Babu Ubwete
Senior Member
- Jan 26, 2008
- 169
- 29
Halmashauri ya jiji la Dsm imekithiri kwa Ufisadi kiasi ambacho wamemmilikisha Yusufu Manji Ufukwe wa Coco Beach kuanzia Police mess mpaka karibu na American Club. Document iliyopo ya mkata feki wa kumilikishwa Manji ina Sahihi ya Naibu meya Ndg Bujugo. Huu ni Ufisadi uliokithiri kwa manispaa ya jiji na tunahitaji wabunge wa mkoa wa dsm wasimamie auditing ya mikataba yote ya jiji na matapeli kama akina manji. Jamaa ananunua property kwa bei ndogo na kuzipangisha kwa bei kubwa at wananchi expense. Hivi tutavumilia ufisadi huu mpaka lini. mama Tiba hebu fuatilia maswala ya ardhi ya umma kubinafsishwa. Pale Africana kuna Botanical garden ya public pia ameuziwa huyu Manji . Tunahitaji mchukue hatua haraka iwezekanavyo.