rebeccamrema
JF-Expert Member
- Oct 3, 2014
- 334
- 196
hamna panic hapa!kitaeleweka tuu, hata kama ripoti haina kitu!tutakitengeneza kinacholingana na ukweli halisi
haaahaa kinacholingana na uongo halisi poleni sana
hamna panic hapa!kitaeleweka tuu, hata kama ripoti haina kitu!tutakitengeneza kinacholingana na ukweli halisi
kipi kimfanye apanic wanaume wamekesha kulinda ripoti original isiibiwe na majambazi ya ccm wewe unaleta ngonjera hapa. Tulia acha mbwembwe
Sio wafilisiwe tu wanyongwe kabisa watu wanawalisha sumu wenzao kuwazoofisha na kuwauwa nao wakikamatwa kitanzi hadharani tu
kwanza chanzo chenye cha habari ni chaga typ:teeth: yan walewale wapigaji!!!MWENYEKITI wa Kamati ya Bunge ya Hesabu za Serikali(PAC),Zitto Kabwe, amesema kamati yake itatoa hoja ya kuanza mchakato wa kikatiba wa kumvua ujaji, Mwanasheria Mkuu wa Tanzania, jaji Frederick Werema.
Mbali na dhamira ya kutaka jaji Werema avuliwe ujaji pia, Zitto amesema kamati yake itapendekeza watu wote waliohusika katika kashfa ya wizi wa akaunti ya Tegeta Escrow, wachukuliwe hatua za kisheria ikiwa ni pamoja na kufilisiwa mali zao.
Zitto, alitoa kauli hiyo jana alipozungumza na Tanzania Daima Jumapili, kuhusu sakata la Escrow linaloendelea hivi sasa.
Majibu ya Zitto yalitokana na maswali ya gazeti hili yaliyotaka kujua hatua zitakazopendekezwa na kamati yake baada ya kukamilisha kazi ya kupitia ripoti ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Serikali(CAG), juu ya akaunti ya Tegeta Escrow.
Alisema kimsingi kilichofanyika katika tukio hilo ni zaidi ya wizi wa kawaida na kwamba wahusika ni vema wakafilisiwa mali zao kisha wachukuliwe hatua nyingine za kisheria.
Suala hili sio wizi wa kawaida bali ni money laundering. Kwa hiyo kufilisiwa ili kurejesha fedha hizo ni hatua nyingine itakayopendekezwaalisema Zitto.
Alisema hatua hiyo itakuwa ni fundisho kwa wengine huku akikumbushia matukio ya wizi wa fedha za Akaunti ya Malipo ya Madeni ya Nje(EPA) na sakata la kampuni ya kufua umeme wa Richmond.
Alisema kamati yake bado inaendelea na kazi na kwamba walichogundua ni kuwa fedha zilizokuwa katika akaunti ya Tegeta Escrow zilikuwa za umma na kwamba kampuni ya Pan Africa Power Resources (PAP) hawakuwa na uhalali wa kuchukua fedha hizo.
PAC bado inaendelea na kazi. Watu wote ambao wamehusika katika wizi huu tutapendekeza wawajibishwe na kuchukuliwa hatua za kisheria.alisema
Tishio kwa wabunge
Baadhi ya wabunge wanaonekana vinara wa kusimamia suala hilo wanaelezwa kutishia maisha ambapo mbunge wa Kigoma Kusini, David Kafulila, ameshatoa ripoti polisi
Wasiwasi wa usalama wa wabunge hao umeongezeka zaidi baada ya taarifa kuwa mbunge wa Musoma Vijijini, Nimrod Mkono (CCM), kulishwa sumu akiwa safarini nchini Uingereza
Mkono inadaiwa ndiye anayejua sakata la IPTL kwakuwa kwa muda mrefu amekuwa akishiriki kwenye kesi akisimamia Tanesco na wizara ya Nishati na Madini
Mbunge huyo anadaiwa kuvujisha siri ya uchotwaji wa fedha hizo kwakuwa Wizara ya Nishati na Madini mwanzoni mwa mwaka huu haikuingia makataba wa kuitumia kampuni ya uwakili ya mbunge huyo
Hata hivyo Mkono, mwenyewe mara kadhaa alishakanusha madai ya kushiriki kwenye kuvujisha siri za ufisadi huo wala kuwa nyuma ya sakata hilo.
Chanzo: Tanzania daima
na wataumbuka kweli wajinga sana wanaendekeza njaa tuu zisizo na maana alafu wanajiita wazalendosawa dada nimetulia nasubiri kuona mnavyoumbuka na bado
MWENYEKITI wa Kamati ya Bunge ya Hesabu za Serikali(PAC),Zitto Kabwe, amesema kamati yake itatoa hoja ya kuanza mchakato wa kikatiba wa kumvua ujaji, Mwanasheria Mkuu wa Tanzania, jaji Frederick Werema.
