Manji atakiwa kuripoti Ofisi za Mamlaka ya Uhamiaji. Pasi 126 za kusafiria zakamatwa ofisini kwake

themagnificient

JF-Expert Member
Dec 13, 2016
988
3,318
Manji ahitajika Uhamiaji: Ofisi ya uhamiaji jijini Dar imemtaka mfanyabiashara Yusufu Manji kuripoti kwenye ofisi hizo baada ya kutoka hospitali alikolazwa.

Ofisa Habari wa uhamiaji mkoa wa Dar es Salaam
amedai kuwa Manji ameajiri watu wanaoishi nchini kinyume cha sheria.

My take;
Kuacha habari hiyo mimi binafsi ningependa kuwashauri mamlaka ya uhamiaji ili kututhibitishia kuwa Operation hii kuwa sio ya visasi wala chuki binafsi kama inavyodhaniwa na wengi. Iendelee kwenye makampuni mengine hasaa yanayomilikiwa na Wahindi

Kumekuwa na Utitiri wa Raia wa India ambao wamekuwa wakifanya kazi ambazo wazawa wana uwezo wa kuzifanya

Wenzetu kenya wameweza kudhibiti utitiri wa Raia wakigeni kufanya kazi ambazo Raia wa kenya wana uwezo wa kuzifanya. Mfano mmojawapo ni kampuni ya Kenya Airways ukiacha Uongozi wa juu ambao ni Kuna Raia wa kigeni wachache. Wengine wote kuanzia mafundi wa ndege hadi marubani ni Wakenya wenyewe
983769e42f3f675acb9e7a422c8546a5.jpg



Mfano mwingine ni kiwanda chao cha kutengeneza Magadi soda yanayotumika kutengeneza sabuni na vitu vingi kana vioo na chupa za glasi (soda hash dese) kiwanda chao kinaitwa TATA CHEMICALS kinachomilikiwa na raia India


Kiwanda hicho kimetoa ajira kwa maelfu ya watu kenya kuanzia ajira rasmi na zile zisizo rasmi. Lakini mshangao ni kuwa katika maelfu ya waajiriwa wa kiwanda hicho Wahindi wapo wawili tu yaani GM(General manager) na Mhindi anaye husika na maswala ya Account tuu,, wengine wote ni wakenya

Lakini hapa kwetu utakuta kampuni kuanzia Utawala hadi Operations sector kumejaa raia wa kigeni

=======

Habari zadi zinasema...

UHAMIAJI WAKAMATA PASSPORT 126 QUALITY GROUP.



Upepo Mchafu umezidi Kumuandama Manji, Baada ya Sakata la Madawa ya Kulevya kumuandama mpaka kufikia kulazwa Hospitalini, Uhamiaji nao wamekuja na Mpya baada ya kukamata Passport 126 ofisini kwake za watu kutoka nje ambao wanafanya kazi kwenye kampuni yake bila vibali vya uhamiaji....

John Msumule ambaye ni Afisa Uhamiaji Mkoa wa Dar es Salaam amesema, hii Kampuni ya Quality Group ipo katika jengo la Quality Center Barabara ya Nyerere kama unaelekea Uwanja wa ndege wa JNIA ni mkono wa kushoto. tumefanya kazi Ijumaa baada ya kuwekwa tu ndani yaani kesho yake jumamosi, tukapata Passport 126, Hizi ndizo zenye makosa. Tumechambua, passport 25 hawana vibali vya kufanya kazi, kwahiyo wanafanya kazi kinyume na utaratibu. Wote hawa hatua zitachukuliwa na watapelekwa Mahakamani.

Lakini lazima niseme ukweli, hawa hawatapelekwa peke yao mahakamani, lazima Yusuf Manji ambaye ndiye mwajiri wa watu hawa ambaye ndiye Mmliki wa Kampuni hii lazima afikishwe mahakamani kujibu shitaka la kuajiri watu wageni wasio na vibali. Jana tulikuwa tumkamate alale mahabusu na leo ndio tumpeleke Mahakamani, Bahati mbaya tulipokwenda kumkamata, tukaapewa taarifa kwamba amelazwa Hospitalini hadi sasa.

Mara tu atokapo, aliport ofisi hii ili tumuunganishwe kwenye kesi hii ya kuajiri watu wasio na vibali. Hatutajali ukubwa wa hela yako, hatutajali cheo chako cha mahali popote pale, hatutajali kwa njia yoyote ile una mamlaka gani katika nchi ya Tanzania.

Utakamatwa, utawekwa ndani, utajibu mashitaka.
Yusuf-Manji-002.jpg

Yusuf Mehbub Manji ni mfanyabiashara maarufu nchini Tanzaznia na Diwani wa Kata ya Mbagala kuu(CCM) Jimbo la Mbagala Dar es Salaam. Vilevile ni Mwenyekiti wa Club ya Mpira ya Nchini Tanzania Yanga Afrika SC.
 
Manji ahitajika Uhamiaji: Ofisi ya uhamiaji jijini Dar imemtaka mfanyabiashara Yusufu Manji kuripoti kwenye ofisi hizo baada ya kutoka hospitali alikolazwa.

>> Ofisa Habari wa uhamiaji mkoa wa Dar es Salaam
amedai kuwa Manji ameajiri watu wanaoishi nchini kinyume cha sheria.

Source:: Mwananchi
Beautiful.Utajiri wa kutapeli na kuibia wengine una mwisho.Za mwizi ni arobaini. Nadhani zimeshafika.
 
Manji ahitajika Uhamiaji: Ofisi ya uhamiaji jijini Dar imemtaka mfanyabiashara Yusufu Manji kuripoti kwenye ofisi hizo baada ya kutoka hospitali alikolazwa.

>> Ofisa Habari wa uhamiaji mkoa wa Dar es Salaam
amedai kuwa Manji ameajiri watu wanaoishi nchini kinyume cha sheria.

Source:: Mwananchi
ila huu unafiki wa serikali mi ndo siutaki kabisa, kuna wachina wangapi na wahindi wangapi wanaishi bila vibari? tena mi ofisi kwangu wapo kibao na wakija rushwa nje nje na unaona
 
Back
Top Bottom