MAONI: CCM imeingia vita vya anga bila ndege za kivita

jingalao

JF-Expert Member
Oct 12, 2011
35,053
28,245
Kwa wiki kadhaa sasa Chama Cha Mapinduzi kimeamua kupambana na CHADEMA kwa kutumia mikutano, maandamano na mitandao ya kijamii.

Mfumo huu wa mapambano umekuwa ukitumiwa na wanaCHADEMA kwa mafanikio makubwa sana.
Ukweli ni kwamba CCM haina utaalamu katika aina hii ya mapambano. CCM imekosa wasemaji wenye vipaji na uwezo wa kuwavuta vijana, wasomi na wafanyakazi ukilinganisha na CHADEMA, mbinu hii mpya ya kuendesha siasa ni muhimu lakini inahitaji wataalamu wa hali ya juu.

CCM ingefanikiwa sana kama ingeendelea kutumia mbinu zake za kawaida kama vile kuhakikisha mabalozi wa nyumba kumi, wenyeviti wa vijiji au mitaa na wakuu wa wilaya wanawajibika ipasavyo kurudisha imani ya chama kwa wananchi na kuhakikisha CCM inashinda kwenye chaguzi mbalimbali.

Hakika ni kosa kubwa kutumia style iliyowatowa CHADEMA kimasomaso huku tukijua CCM ni mbabe wa vita ya mtaa kwa mtaa au nyumba kwa nyumba.

Nape umetuingiza katika vita vya anga bila kuwa na maandalizi ya kutosha na matokeo yake yatakuwa mabaya sana kwa upande wa CCM.

TAHADHARI KWA MODS-Naomba thread hii isifutwe au kuunganishwa na thread nyingine kama mlivyonifanyia jana.


KWA HISANI YA MTU WA TANZANIA
 
ccm wameona hizo siasa za kibabe na ukiritimba hazieleweki tena kwa kizazi cha leo.

wewe ulitumainia kuwa wadanganyika wataishi kwa unyenyekevu wa woga milele???? advantage waliyokuwa nayo ccm ni kuwa waliendeleza ushenzi wa kikoloni wa mzungu na mwarabu dhidi ya ndugu zao.
Mfano hai nilioshuhudia mimi miaka ya 70's nikiwa bado mtoto ni watu wazima wenye wake na watoto wakikimbia baada ya landrover ya mkuu wa wilaya kuonekana inakuja kijijini. Mkuu wa wilaya siku hizo alikuwa kama sultan au governor wa malkia alikuwa na uwezo wa kumkamata mtu yeyote kijijini na kumpeleka gerezani bila kuulizwa. Sasa mambo kama hayo ccm waliarithi kutoka kwa wakoloni na wameyaendeleza katika kipindi chao chote cha kutawala. Walikuwa wanabadilisha majina tu mara kigogo, mara kingunge mara mtu mkubwa mara mtu mzito nk wakimaanisha vijisultani na vi governor vi mungu mtu.
Miaka ya 80's baada ya vita kulikuwa na shida za bidhaa, maji na umeme wa mgao ukaanza, ukubwa wa mtu ulikuwa ni kuwa na huduma zote muhimu wakati wananchi wengine hawana, walikuwa hawapangi mistari ya foleni ili kupata mahitaji kama wananchi wengine bali walikuwa wanapelekewa majumbani mwao na watumishi wa mashirika au serkali, wakienda hospitali au kukata ticket za usafiri nk wao wanaruka foleni ukinung'unika unaambiwa kwani wewe humjui huyo ni nani?? mtu mkubwa huyo!!!

Miaka ya 90's siyo tu waliendeleza ushenzi wao bali pia wakaanza kujilimbikizia mali, kupeleka watoto wao ng'ambo nk wakaanza kuigawa jamii katika matabaka ya walionacho na wasionacho, hali iliyofanya watu waanze kulalamika lakini kwa ajili ya kutokuwepo kwa elimu na hofu iliyojengeka kwa muda mrefu ya wananchi kwa serkali, basi ccm waliendelea kujihakikishia umilki wa serkali na kuendelea kutawala kwa hiari au mabavu, kwa hadaa au kwa chochote kile

Sasa watu wameamka wanataka ukombozi wa kweli, wawe huru kutoa maoni na kuwaajibisha viongozi uchwara wanaorudisha nyuma maendeleo ya nchi yao. Hapa tulipofika haogopwi mtu tena siyo mjumbe, mtendaji wala mkuu wa wilaya au mkoa, waziri wala mtoto wa raisi, muda wa ukoloni umeendelea sana na sasa saa ya ukombozi imewadia, wenye akili wameliona hilo!!
 