Mbali na dhamira ya kutaka jaji Werema avuliwe ujaji pia, Zitto amesema kamati yake itapendekeza watu wote waliohusika katika kashfa ya wizi wa akaunti ya Tegeta Escrow, wachukuliwe hatua za kisheria ikiwa ni pamoja na kufilisiwa mali zao.
Zitto, alitoa kauli hiyo jana alipozungumza na Tanzania Daima Jumapili, kuhusu sakata la Escrow linaloendelea hivi sasa.
Majibu ya Zitto yalitokana na maswali ya gazeti hili yaliyotaka kujua hatua zitakazopendekezwa na kamati yake baada ya kukamilisha kazi ya kupitia ripoti ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Serikali(CAG), juu ya akaunti ya Tegeta Escrow.
Alisema kimsingi kilichofanyika katika tukio hilo ni zaidi ya wizi wa kawaida na kwamba wahusika ni vema wakafilisiwa mali zao kisha wachukuliwe hatua nyingine za kisheria.
Suala hili sio wizi wa kawaida bali ni money laundering. Kwa hiyo kufilisiwa ili kurejesha fedha hizo ni hatua nyingine itakayopendekezwaalisema Zitto.
Alisema hatua hiyo itakuwa ni fundisho kwa wengine huku akikumbushia matukio ya wizi wa fedha za Akaunti ya Malipo ya Madeni ya Nje(EPA) na sakata la kampuni ya kufua umeme wa Richmond.
Alisema kamati yake bado inaendelea na kazi na kwamba walichogundua ni kuwa fedha zilizokuwa katika akaunti ya Tegeta Escrow zilikuwa za umma na kwamba kampuni ya Pan Africa Power Resources (PAP) hawakuwa na uhalali wa kuchukua fedha hizo.
PAC bado inaendelea na kazi. Watu wote ambao wamehusika katika wizi huu tutapendekeza wawajibishwe na kuchukuliwa hatua za kisheria.alisema
Tishio kwa wabunge
Baadhi ya wabunge wanaonekana vinara wa kusimamia suala hilo wanaelezwa kutishia maisha ambapo mbunge wa Kigoma Kusini, David Kafulila, ameshatoa ripoti polisi
Wasiwasi wa usalama wa wabunge hao umeongezeka zaidi baada ya taarifa kuwa mbunge wa Musoma Vijijini, Nimrod Mkono (CCM), kulishwa sumu akiwa safarini nchini Uingereza
Mkono inadaiwa ndiye anayejua sakata la IPTL kwakuwa kwa muda mrefu amekuwa akishiriki kwenye kesi akisimamia Tanesco na wizara ya Nishati na Madini
Mbunge huyo anadaiwa kuvujisha siri ya uchotwaji wa fedha hizo kwakuwa Wizara ya Nishati na Madini mwanzoni mwa mwaka huu haikuingia makataba wa kuitumia kampuni ya uwakili ya mbunge huyo
Hata hivyo Mkono, mwenyewe mara kadhaa alishakanusha madai ya kushiriki kwenye kuvujisha siri za ufisadi huo wala kuwa nyuma ya sakata hilo.
Chanzo: Tanzania daima
Singasinga Seth na familia yake wanamiliki 50% ya hisa za PAP. Huyo mmiliki mwingine wa 50% ndiye kinara wa dili hili chafu.
Aliye msafi na awe wa kwanza kurusha jiwe.
Thubutu! labda kama hawajipendi. shaba hadharani. usicheze na serikali za kikominist hata siku moja. hao ni rahisi kwenda kuomba ushauri kwa Al-Shabab kuliko kwa wachina.Ushirikiano wetu na China unakua sana kwa sasa nadhani watusaidie kutoa mapendekezo ya namna ya kushughulikia tatizo la ESCROW. Si unajua siku zote ukipata tatizo unapata ushauri kwa rafiki wako wa karibu au sivyo?
Katika kile kinachoonesha kama kupanic na hofu kwa ripoti ya CAG baada ya kuonesha kuwa hakuna kasoro katika mchakato wa utoaji wa fedha za escrow, Mwenyekiti wa kamati ya PAC ameibuka na kutoa mapendekezo yafuatayo
1.PM KUJIUDHURU KWA KUSHINDWA USIMAMIZI
2.AG AMESAMEHE VAT
3.PROF AJIUZURU KWA KUMLETA RUGEMALIRA
4.MASELE AJIUZURU KWA KUMSHAMBULIA BALOZI.
Katika mapendekezo yake hapo juu Zitto ameonyesha kuweweseka na kile ripoti ya CAG kimebaini kuhusu mchakato wa utoaji fedha za escrow ambazo inasemekana ni malipo halali ya IPTL