Maono yangu: Lowassa ameacha kura CCM

Maono yangu: Lowassa ameacha kura CCM

Lowassa ameacha kura nyingi sana CCM hao watakaompigia ni wachache sana, wengi hawapo tayari kuiacha CCM na kuichagua Ukawa.
Mnasahau kinachaguliwa chama na sio mtu.
Ukawa wanapoteza kura za wale walioumia kwasababu ya vyama vyao. Ukawa wamepoteza maana ya upinzani, wale waliokuwa wanawaamini hawatawachagua baada ya kuona wamesalitiwa.

Hujui ukisemacho, kura za Lowassa zilizokuwa CCM watampa bila shaka..... Lowassa alijenga personal friendship na wanachama na sio kwamba walimfata kwa sababu ya nguvu yake kwenye chama....

Hii ni vita ya nje na vile vile ni vita ya ndani.... Trust Me ndani ya wanachama wa CCM Lowassa atapata zaidi ya kura millioni 3.5 out of millioni 6..... Ambacho msahau ni CCM kupata kura za Ukawa, hiyo ni ndoto kabisa....
 
Lowassa akishindwa kwenye uchaguzi mkuu mtamlaumu nani?

Mkuu UKAWA wamepiga.Hesabu ya mbali,Calculated Risk,wakiukosa Urais Ubunge.lazima waongeze.viti iwe isiwe,na.wanaobeza nguvu ya Lowasa wasubiri kuona.nyeti za kuku
 
Tatizo ni maadili yake tu, wala siyo suala la kaingia lini kwenye chama...!

Mifumo ndiyo inayotoa mwelekeo wa kiongozi. Kama mifumo ni mibovu hata kiongozi awe muadilifu kiasi gani, ufisadi hautakoma.

Ninachoweza kusema ni kwamba viongozi wetu tunawaamini. wao ndo wako huko field, wamesoma upepo wote. kama wakiridhika kuwa fulani atuwakilishe mimi nitawaunga mkono 100%
 
Huku Tanzania tunachaguwa mtu na sio Chama.Uchaguzi uliopita tulimchaguwa JK kama yeye na siyo Chama...na uchaguzi huu watu watamchaguwa EL kama yeye na siyo chama wakitilia manani shortcut ya kumpata mgombea iliyofanywa na ccm.
 
Lowassa hawezi kuwa raisi. Labda kama sio CCM niijuayo. Hapa afe NEC afe mpiga kura CCM lazima ilinde kiti. Wapiga kura wenyewe Wa kupewa kofia na kanga wamesarenda? Vijana wapiga kelele nao wana njaa mwanzo mwisho wakipewa buku 20 tu wameuza kura. Tanzania bado sana kuitoa CCM kwakuwa ndio ina dola, watz bado njaa sana (meaning maadili yameporomoka kuanzia ngazi ya mtu binafsi so wanashawishika kwa vitu vidogo), kutoeleweka kwa upinzani Leo wana agenda hii kesho wanaipinga wenyewe, na Lowassa mwenyewe ni lateral representation ya uchafu.
 
Tatizo ni maadili yake tu, wala siyo suala la kaingia lini kwenye chama...!

Sauli kabla ya kuwa mtume wa Mungu (Mtume Paulo) alikuwa na maadili mabaya sana. Lakini baada ya kumjua Mungu aliachana na tabia mbovu na kuwa mwadilifu mbele ya Mungu na jamii. Vivyo hivyo kwa Lowassa baada ya kuachana na mfumo fisadi wa CCM na kuhamia CHADEMA anakuwa mtu safi maana atakuwa ametubu kuachana na madhambi yaliyosababishwa na mfumo wa kifisadi wa CCM. Pia mfumo safi wa CHADEMA utaendelea kumfanya awe safi zaidi.
 
Kumsafisha itataka uwe na moyo wa chuma.