CCM HAWAACHI KUOTA MCHANA KWEUPE,KATIKA KAMPENI ZAO ZA KUWAPUUZA WATANZANIA WAMEANDAA ULAGHAI MWINGINE ILI WAPATE KURA ZA WAPUMBAVU.
1.KUANZISHWA BENKI YA WAKULIMA
2.KUANZISHA BENKI YA VIJANA
KATIKA UANZISHWAJI BENKI HIZO SERIKALI INA MPANGO WA KUWAHADAA WATZ KWA KUWAAMBIA WATAWAKOPESHA MIKOPO YENYE RIBA NAFUU,KUANZIA MILLION 1MPAKA 15.LAKINI KATIKA UOMBAJI HUO UNAHUSISHA WAJUMBE WA NYUMBA KUMI KAMA MAWAKALA WAO ILI UPATE MKOPO,CHA KUCHEKESHA ZAIDI INAAMINIKA CCM IMEJIPANGA KUTUMIA KITAMBULISHO CHA URAIA NA HASA CHA KUPIGIA KURA KAMA MTAJI WA KUWAPATA HAO WALENGWA.NA KUHAKIKISHA WANAOCHUKUA MIKOPO WOTE WATAIPIGIA CCM UCHAGUZI KUANZIA UDIWANI WA 2014 NA UCHAGUZI MKUU 2015.LAKINI WAJUMBE WENGI WANA WASIWASI KUWA VIJANA WALIO WENGI WAMEELEVUKA SANA NA WATAKULA PESA ZAO NA KUWAPIGIA WAPINZANI.CCM ILITUMIA MKUTANO WA JANGWANI KAMA KIPIMA JOTO SASA WAMEANZA KUINGIWA NA WASIWASI MAANA MKUSANYIKO ULE HAUKUKAMILIKA BILA YA PESA SASA WANAJIULIZA BILA VIKINDI VYA SANAA KWELI WATAKUBALIKA,MJUMBE ALIYE KARIBU NA NAPE KASEMA CHADEMA INAWANYIMA USINGIZI KULIKO HATA MAGONJWA YA WAZAZI WAO AU WANANDOA WAO.
BINTI MREMBO LUMUMBA CCM
:confused2:
 
CCM HAWAACHI KUOTA MCHANA KWEUPE,KATIKA KAMPENI ZAO ZA KUWAPUUZA WATANZANIA WAMEANDAA ULAGHAI MWINGINE ILI WAPATE KURA ZA WAPUMBAVU.
1.KUANZISHWA BENKI YA WAKULIMA
2.KUANZISHA BENKI YA VIJANA
KATIKA UANZISHWAJI BENKI HIZO SERIKALI INA MPANGO WA KUWAHADAA WATZ KWA KUWAAMBIA WATAWAKOPESHA MIKOPO YENYE RIBA NAFUU,KUANZIA MILLION 1MPAKA 15.LAKINI KATIKA UOMBAJI HUO UNAHUSISHA WAJUMBE WA NYUMBA KUMI KAMA MAWAKALA WAO ILI UPATE MKOPO,CHA KUCHEKESHA ZAIDI INAAMINIKA CCM IMEJIPANGA KUTUMIA KITAMBULISHO CHA URAIA NA HASA CHA KUPIGIA KURA KAMA MTAJI WA KUWAPATA HAO WALENGWA.NA KUHAKIKISHA WANAOCHUKUA MIKOPO WOTE WATAIPIGIA CCM UCHAGUZI KUANZIA UDIWANI WA 2014 NA UCHAGUZI MKUU 2015.LAKINI WAJUMBE WENGI WANA WASIWASI KUWA VIJANA WALIO WENGI WAMEELEVUKA SANA NA WATAKULA PESA ZAO NA KUWAPIGIA WAPINZANI.CCM ILITUMIA MKUTANO WA JANGWANI KAMA KIPIMA JOTO SASA WAMEANZA KUINGIWA NA WASIWASI MAANA MKUSANYIKO ULE HAUKUKAMILIKA BILA YA PESA SASA WANAJIULIZA BILA VIKINDI VYA SANAA KWELI WATAKUBALIKA,MJUMBE ALIYE KARIBU NA NAPE KASEMA CHADEMA INAWANYIMA USINGIZI KULIKO HATA MAGONJWA YA WAZAZI WAO AU WANANDOA WAO.
BINTI MREMBO LUMUMBA CCM
:confused2:

Bado wanaendelea kutumia mtaji wao mkubwa, ambao ni umaskini wa waTZ!! Safari hii sidhani kama watafanikiwa
 
andrews ukiandika bila kuweka hiyo mifont yako inayotuumiza macho utaeleweka tu, otherwise mbwembwe nyingine hizi ni za kijinga tu. nimevumilia lakini nimeshindwa ni kweli tu ndio umuweka mtu huru.
 
