Mapendekezo katiba mpya: Tunahitaji makamu wa rais?

Katiba mpya ni lazima iyakinishe vyeo vya watendaji wakuu wa serikali, suala la awepo makamu wa raisi ama la, litemegemee umuhimu wa kiutendaji, katiba ni lazima iweke majukumu kamili ya kiutendaji, kwa sasa yupo yupo tu kama kumwakilisha raisi kwenye mambo ya kiitifaki hana mamlaka kamili kiutendaji kiserikali hata kama yapo hayaonekani kwa madaraka aliyonayo sasa sidhani kama anaweza hata kumfukuza kazi mkurugenzi wa wilaya. Hii nafasi ina umuhimu wake sana kumsaidia raisi kiutendaji tatatizo lilipo ni kuwa raisi wetu si rahisi kukubali kupunguza madaraka yake, labda katiba iweke wazi kama makamu wa raisi ni lazima atoke Zanzibar, hivi sasa tuna mgongano wa katiba zetu iweje raisi wa Zanzibar awe waziri kwenye muungano? Je mkubwa kimadaraka ni nani; ni lazima siasa za kiccm tuweke pembeni na tuangalie maslahi ya Taifa, suala la mgombea mwenza atoke wapi viachiwe vyama vyenyewe viamue, ili kuboresha muungano wazinzibar wapewe nafasi ya kuujadili kama wanautaka au la; inaonekana tunawalazimisha wameshasema Zanzibar haitachangia gharama za katiba mpya; hiyo itakuwa ni jukumu la serikali ya muungano; sasa kama sio kujichanganya wao ni kitu gani? je wao hawamo kwenye muungano tunaoungelea?

Chama
Gongo la Mboto DSM.
 
Rais ni mfumo,

kwahiyo watu wengi wanaangalia kwa macho dhahifu kuona kazi za makamo wa rais, kwakuwa wanaangalia kwa macho na fikra pana awaoni nafasi ya makamo wa rais ina umuhimu gani katika taifa letu.

Kwanza napenda kusema namchukia makamo wa rais lakini sichukii cheo cha makamo wa rais, kwani kikitumiwa vizuri ni moja vya taasisi za urais katika ushauri wa mambo mazito ya nchi, pia kutokana na yeye kutoingilia mambo mengi ya kiutendaji ya kila siku anajiweka katika nafasi nzuri ya kubobea katika tafiti na kuibua mambo mengi ya kuweza kumshauri rais yaingie katika mfumo wa utekelezaji pia ni mtu anayeweza kupima mwendo wa serikali kwani yeye ni mtendaji nusu asiyelimbikiziwa kazi nyingi.


Makamu wa rais kutojaziwa kazi nyingi za kufanya zinamuwezesha kuwa na muda wa kutafiti mambo mbali mbali na kufuatilia maagizo ya rais kwa watendaji wadogo, wengi wa watanzania tumekariri kuwa kazi ya mtu ni lazima kuwe na mlundikano wa mafaili katika meza ya mtu ndio tusema ana kazi ya kufanya.

 


Umenena vyema. Mimi kwa mtazamo wangu naona kama nchi hatuwahitaji wote wawili yaani makamu wa rais na waziri mkuu. Tuna rais mtendaji ana ndiye mkuu wa serikali. Waziri mkuu yupoyupo tu hana lolote analoweza kuamua bila rais kukubali. Ndio maana hata Lowassa amewashinda hoja wanaompinga kwenye vikao vya juu vya CCM kwa sababu kimsingi maamuzi yote kuhusu Richmond yalibarikiwa na baraza la Mawaziri likiongozwa na rais. Uhusiano wa Rais na waziri mkuu ni sawa na uhusiano wa mwalimu na kiranja wa darasa ambaye kimsingi hana anachoweza kuwafanya wanafunzi wenzake zaidi ya kuwashitaki kwa mwalimu.

