Maneno yenye ishara mbaya katika uhusiano na mpenzi wako

englibertm

JF-Expert Member
May 1, 2009
9,252
6,207
Rafiki zangu, nazungumza juu ya kauli ambazo zina ishara mbaya kwenye uhusiano. Wakati mwingine unaweza kumsikia mpenzi wako akikuambia maneno ya ajabu sana, lakini usielewe maana yake ni nini.

Ngoja nikuambie, kila kinachotoka kinywani mwa mpenzi wako kukuambia wewe kina maana yake. Lengo ni kujifunza; kufahamu maneno hayo na maana zake. Wiki iliyopita tulianza na maneno, huvutii na hupendezi. Sasa tuendelee.

UNANUKA...
Mwenzi ambaye hana mpango tena na wewe, ataanza kukuonea kinyaa. Maneno ya kejeli kwake si suala la kujiuliza mara mbili. Ni rahisi sana kukuambia unanuka!

Ebwanae unanuka jasho sana, hebu kaoge kwanza, anaweza kukuambia hivyo.

Katika hali ya kawaida kabisa hii ni dharau, ila inawezekana labda mpo katika hatua ya kuelekea kwenye mahaba, lakini ulipomsogezea kinywa chako, ukakutana na maneno haya: Aaaah! Mh...unanuka mdomo bwana, sitaki!

Pia unaweza kumsikia akisema: Ongea taratibu unanirushia mate bwana.

Hizi si kauli njema na bila shaka anajaribu kukuonesha jinsi ambavyo umepungua thamani kwake.

Huwezi kunuka kwa mpenzi wako, siku zote huwa unanukia, lakini kama ameona dosari yoyote na yeye kama mwenzi wako wa karibu ana wajibu wa kuhakikisha anatumia lugha nzuri kukurekebisha, lakini kwa kuwa hana mapenzi na wewe, hana haja ya kuonesha mapenzi yake, anakubwatukia atakavyo!

SINA MPANGO WA KUOA
Wengi wanapokuwa katika uhusiano wanakuwa na ndoto zao, lakini ni aghalabu kukuta mtu yupo kwenye uhusiano wa kula raha tu! Mara nyingi ndoto kubwa huwa ni ndoa, ingawa ni vyema kupeana muda wa kuchunguzana kwa muda mrefu zaidi kabla ya kufikia azimio hilo muhimu maishani.

Lakini unapokuwa na mpenzi wako faragha, kwenye mazungumzo au katika matembezi ya jioni halafu ghafla akakuambia hana mpango wa kuoa au kukuoa, ni kama anakupa tiketi ya kukuacha.

Pima kauli hii, kama anazungumza kwa mzaha utagundua na kama yupo serious pia utajua. Angalia macho yake na namna anavyoweka mkazo kwa kauli yake hiyo.

Lakini hata kama hatakuambia hana mpango wa kukuoa lakini kusema kwamba hana mpango wa kuoa kwa muda huu (huo) nayo ni alama kwamba hana ndoto ya kuendelea nawe tena na kama ataendelea, anapoteza muda tu.

HUJUI MAMBO...
Hii ni mbaya zaidi maana inagusa eneo ambalo wengi hawapendi kuonekana hawawezi! Unaweza kuwa naye chumbani, ukijitahidi kadri uwezavyo kuhakikisha anafurahia, lakini ghafla unashangaa anakuambia hujui mambo!

Tena wakati anakuambia, anatamka kwa kumaanisha huku akitaka uongeze ujuzi maana muda wote mliokuwa naye hapo, ni kama mlikuwa mnacheza!

Jifunze ubunifu, kila siku huwa unaniacha kama nilivyokuja...nikueleze tu ukweli kwamba, hujawahi kukata kiu yangu hata siku moja! Kwa kauli hii, hapo una mpenzi tena jamani?

Tafakari anachokuambia, kama kinaingia akilini au la. Rafiki zangu, natamani sana kuendelea kuandika, lakini nafasi yangu inanibana.
 
Kauli kama hizo hutolewa na watu wenye mapenzi batili...
 
Kwa mpenzi wako hauwezi kunuka !! Hata kama hauji safishi ??

Acha masihara basi mkuu..
 
Wanawake wanaongoza kwa kusema wanaume wananuka ila wanajisahau. Kutana na mwanamke ananuka kwapa, kwenye mikunjo ya mwili (paja, shingo na kwenye mifereji
 
Unafeli mkuu akinuka mdomo kamnunuloe colgate...😀😀😀
Kuna mmoja nilimwambia kabisa ingawa ilikuwa kistarabu lakini ali mind sana. Baadae alibadilika. Yaani ilikuwa ukipiga bao moja mi naenda bafuni naoga yeye haendi. Majasho na mashahawa anabaki nayo anataka nipige tena. Aah wapi.
 
wa kwangu nilivofilisika analikuwa ananiuliza ulijisugua vizuri wakati utanaoga, after ten years in love!
Inawezekana sio kwa sababu ulifilisika ispokuwa baada ya wewe kufilisika ukawa hujijari tena mambo ya sopusopu
 
Back
Top Bottom