Last edited by a moderator:
Unategemea nini kwenye chama ambacho wazee ndo kila kitu hawataki vijana na ndio maana hata mbinu zao niza karne ya 13. hawasomi nyakati kwao ccm madaraka ni kuiba mpaka mwisho, unategemea watawachia vijana? ambao sasa ndo wako CDM kuongoza UKOMBOZI
 
Unategemea nini kwenye chama ambacho wazee ndo kila kitu hawataki vijana na ndio maana hata mbinu zao niza karne ya 13. hawasomi nyakati kwao ccm madaraka ni kuiba mpaka mwisho, unategemea watawachia vijana? ambao sasa ndo wako CDM kuongoza UKOMBOZI
vijana wa ccm lazima watoke kwenye ukoo wa kiongozi ndio apate madaraka
 
naona bado ccm inaamini kufanikiwa kupitia mbinu za chadema!


KWA HISANI YA MTU WA TANZANIA
 
Aliyeiroga ccm alishafariki, sasa ni ngumu kupata dawa ya kuzingua zindiko.
Njia hiyo waliyoamua kuitumia ndiyo itawamaliza.
Watu wenyewe wababu wataweza kuhimili aibu za uzeeni?
Nilicho na uhakika nacho ni kwamba njia hiyo wataiacha baada ya muda mfupi kwa kuchemsha vibaya. Kuna maeneo watarushiwa mawe, believe itg
 
Sasa hivi CCM ni chama kisicho rasmi cha upinzani, kila kitu wanajipima na CHADEMA.

Wataendeshwa mchakamchaka hadi wenyewe watachoka. Watarudi kwenye wizi wa kura, lakini safari hii wizi utakumbana na nguvu ya umma.
 
kama kweli mikakati wanayotumia hivi sasa ccm watashindwa vibaya tunalalamika nini??? kwanini mnamuamsha aliyelala/[ kama kweli amelala?] au ni uoga fulani kuwa pengine watashinda??? vinginevyo adui wako muombe njaa.
kama mkakati wao wa sasa ni mbovu basi iwe furaha kwa upinzani maana uhakika wa upinzani kuingia ikulu uchaguzi ujao ni wa uhakika zaidi vinginevyo jamaa kama wataendelea na 4w-drive huko mbele maajabu yanaweza kutokea kwa kuingia tena ikulu by wider margin than before sasa sijui ikitokea hivyo mtasusa?????[haya ni maoni tu]
 
kazi kwao walioanzisha hiyo vita, tunachotaka mujue, sisi watanzania tumechoshwa na namna CCM wanavyoliendesha hili Taifa kama vile wanagawana maandazi juu ya rasilimali zetu............. kazi ni moja tu kuwaweka pembeni sasa..... Tunawaomba wajiandae kisaikolojia kukabidhi Nchi hii kwa watu wengine kwa usalama na amani yetu kama ilivyo.........Freedom is coming tomorrow(2015)
 
CCM HAWAACHI KUOTA MCHANA KWEUPE,KATIKA KAMPENI ZAO ZA KUWAPUUZA WATANZANIA WAMEANDAA ULAGHAI MWINGINE ILI WAPATE KURA ZA WAPUMBAVU.
1.KUANZISHWA BENKI YA WAKULIMA
2.KUANZISHA BENKI YA VIJANA
KATIKA UANZISHWAJI BENKI HIZO SERIKALI INA MPANGO WA KUWAHADAA WATZ KWA KUWAAMBIA WATAWAKOPESHA MIKOPO YENYE RIBA NAFUU,KUANZIA MILLION 1MPAKA 15.LAKINI KATIKA UOMBAJI HUO UNAHUSISHA WAJUMBE WA NYUMBA KUMI KAMA MAWAKALA WAO ILI UPATE MKOPO,CHA KUCHEKESHA ZAIDI INAAMINIKA CCM IMEJIPANGA KUTUMIA KITAMBULISHO CHA URAIA NA HASA CHA KUPIGIA KURA KAMA MTAJI WA KUWAPATA HAO WALENGWA.NA KUHAKIKISHA WANAOCHUKUA MIKOPO WOTE WATAIPIGIA CCM UCHAGUZI KUANZIA UDIWANI WA 2014 NA UCHAGUZI MKUU 2015.LAKINI WAJUMBE WENGI WANA WASIWASI KUWA VIJANA WALIO WENGI WAMEELEVUKA SANA NA WATAKULA PESA ZAO NA KUWAPIGIA WAPINZANI.CCM ILITUMIA MKUTANO WA JANGWANI KAMA KIPIMA JOTO SASA WAMEANZA KUINGIWA NA WASIWASI MAANA MKUSANYIKO ULE HAUKUKAMILIKA BILA YA PESA SASA WANAJIULIZA BILA VIKINDI VYA SANAA KWELI WATAKUBALIKA,MJUMBE ALIYE KARIBU NA NAPE KASEMA CHADEMA INAWANYIMA USINGIZI KULIKO HATA MAGONJWA YA WAZAZI WAO AU WANANDOA WAO.
BINTI MREMBO LUMUMBA CCM
:confused2:

Mkuu una ujumbe mzuri, ila tusaidie wasomaji wako kutoweka rangi, na pia herufi ndogo zinasomeka kwa raha zaidi.

