- Wakati umefika wa kupunguza msururu wa Viongozi wa juu, na hasa gharama za kuwatunza waki-retire, I mean people naomba kuuliza hivi kweli tunawahitaji Waziri Mkuu na Makamu wa Rais katika Serikali yetu? kwa maoni yangu one has to go kwenye katiba mpya na hasa Makamu wa Rais, kama ni muhimu kuwa naye basi Waziri Mkuu ashike hiyo nafasi kama zamani.
- The idea kwamba hata Visiwani kunakuwa na Makamu wa Rais, tena wawili it does not make a sense at all, wanafanya nini? Hivi vinakuwa ni vyeo vya huruma tu, under whose expense? kodi yetu wananchi wakati ni sasa kwenye katiba mpya kuondokana na na huu msururu wa Viongozi wa juu, tuwe na huruma kwa Walalahoi kidogo jamani!
MUCH RESPECT PEOPLEs!
William @..NYC, USA: Mutuz Le Baharia!
Mkuu @ New york, mapendekezo yako ni mazuri ila mara nyingi nikiona Taifa kubwa kama Marekani linakuwa na makamu wa Rais basi hiyo nafasi ina umuhimu wake isipokuwa tu hapa kwetu hii ndio imekuwa maalum kwa ajili ya kuwafariji Wazanzibar kutokana na mfumo wa siasa uchwara.
Sasa basi mimi pendekezo langu kwenye katiba mpya ni kufuta kabisa cheo cha ukuu wa wilaya, hawa ni kundi la majobless ambao hawana tija kwa Taifa.
Mkurugenzi wa almashauri anatosha kabisa kuwajibika kwa ajili ya wilaya yake huku akiwa na makatibu tawala wa wilaya na mawaziri sio lazima wawe wabunge, maana kama una wabunge wa category ya Livingstone Lusinde sijui hilo baraza utaliundaje, maana ni afadhali uwe na mawaziri kama kina Joti wa ze comedy wanaweza kuwa na maana zaidi.
Nchi ni watu. Kumbe ni miti? Huwezi kusema Tanzania ni tajiri kama watu wa Tanzania ni masikini.Tuandike katiba kwa kuzingatia kuwa sisi ni nchi masikini?... Tanzania ni nchi tajiri yenye watu masikini....
Mi nadhani ni mfumo au utaratibu kama ule unaotumika Marekani ya Kaskazini U.S.AMawazo mazuri sana mkuu wangu isipokuwa tu ktk mfumo huo rais atachaguliwa vipi? kutokana na 1. Popular vote; 2.Mwenye wajumbe wengi ktk Bunge la Muungano (Upper house) au 3.Matokeo ya chaguzi za majimbo ktk states mbili (Tanganyika/ Zanzibar) .
- Yapi majukumu ya rais tukisha kuwa na mfumo kama huu. Maadam kila state itakuwa na waziri mkuu wake, hawa watakuwa na madaraka juu ya uthibiti, usimamiaji na utekelezaji wa kila siku kazi na shughuli za states hizo ni nani atachukua nafasi ya waziri mkuu ktk serikali ya Muungano.
Samahani nimefanya editing baada ya kuona umependekeza makamu wa rais kuchukua nafasi ya waziri mkuu bunge la Muungano..
Mkuu huoni kaa huyu rais atakuwa - ceremonial President maanake sioni kazi ilobakia ikiwa kila state itajitawala na bunge la muungano kuna makamu wa rais, yeye rais atakuwa na madaraka gani haswa?
Rais wa Jamhuri ya Muungano ndiye anakuwa Amiri jeshi Mkuu wa majeshi ya ulinzi na usalama, mkuu wa nchi. Kila Waziri Mkuu atateua Baraza lake la Mawaziri bila kuingiliwa na Rais. Rais wa muungano atateua Mawaziri kwa Wizara za Muungano tu - Nje, Ulinzi, Ndani, Union Treasury.
Ni kweli Rais na Mawaziri wakuu wataweza kutoka vyama tofauti. Huu ndio mfumo uliopo hata sasa kwamba WM anatoka chama chenye wabunge wengi na sio lazima kiwe chama anachotoka Rais.