TUJITEGEMEE
JF-Expert Member
- Nov 6, 2010
- 23,914
- 23,079
Kumuita mwenzako mhuni unatakiwa uwe na ushahidi unaohalisika kudhibitisha, ili neno halitumiki hivi hivi kimasihara masihara hasa kwa mwandishi makini wa habari.
Kwanza aliyesema ni dhambi kuwa mwanachama wa CCM nani? Ningekuwa CCM wala nisingejikana na kuona haya maana hiyo ni haki yangu ya kikatiba.
1. Nyie kama TBC mnawaunga mkono akina nani? Kama ni CCM basi mnastahili mlichofanyiwa; kwa kuwa hamna shirika na watanzania.Nachelewa kusema kuwa tabia iliyoanzishwa na baadhi ya wafuasi wa CHADEMA kuwaona kila wasio waunga mkono ni wasaliti haifai na wala haileti picha ya uvumilivu wa kisiasi ambao tungetarajia kuuona ukihubiriwa kwa vitendo na yoyote anajipambanisha na chama au jumuiya makini.
thibitisha kama hao ni wana CHADEMA! Huna maana Gamba wewe
hilo ndilo lililonishangaza! Hao ndiyo waandishi wetu wasiokuwa na ethics! Mtu unatukana jamii nzima kwa ajili ya watu watatu! Nani muhuni kama si yeye
Tatizo shule za kuunga-unga,waandishi kama hawa ni kuchapa vibao.Unatafuta kulambwa na wewe, kwani ni lazima ufuate mkumbo si useme la kwako tu, jiangalie mtoto wa kiume shauri lako.
Pamoja na changamoto zinazoikabili tasnia ya habari nchini bado watanzania wanapaswa kuheshimu na kuthamini huduma ambayo wote tunajua mazingira yalivyo si tu Tanzania lakini bara zima la Afrika linapokuja suala la Uhuru wa vyombo vya habari. Kitendo kilichoripotiwa kwenye mitandao mbalimbali ya kijamii kuwa, baadhi ya wakazi wa jiji la Arusha ambao kwangu nawaona ni "wakazi wahuni" kujaribu kuwazuia waandishi kutoka Shirika la Utangazaji Tanzania (TBC) kufanya kazi yao kwa kigezo kuwa wanatoa taarifa za kupotosha hazina msingi na walipaswa kutafuta njia nyingine ya kuonyesha kwao kutoridhishwa na utendaji wa shirika hilo. Nachelewa kusema kuwa tabia iliyoanzishwa na baadhi ya wafuasi wa CHADEMA kuwaona kila wasio waunga mkono ni wasaliti haifai na wala haileti picha ya uvumilivu wa kisiasi ambao tungetarajia kuuona ukihubiriwa kwa vitendo na yoyote anajipambanisha na chama au jumuiya makini.
NB: Huu ni mtazamo wangu binafsi kama mwanahabari, wala hakuna mahusiano na itikadi au maslahi ya shirika lolote.