sulphadoxine
JF-Expert Member
- Nov 1, 2010
- 2,257
- 644
Mapadri wanne raia wa Italia wa kanisa katoliki,wamefariki dunia ,baada ya gari walilokuwawakisafiria kupata ajali.
Ajali hiyo ilitokea jana saaa 5v asubuhi katika eneo la Ruvu kwa zola wilaya ya kibaha,mkoani pwani baada ya gari dogo walilokuwa wakisafiria kugongana uso kwa uso na lori.
Kamanda wa polisi wa mkoa huo amedhibitisha kutokea kwa jali hiyo na kusema miili ya marehemu imehifadhiwa katika hospitali teule ya tumbi wilayani humo na kuwataja mapadri hao kuwa ni Sylverio Ghelli(72), wa parokia ya pugu aliye kuwa akiendesha gari walilokuwa wakisafiria,Mapadri wengine waliofariki aliwataja kuwa ni Corrad Trivivelli,Luciano Baffgi na aliye fahamika kwa jina moja la Andrea.
Alisema mapdari hao walikuwa wakitokea katika dayosisi ya kongwa mkoani Dodoma kwenda parokia ya pugu,jijini Dar es salaam na wote walikuwa kwenye gari dogo aina ya Toyota Land Cruiser lenye namba za usajli T903 ACQ .
Bwana alitoa bwana ametwaa.
Ajali hiyo ilitokea jana saaa 5v asubuhi katika eneo la Ruvu kwa zola wilaya ya kibaha,mkoani pwani baada ya gari dogo walilokuwa wakisafiria kugongana uso kwa uso na lori.
Kamanda wa polisi wa mkoa huo amedhibitisha kutokea kwa jali hiyo na kusema miili ya marehemu imehifadhiwa katika hospitali teule ya tumbi wilayani humo na kuwataja mapadri hao kuwa ni Sylverio Ghelli(72), wa parokia ya pugu aliye kuwa akiendesha gari walilokuwa wakisafiria,Mapadri wengine waliofariki aliwataja kuwa ni Corrad Trivivelli,Luciano Baffgi na aliye fahamika kwa jina moja la Andrea.
Alisema mapdari hao walikuwa wakitokea katika dayosisi ya kongwa mkoani Dodoma kwenda parokia ya pugu,jijini Dar es salaam na wote walikuwa kwenye gari dogo aina ya Toyota Land Cruiser lenye namba za usajli T903 ACQ .
Bwana alitoa bwana ametwaa.