ligendayika
JF-Expert Member
- Aug 31, 2012
- 1,183
- 198
bila hivyo magazeti yataandika nini dili hizo
CCM ingefanikiwa sana kama ingeendelea kutumia mbinu zake za kawaida kama vile kuhakikisha mabalozi wa nyumba kumi, wenyeviti wa vijiji au mitaa na wakuu wa wilaya wanawajibika ipasavyo kurudisha imani ya chama kwa wananchi na kuhakikisha CCM inashinda kwenye chaguzi mbalimbali.
Habari za asubuhi kubwajingabado naendelea kumuonya nape kuwa ccm haiwezi vita vya mtandaoni!
Ukifuatilia posts ndani ya jamvi hili utaona ccm inavyozidi kubomolewa.
Kwa wiki kadhaa sasa Chama Cha Mapinduzi kimeamua kupambana na CHADEMA kwa kutumia mikutano, maandamano na mitandao ya kijamii.
Mfumo huu wa mapambano umekuwa ukitumiwa na wanaCHADEMA kwa mafanikio makubwa sana.
Ukweli ni kwamba CCM haina utaalamu katika aina hii ya mapambano. CCM imekosa wasemaji wenye vipaji na uwezo wa kuwavuta vijana, wasomi na wafanyakazi ukilinganisha na CHADEMA, mbinu hii mpya ya kuendesha siasa ni muhimu lakini inahitaji wataalamu wa hali ya juu.
CCM ingefanikiwa sana kama ingeendelea kutumia mbinu zake za kawaida kama vile kuhakikisha mabalozi wa nyumba kumi, wenyeviti wa vijiji au mitaa na wakuu wa wilaya wanawajibika ipasavyo kurudisha imani ya chama kwa wananchi na kuhakikisha CCM inashinda kwenye chaguzi mbalimbali.
Hakika ni kosa kubwa kutumia style iliyowatowa CHADEMA kimasomaso huku tukijua CCM ni mbabe wa vita ya mtaa kwa mtaa au nyumba kwa nyumba