CCM msafi nani? anzia mwenyekiti wao mpaka mjumbe wa nyumba 10. Rotten altogether hivyo CCM hamna haki ya kumnyooshea kidole Lowassa ilhali nyie ni wachafu zaidi yake
 
Lowassa ameacha kura nyingi sana CCM hao watakaompigia ni wachache sana, wengi hawapo tayari kuiacha CCM na kuichagua Ukawa.
Mnasahau kinachaguliwa chama na sio mtu.
Ukawa wanapoteza kura za wale walioumia kwasababu ya vyama vyao. Ukawa wamepoteza maana ya upinzani, wale waliokuwa wanawaamini hawatawachagua baada ya kuona wamesalitiwa.

Siasa sio kama dini. Hakuna neno hata moja linalosemwa kwenye siasa linamaanisha exactly kama lilivyosemwa. So don't be surprise na mabadiliko kama hayo. Jamaa wameona opportunity kupitia Lowassa, wakaichukua. Trust me, kama ungekua kwenye game ungeelewa vizuri kuwa siasa sio uadui na an individual person kama wengi tunavyofikiria.
 
Lowassa ameacha kura nyingi sana CCM hao watakaompigia ni wachache sana, wengi hawapo tayari kuiacha CCM na kuichagua Ukawa.
Mnasahau kinachaguliwa chama na sio mtu.
Ukawa wanapoteza kura za wale walioumia kwasababu ya vyama vyao. Ukawa wamepoteza maana ya upinzani, wale waliokuwa wanawaamini hawatawachagua baada ya kuona wamesalitiwa.

Hiyo ni hadithi isiyoyakweli Pole sana kwani hata mimi nilikuwa CCM nikaihama kwa kutoridhishwa na utendaji wake kwa wananchi.
 
Lowassa ameacha kura nyingi sana CCM hao watakaompigia ni wachache sana, wengi hawapo tayari kuiacha CCM na kuichagua Ukawa.
Mnasahau kinachaguliwa chama na sio mtu.
Ukawa wanapoteza kura za wale walioumia kwasababu ya vyama vyao. Ukawa wamepoteza maana ya upinzani, wale waliokuwa wanawaamini hawatawachagua baada ya kuona wamesalitiwa.

granted. but embu nenda hatua moja mbele zaidi udadavue kwa vielelezo vya kitakwimu ili tusiojua tujifunze, chief.
 
Mbona mnatoana roho wakati Lowassa yupo kimya hajatamka chochote, subirini atamke kwanza msimalize nguvu zenu bure.
 
EL hajasimama mwenyewe kwenye maamuzi haya. EL kasimamishwa na KITENGO kwa kazi maalum kuua Ukawa. Anaelekea kutekeleza kazi aliyotumwa.
 
Lowassa hawezi kuwa raisi. Labda kama sio CCM niijuayo. Hapa afe NEC afe mpiga kura CCM lazima ilinde kiti. Wapiga kura wenyewe Wa kupewa kofia na kanga wamesarenda? Vijana wapiga kelele nao wana njaa mwanzo mwisho wakipewa buku 20 tu wameuza kura. Tanzania bado sana kuitoa CCM kwakuwa ndio ina dola, watz bado njaa sana (meaning maadili yameporomoka kuanzia ngazi ya mtu binafsi so wanashawishika kwa vitu vidogo), kutoeleweka kwa upinzani Leo wana agenda hii kesho wanaipinga wenyewe, na Lowassa mwenyewe ni lateral representation ya uchafu.

Kwanin umewa-underestimate wananchi kiasi hivyo?
 
EL hajasimama mwenyewe kwenye maamuzi haya. EL kasimamishwa na KITENGO kwa kazi maalum kuua Ukawa. Anaelekea kutekeleza kazi aliyotumwa.

Nimehisi hivyo hata mimi.
Sijawa comfotable Lowassa kuingia Ukawa. Kuna mtu nyuma ya maamuzi yake na watu walio ndani ya Ukawa wapo wanaoshinikiza haya yote.
 
Back
Top Bottom