mtwa mkulu
JF-Expert Member
- Sep 11, 2013
- 8,098
- 9,994
Wakuu kama tulivyo shuhudia siku za hivi karibuni chama cha Mapinduzi kimejikita katika dhana ya utendaji zaidi huku wenzetu wa upande wapili wakijikita katika kupinga tuu japo wakati huu hawana hoja sana kwa vile hakuna events nyingi kama awamu nyingine. Hata huko katika mitandao ya kijamii wanao pinga na kukubali sera za chama wamekuwa na mikinzano mikali kiasi kwamba ni ngumu kubashiri nani anazidi kwa wingi tofauti na ule utawala dhaifu kama alivyo sema kamanda mnyika.
Kuna umuhimu mkubwa sana wa kubadili kikosi kazi cha chama ili ziwepo sura mpya na yafuatayo ni mapendekezo yangu kwa nafasi mbili tu ambazo zikitiliwa mkazo chama kitakuwa kipya na hatari. Unaruhusiwa kuadd mapendekezo yako kwakuwa kwapamoja tunaijenga CCM mpya.
KATIBU MKUU WA CHAMA; Ndugu Humphrey Pole pole
Kada kindaki ndaki wa chama msafi asiye na hata chembe ya dhuruma moyoni mwake muumini wa sera na falsafa za mwalimu Nyerere. Kwapendekezo langu Kinana amefanya kazi nzuri kwa maana kuwa kama akiondolewa ni ili apumzike tuu na kushauri damu changa zipige kazi. Pole pole ameshindwa kuwa katibu wa itikadi na uenezi katika jukumu la kukizungumzia chama lakini amefanikiwa sana kuwa na mikakati na mbinu kiasi kwamba kwa siku za hivi karibuni amekibeba chama. Nashauri kwa maoni yangu ni muda wa kada huyu kuwa katibu wa chama.
ITIKADI NA UENEZI; Jery Muro
Kwa mtazamo wangu huyu mwanamume asiye na hata chembe la woga moyoni mwake anafaa kutwaa hii nafasi.. Anaweza kujenga hoja na kukizungumzia chama. Ni rasilimali adhimu ambayo tumeiweka pending. Tukumbuke kuwa siku za hivi karibuni Mwanamume huyu amekuwa akiandaa makombora ambayo kwakweli yanawanyima usingizi ndugu zetu wa ng'ambo ya pili.... amekuwa akijibu pumba zao kwa weredi wa hali ya juu kiasi cha kuwakosesha hata cha kusema hawa mabwana
Naamini kwa kuweka vichwa hivi viwili tutafika mbali. Mungu ibariki Tanzania Mungu ibariki CCM
Kuna umuhimu mkubwa sana wa kubadili kikosi kazi cha chama ili ziwepo sura mpya na yafuatayo ni mapendekezo yangu kwa nafasi mbili tu ambazo zikitiliwa mkazo chama kitakuwa kipya na hatari. Unaruhusiwa kuadd mapendekezo yako kwakuwa kwapamoja tunaijenga CCM mpya.
KATIBU MKUU WA CHAMA; Ndugu Humphrey Pole pole
Kada kindaki ndaki wa chama msafi asiye na hata chembe ya dhuruma moyoni mwake muumini wa sera na falsafa za mwalimu Nyerere. Kwapendekezo langu Kinana amefanya kazi nzuri kwa maana kuwa kama akiondolewa ni ili apumzike tuu na kushauri damu changa zipige kazi. Pole pole ameshindwa kuwa katibu wa itikadi na uenezi katika jukumu la kukizungumzia chama lakini amefanikiwa sana kuwa na mikakati na mbinu kiasi kwamba kwa siku za hivi karibuni amekibeba chama. Nashauri kwa maoni yangu ni muda wa kada huyu kuwa katibu wa chama.
ITIKADI NA UENEZI; Jery Muro
Kwa mtazamo wangu huyu mwanamume asiye na hata chembe la woga moyoni mwake anafaa kutwaa hii nafasi.. Anaweza kujenga hoja na kukizungumzia chama. Ni rasilimali adhimu ambayo tumeiweka pending. Tukumbuke kuwa siku za hivi karibuni Mwanamume huyu amekuwa akiandaa makombora ambayo kwakweli yanawanyima usingizi ndugu zetu wa ng'ambo ya pili.... amekuwa akijibu pumba zao kwa weredi wa hali ya juu kiasi cha kuwakosesha hata cha kusema hawa mabwana
Naamini kwa kuweka vichwa hivi viwili tutafika mbali. Mungu ibariki Tanzania Mungu ibariki CCM