Manyanyaso haya yatatuletea mauti

Sky Eclat

JF-Expert Member
Oct 17, 2012
57,597
215,272
Habari za J2 wapendwa,

Huyu shost mtakuwa mnamfahamu ni yule tulipata pamoja Ki-paimara katika lile kanisa. Shost huyu kwao wamezaliwa mabinti 6 hawana kaka na mabinti wote sita wametoka mashallah. Shost alipomaliza IV matokeo yalikuwa ya kawaida, alifanikiwa kusoma secretarial course na kupata kazi pia alibahatika kupata ndoa ya kanisani, mwenzangu alipata bahati ya kukaa madhabahuni tena na gauni leupe, kwangu mimi vilikoma baada ya ki-paimara.

Basi bwana shost alipata mume ambae alisaidia sana kwao, alisaidia ada za wadogo zake, alisaidia matengenezo ya nyumba wa wakwe na pia kuongeza mtaji kwenye biashara ya baba. Shost anaendelea na ajira yake, watoto watatu na msaidizi wa kazi za ndani ni mdada.

Shost amekuja kugundua kuwa msaidizi wa kazi za ndani ana uja uzito, uliza maswali dada amegoma kabisa kumtaja mhusika, shost anamsubiri mume wake amfahamishe kuwa dada ajira imekoma, mume amekuja juu ajira imekoma kwa sababu gani, kwani anashindwa kufanya kazi, hapana ana mimba, sasa mimba ni ugonjwa?

Baada ya mahojiano marefu, shost anagundua kuwa mimba ni ya mume wake, na pia hayuko tayari kumrudisha kijijini kwao anadai kwa usalama wa afya yake, Dar ndiyo kuna hospitali nzuri akae mpaka ajifungue.

Kwa kweli shost ana hali mbaya sana, ana hasira na anataka kuondoka, wazazi wanamshauri akae tu kwani huyu mwanaume ni kama mkombozi wa familia. Nikiangalia hali hii kwakweli wanaume haya sasa ni manyanyaso kisa unasaidia ukoo wa mke ndiyo umfanyie haya? Matokeo yake mtu anaamua kujiua.
 
Kwasababu tuna yakujifunza kutokana na matatizo yao ndiyo maana ninayaweka hapa, sasa nikiwaambia mashost zangu wanakwenda Hawaii kila summer kula bata mbona hayo ya kawaida mkuu.

Kwan hatuwezi kujifunza kitu kutoka story za kula bata hawaii?!
 
Wanaume sometimes tunazidi tamaa mpaka hous girl jamani nanyie wanawake jifunzeni kusoma mchezo kabla sio house girl anakuwa msafi kuliko mother house
 
Wanaume sometimes tunazidi tamaa mpaka hous girl jamani nanyie wanawake jifunzeni kusoma mchezo kabla sio house girl anakuwa msafi kuliko mother house
Mkuu si tamaa tu, sasa mtu anajua umefahamu kosa lake na bado anataka house girl akae mpaka akijifungua, ni kama umeletewa mke mwenza ndani ya nyumba.
 
Shida baadhi yenu huwa mnawaachia kazi zote housegirls isipokuwa moja tu. Mume anaamua kuifanyia finishing.
Pole yake lkn. Akitaka aondoke tu. Huyo mume ameshamdondokea hg and there's nothing she can do about it
Huyu mwanaume kwenye familia ya shost ni malaika aliyetoka mbinguni, akitaka aondoke hawatamuelewa.
 
Mwambie Shost kuwa msaidizi wa kazi za ndani ni msaidizi wa shughuli zingine pia siyo kufua na kupika tu kwahiyo mwambie awe mpole na akubali matokeo, inawezakana na yeye alijisahau sana.
 
Umezungukwa na watu wa ajabu ajabu mkuu khaaaa kila cku vihoja.. mpe pole shost ako ajikaze
 
Umezungukwa na watu wa ajabu ajabu mkuu khaaaa kila cku vihoja.. mpe pole shost ako ajikaze
May be mkuu when I'm around them this is only what I get, labda ni psychological set up of my brain to pick up the faults.
 
Back
Top Bottom