Makamu wa raisi ni cheo ambacho sijawahi kuona manufaa yake tangu kilipoanzishwa. Siko zote huwa najiuliza hivi huyu jamaa job description yake ni ipi? je kila siku anapoenda ofisini anafanya nini ndani ya masaa nane anayokuwa ofisini? Labda wajuzi watakuja kutuelimisha.
 


kaka nimeipenda hiyo ya kwenye red huyu jamaa ukimsikiliza unatamani hata kuvunja tv jinsi alivyo empty head hivi anakaaga anatafakari anachokizungumza? wenje alimwambie fulsa ya kusoma tulipewa wote mimi niilitumia vizuri mwenzangu hukuitumia lilikuwa ni tusi ambalo kwa watu tuliendea shule tulilielewa ila yeye maskini wa mungu hakupata kitu. eti ndio mtu anatunga sheria bungeni lol WILLIAM MALECELA what do u expect tutapata katiba nzuri kutoka kwenye kichwa kama hiki? viti maalum je wanaopiga makofi tu bungeni? look at vijana kama John mnyika, wenje, halima mdee!!
 
Tuandike katiba kwa kuzingatia kuwa sisi ni nchi masikini?... Tanzania ni nchi tajiri yenye watu masikini....
Nchi ni watu. Kumbe ni miti? Huwezi kusema Tanzania ni tajiri kama watu wa Tanzania ni masikini.

Ni muhimu tuunde katiba inayotambua kwamba sisi ni masikini. Itakayotutoa kwenye umasikini, sio tu jedwali zuri la mgawanyo wa "uwajibikaji" au madaraka. Hizo ni siasa. Tunapoteza muda mwingi kufikiria siasa, wakati kipaumbele chetu cha kwanza kinatakiwa kiwe kuondoa umasikini. Huwezi kutatua tatizo la umasikini kama unakataa ukweli kuwa, kwa kuanzia, wewe ni masikini.

Nchi masikini haiwezi kumudu mawaziri wakuu kibao, makamu wa marais kibao, maserikali kibao na mabunge kibao na wawakilishi kibao. Hatuwezi kufuta umaskini kama hatutumii mali zetu finyu kichumi.

Na kwa kuanzia, tungepunguza mzigo wa Zanzibar.
 
Mi nadhani ni mfumo au utaratibu kama ule unaotumika Marekani ya Kaskazini U.S.A
 

Zitto hapo umenichanganya. Kama Rais atateuwa Mawaziri wa Nje, Ulinzi, Ndani na Union Treasury, ina maana watakuwa accountable kwa Rais, na Mawaziri Wakuu wa pande zote mbili can't question them. Hao mawazi walioteuliwa na rais, wataingia vipi kwenye cabinet ya bara na visiwani?
 
Muungano ufe kabisa. Hakuna faida yoyote ya muungano zaidi ya raia wa pande zote mbili kulalamika wanapunjwa rasilimali zao pamoja na kuongeza gharama za uendeshaji nchi kwa kuwa na lundo la viongozi wa muungano kwa gharama ya walipa kodi ambao wengi wetu ni watu wa kipato cha chini. Vyama vyote vya upinzani vinataka serikali tatu. Serikali ya tatu ifanye kazi gani wakati kila nchi itakuwa na serikali yake yenye mamlaka kamili kama si kufuja hela za walipakodi wachovu? Nini kitakachofanya kwamba raia wa pande hizi mbili wasilalamike kwamba upande mmoja una viongozi wengi kwenye serikali ya muungano kuliko mwingine? Kazi gani zitakazofanywa na serikali ya muungano bila kuingiliana na kazi za serikali husika za nchi?
Huu ni wakati mgumu kwa uchumi wetu kutokana na misukosuko ya dunia ya kiuchumi. Hatuna budi kufanya maamuzi yenye maslahi ya kiuchumi kuliko kun'gan'gania mfumo ambao hauna tija kwa mataifa yetu.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…