neno mimi siwezi kuelewana naye ni bora kumuacha abwate mwenyewe na akishatulia tutaongea kiustaarabu. Je, na wale Wanaume wanaopiga wanawake zao kwa sababu ambazo hata haziingii akilini huwa wanafikiria nini hasa hadi kuwapa mikong'oto ya kutisha Wapenzi wao?
 
kumpiga mpenzi wako ni kujidhalilisha na kumdhalilisha mwenzio...........
 
ni kweli mara nyingi wanawake wanapenda sana kuongea....lkn ni vizuri vitu vikawa vinajadiliwa taratibu kwa masikilizano watu waelewane lakini uatakuta mwanamke hapewi nafasi ya kuongea.....mbabe anataka atakachoongea yeye ndo kiwe hicho hicho....hata kam kosa lake hv nanai atakubali hapo.....lazima marumbano yatokee lakini hata kama mtu unahasira vip jaribu kucontrol hasira zako lakini sio kutukanana mbele ya kadamnasi....na kupigana ni aibu tupu.....au unapomtukana mwenzako matusi ya nguoni mbele za wtu unajidhalilish awewe mwenyewe na huyo unaemtukana......thanx sana kwa alie anzisha hii topic i wish i can say more....lakin i can't.....
 
ni kweli mara nyingi wanawake wanapenda sana kuongea....lkn ni vizuri vitu vikawa vinajadiliwa taratibu kwa masikilizano watu waelewane lakini uatakuta mwanamke hapewi nafasi ya kuongea.....mbabe anataka atakachoongea yeye ndo kiwe hicho hicho....hata kam kosa lake hv nanai atakubali hapo.....lazima marumbano yatokee lakini hata kama mtu unahasira vip jaribu kucontrol hasira zako lakini sio kutukanana mbele ya kadamnasi....na kupigana ni aibu tupu.....au unapomtukana mwenzako matusi ya nguoni mbele za wtu unajidhalilish awewe mwenyewe na huyo unaemtukana......thanx sana kwa alie anzisha hii topic i wish i can say more....lakin i can't.....


why not?
Ongea vyote.........
 
Duh lakini wadada ndio mara nyingi hawana simile, bomba likipasuka wanatoa mpaka mambo ya sirini
 
Dawa ya moto ni maji - mwenzako akipanda juu sana kwa maneno (kama moto) inabidi the other partner ashuke na kunyamaza kimya (kama maji) - hapo mtu kuongea mwenyewe mwisho ataona aibu na kunyamaza -hatimaye hasira zikimwisha muda wa maongezi utakuwepo.

Ndio maana Bible inasema katika kitabu cha Mithali "HASIRA HUKAA KIFUANI MWA MPUMBAVU"
na Msemo wa Kiingereza ambao ni common unasema "NEVER URGE WITH A FOOL, PEOPLE MIGHT NOT NOTICE THE DIFFERENCE"
 
Mimi nafikiri wakati mwingine ni bora
kila mtu kabla hujaanza kuingia kwenye mapenzi
na mtu ni bora kujua kwamba,
masuala ya kugombana na kupata maudhi kwenye mapenzi
ni mambo ya kutegemea na kutarajia......kilicho cha maana
ni wewe mwenyewe kujifunza namna ya ku deal na ugomvi
na maudhi yanayokuja na mapenzi.....it is part of any relationship.....

Sasa basi cha kushangaza ni kuwa wapo watu wakiwa na ugomvi
kidogo na wapenzi wao ni aibu tupu......
Yaaani aibu mpaka kwa majirani au wapita njia.........
Wengine ugomvi mpaka watu wanajaa kuwasikiliza na ukikuta
yanayozungumzwa ni aibu ,aibu aibu........

Pamoja na yote mimi naamini mwanaume ukiwa na msimamo na unajua
kum handle mwenzio tangu mwanzo mambo mengi yasio faa yanaweza ku epukwa.....
Hivi ni lazima watu wazima mfokeane mbele ya watoto????
Au ugomvi mpaka majirani wanakuja kuwaamua??????
Utakuta mtu anajaribu kumtukana mpenzi wake mbele ya watu as if
na yeye hajitukani kwa ujinga wake.....

Mimi huwa naona watu kama mmechokana ni bora kuachana kwa heri bila ugomvi
na sio unakuta watu wazima,shule wameenda,pesa wanayo lakini
ikifika jioni ni ugomvi,ugomvi mpaka wapita njia wanasimama kufaidi sinema ya bure...

Ni kweli wanawake wana maudhi sana.but mwanaume ukiwa mstaarabu
matatizo mengine yanaepukika........
Tusisahau nobody is perfect...........................................


Ni kweli kabisa hapa wanaume ndio tunaotakiwa kuwa wastaarabu zaidi. Kama ambavyo amani isivyo nunuliwa ni kwa struggle ndivyo yalivyo mapenzi. Wapenzi wanapozidi kukosoana na kusameheana ndivyo penzi linavyozidi kustawi.
 
