Mashabiki wa Man U ndio wanaoongoza kuwa na hasira kwenye mpira.!
Wana hasira kuliko wale wanaojiua baada ya kichapo kutoka kwa Man United?
www.goal.com/en-india/news/221/champions-league/2009/05/06/1249621/kenyan-fan-commits-suicide-after-arsenals-champions-league
news.sky.com/story/691459/arsenal-fans-suicide-over-man-utd-defeat
www.independent.co.uk/sport/football/news-and-comment/arsenal-fan-hangs-himself-after-manchester-united-defeat-1680088.html
usidhubutu kuwaambia ukweli kuwa timu yao mbovu mtagombana, wengi wanatamani babu arudi sababu aliwazoesha ushindi hata kama timu imezidiwa itashinda tu. !!
Wengi? Una chanzo chochote cha kuonyesha mashabiki wengi wa United wanatamani hivyo?
Marefa wengi walikua wanamwogopa Babu wakati mwingine hata FA walimtetemekea.!!
Una ushahidi wowote? Onyesha wakati ambapo marefa walimwogopa SAF, na wakati ambapo FA walimtetemekea! Ingekuwa hivyo, basi United angekuwa bingwa kila msimu! Kuna misimu United ilimaliza ligi bila ya kombe hata moja chini ya SAF. Misimu ya 1986/87, 1987/88, 1988/89, 1994/95, 1997/98, 2001/02 na 2004/05. Vipi unasemaje hapo, FA na marefa hawakuwepo?
Poleni mashabiki wa Man u, itabidi muwaombe mashabiki wa Arsenal wawaeleze wanaishije na timu yao kwa ushindi wa kubahatisha na kupata vikombe ni majaaliwa.!!
Pole ya nini? Kufungwa mara 1 katika mechi 3?!? Mbona United ndiyo staili yake; kuanza ligi kwa kusuasua. Msimu wa jana, tulianza na kichapo kutoka kwa the Tofees, chini ya SAF! Mbona hukutoa pole na kusema FA na marefa wanamtetemekea na kumwoga SAF?!?
Husipende kujifanya unaifahamu United; hauifahamu. SAF alivyoanza kufundisha msimu wa kwanza alimaliza wa 11, huku msimu mzima akipigana kuepuka kushuka daraja. Msimu uliofuata alimaliza pointi 9 nyuma ya mabingwa Liverpool licha ya kuwasajili Steve Bruce na Brian McClair waliokuwa moto kipindi hicho.
Nachotaka kukwambia ni kwamba, mimi kama mfuasi wa United, nina imani kubwa sana na
Moyes na chama langu kiujumla. Kipindi cha SAF kimeshaisha sasa chama linasonga mbele chini ya
Moyes' Red and White Army . Na utazidi kuichukia United mpaka kaburini
hater