MamaSamia2025
JF-Expert Member
- Mar 29, 2012
- 10,202
- 22,244
WAFUATAO WAPEWE UDAKTARI WA HESHIMA HARAKA SANA.
Leo nami nimeona nitoe maoni yangu kuhusu hili suala la watu kutunukiwa udaktari wa heshima kwa mambo waliyoyafanya kwenye jamii. Gumzo kubwa ni baada ya Mheshimiwa Musukuma kupata udaktari wa heshima siku za hivi karibuni. Huenda kuna mambo makubwa Mh Musukuma kayafanya huko Geita hadi maeneo ya jirani Chato ndo maana wasomi wakaona wamtunuku.
Sasa mimi leo nimekuja na majina ambayo naona yanastahili kupewa udaktari wa heshima kwa mambo makubwa waliyoyafanya hapa nchini, haya majina yataambatana na ufafanuzi mfupi;
1. FILBERT BAYI
Huwezi kutaja riadha Tanzania bila kulitaja jina la Filbert Bayi. Huyu mzee alikuwa mwanariadha mashuhuri duniani aliyevunja rekodi kwenye mbio fupi za mita 1500 na maili moja. Sifa alizoziletea nchi sio za kubahatisha au za ku-boost na kiki kama vijana wa leo wanavyofanya. Hata baada ya kustaafu bado ameendelea kujihusisha na mchezo wa riadha huku pia akiwa katibu mkuu wa kamati ya olimpiki. Kimsingi huyu mzee ni miongoni mwa wazalendo wachache waliopo hapa nchini. Nadhani anastahili kuitwa Dr. Filbert Bayi.
2. Leodger Tenga
Huyu mzee kama ilivyo kwa Bayi pia naye alikuwa mwanamichezo wa mpira wa miguu aliyekuwepo kwenye timu iliyoshiriki kombe la Afrika. Pia kwenye uongozi wake TFF alileta mabadiliko makubwa baada ya kupokea uongozi uliokuwa chini ya Muhidin Ndolanga. Apewe udaktari maana hakuna namna.
3. Mr II "Sugu"
Huyu aliubeba muziki wa Bongo Fleva mabegani. Kupitia uvumilivu wake na kujituma aliweka misingi ya hii Bongo fleva ya leo. Apewe PhD
4. Master Jay, P-funk na Mika Mwamba.
Hawa watayarishaji wa mwanzo wa muziki wanastahili tuzo kwa kazi kubwa waliyoifanya. Kupitia ndoto zao wakaleta matumaini kwa vijana wengi.
5. Zitto Kabwe
Huyu kwa upambanaji wake alisababisha vijana wengi wajihusishe na siasa. Pia kupitia hoja zake bungeni ilibidi baadhi ya sheria zifanyiwe marekebisho hasa zinazohusu madini. Nadhani Zitto apewe tu hiyo PhD.
6. Mbwana Samatta
Mtanzania wa kwanza kucheza ligi kuu ya England. Haina haja ya kujadili sana kuhusu Samatta. Apewe PhD haraka sana.
7. Augustine Lyatonga Mrema
Mzee wa Kiraracha apewe tu hiyo PhD kwa sababu ni mmoja wa waasisi wa upinzani Tanzania walioleta mabadiliko makubwa kwenye siasa za nchi hii.
8. Haji Manara
Leo nami nimeona nitoe maoni yangu kuhusu hili suala la watu kutunukiwa udaktari wa heshima kwa mambo waliyoyafanya kwenye jamii. Gumzo kubwa ni baada ya Mheshimiwa Musukuma kupata udaktari wa heshima siku za hivi karibuni. Huenda kuna mambo makubwa Mh Musukuma kayafanya huko Geita hadi maeneo ya jirani Chato ndo maana wasomi wakaona wamtunuku.
Sasa mimi leo nimekuja na majina ambayo naona yanastahili kupewa udaktari wa heshima kwa mambo makubwa waliyoyafanya hapa nchini, haya majina yataambatana na ufafanuzi mfupi;
1. FILBERT BAYI
Huwezi kutaja riadha Tanzania bila kulitaja jina la Filbert Bayi. Huyu mzee alikuwa mwanariadha mashuhuri duniani aliyevunja rekodi kwenye mbio fupi za mita 1500 na maili moja. Sifa alizoziletea nchi sio za kubahatisha au za ku-boost na kiki kama vijana wa leo wanavyofanya. Hata baada ya kustaafu bado ameendelea kujihusisha na mchezo wa riadha huku pia akiwa katibu mkuu wa kamati ya olimpiki. Kimsingi huyu mzee ni miongoni mwa wazalendo wachache waliopo hapa nchini. Nadhani anastahili kuitwa Dr. Filbert Bayi.
2. Leodger Tenga
Huyu mzee kama ilivyo kwa Bayi pia naye alikuwa mwanamichezo wa mpira wa miguu aliyekuwepo kwenye timu iliyoshiriki kombe la Afrika. Pia kwenye uongozi wake TFF alileta mabadiliko makubwa baada ya kupokea uongozi uliokuwa chini ya Muhidin Ndolanga. Apewe udaktari maana hakuna namna.
3. Mr II "Sugu"
Huyu aliubeba muziki wa Bongo Fleva mabegani. Kupitia uvumilivu wake na kujituma aliweka misingi ya hii Bongo fleva ya leo. Apewe PhD
4. Master Jay, P-funk na Mika Mwamba.
Hawa watayarishaji wa mwanzo wa muziki wanastahili tuzo kwa kazi kubwa waliyoifanya. Kupitia ndoto zao wakaleta matumaini kwa vijana wengi.
5. Zitto Kabwe
Huyu kwa upambanaji wake alisababisha vijana wengi wajihusishe na siasa. Pia kupitia hoja zake bungeni ilibidi baadhi ya sheria zifanyiwe marekebisho hasa zinazohusu madini. Nadhani Zitto apewe tu hiyo PhD.
6. Mbwana Samatta
Mtanzania wa kwanza kucheza ligi kuu ya England. Haina haja ya kujadili sana kuhusu Samatta. Apewe PhD haraka sana.
7. Augustine Lyatonga Mrema
Mzee wa Kiraracha apewe tu hiyo PhD kwa sababu ni mmoja wa waasisi wa upinzani Tanzania walioleta mabadiliko makubwa kwenye siasa za nchi hii.
8. Haji Manara