Kuna mwanamke mmoja alikuta Condom kwenywe mfuko wa suruali ya mmewe badala ya kumuulizia huko huko chumbani akabeba Condoms zake na kwenda nje analia baba fulani ndo nini hiki yaani unataka kuniua huku kaning'iniza hiyo zana majirani kuanza kujaa tele ..mme alichofanya alimvutia ndani na kuanza kumpa kipigo cha mbwa mwizi.. bila ya kutoa maelezo ya Condoms
mie nilicheka sana na kujiuliza Condoms kakuta ndani akiwa chumbani nini kilimtuma kutoka nje na kuanza kupiga mayowe?
 
Ustarabu ni kitu kigumu sana na inategemea mtu hasira zako ziko je... Kama unalipuka ni ngumu kuwa muangalifu wa kelele na uko wapi... Laiki kujifunza PATIENCE is very important mtaishia wote kuonekana wajinga na wenye tabia za kitoto mbele ya watu...
 
Akina Mama jamani, hata mkiwa chumbani sometimes ukipigiwa simu tu ya ofisini na mfanyakazi mwenzio wa ofisi akiwa wa kike ni nongwa oooh kwa nini akupigie wewe tu? km ni boss wako utafanyeje? basi hapo kelele tuu mwanamke wako huyooo, mara oooh mnajuana kuweni na simile basi tusikilizeni kwanza
 
Mimi sidhani kama mafahali wawili wanaweza kukaa zizi moja... na siku zote mwanamke mwenye busara hawezi kujibizana na mwanaume (au mtu yeyote) mbele ya kadamnasi. Kama alivyosema Preacher hapo juu, hapa busara inahitajika zaidi.
 
ni kweli mara nyingi wanawake wanapenda sana kuongea....lkn ni vizuri vitu vikawa vinajadiliwa taratibu kwa masikilizano watu waelewane lakini uatakuta mwanamke hapewi nafasi ya kuongea.....mbabe anataka atakachoongea yeye ndo kiwe hicho hicho....hata kam kosa lake hv nanai atakubali hapo.....lazima marumbano yatokee lakini hata kama mtu unahasira vip jaribu kucontrol hasira zako lakini sio kutukanana mbele ya kadamnasi....na kupigana ni aibu tupu.....au unapomtukana mwenzako matusi ya nguoni mbele za wtu unajidhalilish awewe mwenyewe na huyo unaemtukana......thanx sana kwa alie anzisha hii topic i wish i can say more....lakin i can't.....

bibie umesema kweli.....wanawake kwa ngonjera hawajambo..ila kwa vile tuu wangu nampenda sana ndo maana naweza kuvumilia maneno ila hatubigani wala kutukanana ni majibishano yakawaida....
hivi hadi leo kuna wanandoa tena wasomi wanaweza kweli kutoa matusi au kutukana dhidi ya wapenzi wao mbele ya kadamnasi....mimi sijaona hayo mambo muda mrefu sasa....
hata mbele ya watoto wangu naogopa sana kumgombeza mama yao...kama baba lazima nionyeshe mfano mzuri ili watoto waweze kujifunza kutoka kwetu
vkeisy2006...sema yote uliyonayo moyoni...
 
@the boss, kuna baadhi ya makabila mwanamke asipopigwa na mpenzi wake atalalamika kuwa mpenzi wake ampendi na isitoshe atadai talaka, ila kwa mimi hiyo kitu siipend na ninamwomba Mungu aninusuru na hilo kabisa
 
kuna mwanamke mmoja alikuta condom kwenywe mfuko wa suruali ya mmewe badala ya kumuulizia huko huko chumbani akabeba condoms zake na kwenda nje analia baba fulani ndo nini hiki yaani unataka kuniua huku kaning'iniza hiyo zana majirani kuanza kujaa tele ..mme alichofanya alimvutia ndani na kuanza kumpa kipigo cha mbwa mwizi.. Bila ya kutoa maelezo ya condoms
mie nilicheka sana na kujiuliza condoms kakuta ndani akiwa chumbani nini kilimtuma kutoka nje na kuanza kupiga mayowe?


wanawake wengine vipigo hutafuta wenyewe...
 
But mgogoro ni muhimu kwenye mahusiano coz inahusisha pande mbili zilizo na maslahi yanayogongana .Cha msingi ni heshima,kama watu wanaheshimiana basi pia njia yao ya kutatua matatizo itakuwa ya kulindiana hashima
 
Akina Mama jamani, hata mkiwa chumbani sometimes ukipigiwa simu tu ya ofisini na mfanyakazi mwenzio wa ofisi akiwa wa kike ni nongwa oooh kwa nini akupigie wewe tu? km ni boss wako utafanyeje? basi hapo kelele tuu mwanamke wako huyooo, mara oooh mnajuana kuweni na simile basi tusikilizeni kwanza

huyo mwanamke ina maana yeye hapigiwi simu na mwanaume yeyote isipokuwa mpenziwe au ndugu yake?
 
teh teh teh duh!!!! huyo mwanamke kweli hazimtoshi yaani kapatwa na atizo akiwa ndani akaenda kulilia nje??????????????? hakuwa na machungu yoyote bali aliamua kumdhalilisha tuu mumewe,
 
My secret weapon has always been silence. Silence is golden and divine. Lkn jamani kuna wale wanaitwa drama queens and kings na kugombana hadharani ni kawaida, na wala hawana cha aibu. Ustarabu comes from within not without, and you cannot teach somebody.
 
Back
Top Bottom