jingalao
JF-Expert Member
- Oct 12, 2011
- 35,053
- 28,245
Kwa wiki kadhaa sasa Chama Cha Mapinduzi kimeamua kupambana na CHADEMA kwa kutumia mikutano, maandamano na mitandao ya kijamii.
Mfumo huu wa mapambano umekuwa ukitumiwa na wanaCHADEMA kwa mafanikio makubwa sana.
Ukweli ni kwamba CCM haina utaalamu katika aina hii ya mapambano. CCM imekosa wasemaji wenye vipaji na uwezo wa kuwavuta vijana, wasomi na wafanyakazi ukilinganisha na CHADEMA, mbinu hii mpya ya kuendesha siasa ni muhimu lakini inahitaji wataalamu wa hali ya juu.
CCM ingefanikiwa sana kama ingeendelea kutumia mbinu zake za kawaida kama vile kuhakikisha mabalozi wa nyumba kumi, wenyeviti wa vijiji au mitaa na wakuu wa wilaya wanawajibika ipasavyo kurudisha imani ya chama kwa wananchi na kuhakikisha CCM inashinda kwenye chaguzi mbalimbali.
Hakika ni kosa kubwa kutumia style iliyowatowa CHADEMA kimasomaso huku tukijua CCM ni mbabe wa vita ya mtaa kwa mtaa au nyumba kwa nyumba.
Nape umetuingiza katika vita vya anga bila kuwa na maandalizi ya kutosha na matokeo yake yatakuwa mabaya sana kwa upande wa CCM.
TAHADHARI KWA MODS-Naomba thread hii isifutwe au kuunganishwa na thread nyingine kama mlivyonifanyia jana.
KWA HISANI YA MTU WA TANZANIA
Mfumo huu wa mapambano umekuwa ukitumiwa na wanaCHADEMA kwa mafanikio makubwa sana.
Ukweli ni kwamba CCM haina utaalamu katika aina hii ya mapambano. CCM imekosa wasemaji wenye vipaji na uwezo wa kuwavuta vijana, wasomi na wafanyakazi ukilinganisha na CHADEMA, mbinu hii mpya ya kuendesha siasa ni muhimu lakini inahitaji wataalamu wa hali ya juu.
CCM ingefanikiwa sana kama ingeendelea kutumia mbinu zake za kawaida kama vile kuhakikisha mabalozi wa nyumba kumi, wenyeviti wa vijiji au mitaa na wakuu wa wilaya wanawajibika ipasavyo kurudisha imani ya chama kwa wananchi na kuhakikisha CCM inashinda kwenye chaguzi mbalimbali.
Hakika ni kosa kubwa kutumia style iliyowatowa CHADEMA kimasomaso huku tukijua CCM ni mbabe wa vita ya mtaa kwa mtaa au nyumba kwa nyumba.
Nape umetuingiza katika vita vya anga bila kuwa na maandalizi ya kutosha na matokeo yake yatakuwa mabaya sana kwa upande wa CCM.
TAHADHARI KWA MODS-Naomba thread hii isifutwe au kuunganishwa na thread nyingine kama mlivyonifanyia jana.
KWA HISANI YA MTU WA TANZANIA