Thanks kwa mchango wako.
 
Kwa wiki kadhaa sasa Chama Cha Mapinduzi kimeamua kupambana na CHADEMA kwa kutumia mikutano, maandamano na mitandao ya kijamii.

Mfumo huu wa mapambano umekuwa ukitumiwa na wanaCHADEMA kwa mafanikio makubwa sana.
Ukweli ni kwamba CCM haina utaalamu katika aina hii ya mapambano. CCM imekosa wasemaji wenye vipaji na uwezo wa kuwavuta vijana, wasomi na wafanyakazi ukilinganisha na CHADEMA, mbinu hii mpya ya kuendesha siasa ni muhimu lakini inahitaji wataalamu wa hali ya juu.

CCM ingefanikiwa sana kama ingeendelea kutumia mbinu zake za kawaida kama vile kuhakikisha mabalozi wa nyumba kumi, wenyeviti wa vijiji au mitaa na wakuu wa wilaya wanawajibika ipasavyo kurudisha imani ya chama kwa wananchi na kuhakikisha CCM inashinda kwenye chaguzi mbalimbali.

Hakika ni kosa kubwa kutumia style iliyowatowa CHADEMA kimasomaso huku tukijua CCM ni mbabe wa vita ya mtaa kwa mtaa au nyumba kwa nyumba.

Nape umetuingiza katika vita vya anga bila kuwa na maandalizi ya kutosha na matokeo yake yatakuwa mabaya sana kwa upande wa CCM.

TAHADHARI KWA MODS-Naomba thread hii isifutwe au kuunganishwa na thread nyingine kama mlivyonifanyia jana.


KWA HISANI YA MTU WA TANZANIA

ccm wanachokifanya ni kama kuigiza. Hakuna mabadiliko ya msingi yanayotegemewa na hii secretariert mpya. Tatizo la ccm ni mfumo hata nyerere angefufuka na kupewa uenyekiti angeshindwa. Ni siku zimefika ni lazima ccm ife kifo cha kawaida 2
 
'Chama Cha Migogoro'...xo wat z ajabu abt that? Wao wanaona fahari kuwa na migogoro na vyama vya upinzani kavile ndio mfumo wa maisha ya kila siku... Yaan wameshafulia na xaxa wanaanza kuozeana na kutokwa na funza huku vilio vikitawala madomo yao...
 
Kwa wiki kadhaa sasa Chama Cha Mapinduzi kimeamua kupambana na CHADEMA kwa kutumia mikutano, maandamano na mitandao ya kijamii.

Mfumo huu wa mapambano umekuwa ukitumiwa na wanaCHADEMA kwa mafanikio makubwa sana.
Ukweli ni kwamba CCM haina utaalamu katika aina hii ya mapambano. CCM imekosa wasemaji wenye vipaji na uwezo wa kuwavuta vijana, wasomi na wafanyakazi ukilinganisha na CHADEMA, mbinu hii mpya ya kuendesha siasa ni muhimu lakini inahitaji wataalamu wa hali ya juu.

CCM ingefanikiwa sana kama ingeendelea kutumia mbinu zake za kawaida kama vile kuhakikisha mabalozi wa nyumba kumi, wenyeviti wa vijiji au mitaa na wakuu wa wilaya wanawajibika ipasavyo kurudisha imani ya chama kwa wananchi na kuhakikisha CCM inashinda kwenye chaguzi mbalimbali.

Hakika ni kosa kubwa kutumia style iliyowatowa CHADEMA kimasomaso huku tukijua CCM ni mbabe wa vita ya mtaa kwa mtaa au nyumba kwa nyumba.

Nape umetuingiza katika vita vya anga bila kuwa na maandalizi ya kutosha na matokeo yake yatakuwa mabaya sana kwa upande wa CCM.

TAHADHARI KWA MODS-Naomba thread hii isifutwe au kuunganishwa na thread nyingine kama mlivyonifanyia jana.


KWA HISANI YA MTU WA TANZANIA





Wataalamu wa kucopy na kupaste!!!!!!!
 
Hivi wana jf wenzangu mnajua tatizo la nchi ye2 nimfumo na si chama? Mm bado nina wasi wasi na hao cdm ina weza kuwa chupa nyengine ila mvinyo ni uleule, sababu cdm ina ongozwa na watu tena wengiwao wame toka humohumo ccm sasa tujiulize nijambo gani jema walili fanya wakiwa huko?
 
Back
Top Bottom