Man of the moment: Reverend Christopher Mtikila

Man of the moment: Reverend Christopher Mtikila

Mudeer,

Salaam aleykum,

Nakusoma sana,hii bayana nikiiangalia mara mbili mbili wallahi hainiishi hamu kuirudia tena,

Shukran sana. Mohamed Said
 
Last edited by a moderator:
Msome tena na umuelewe....
Hivi enzi za nyerere huyu mzee Mohd Said alikuwaga wapi? Imekuaje anaonekane vocal sana kipindi hiki kwenye mitandao inayopitiwa na vijana zaidi huku akiwaaminisha kwamba yeye ndo anayejua tulikotoka, tulipo, na tunapokwenda!! Kweli kama ana kipaji cha maono na akiwa ni mwanahistoria mzuri kama anavyojitanabaisha humu JF kwa data ambazo ninazidoubt ilikuwaje akaachwa nje ya uongozi wa mwalimu au hata mwinyi au hata mkapa!? asichaguliwe kuongoza wananchi wa japo eneo analoishi tu??

Humu mitandaoni ni vijana zaidi wamo... ni kwa nini asishiriki katika ligi za wazee wenzake kina warioba, Agustino Rama, Kingunge, Iddi Simba etc etc. ili tumuone ubavu wake akipambana na wazee wenzake kwenye jumuia za carriber yake? Humu amebaki kutema sumu na kupotosha vijana na kujenga chuki miongoni mwa wakristu na waislamu akijificha nyuma ya key-board bila kujali ni madhira gani yataipata nchi yetu usoni pindi mbegu anazopanda zitakapo komaa.

Hata huko nje anakoalikwa nna imani anatumika tu kama sample ya kufundishia wanafunzi waelewe ni jinsi gani binadamu anavyoweza badili historia ya kweli ikaonekana ni ubatili mtupu na akaingiza uongo unaompa advantage yeye na ukasupportiwa na vijidocument vya hapa na pale kisha akakomaa na huo uongo to the extent ya kupata wafuasi na waumini ambao ni wavivu wa kuthibitisha mambo na kufanya utafiti.

Huyu mzee hata sura yake hajulikani barabara tofauti na mch. Mtikila ambaye anajulikana live! kaandika hii makala kwa uoga wa hali ya juu kwa kumuogopa Rev. Mtikila, hata heading yake tu ni polite na humo ndani hajamshambulia Rev. vibaya kama anavyomshambuliaga Baba wa taifa Mwl J. K. Nyerere... Hivi ni kwamba anaogopa Mziki wa Mtikila!!?? Au anamheshimu Mtikila zaidi ya Nyerere? Au anasubiria Mtikila akivuta ndo aanze kumshambulia kama anavyomshambulia Kipenzi chetu baba wa taifa Mwl J. K Nyerere!!?

Kwa nini ameandika hii makala kwa kizungu? Unafikiri Rev. Mtikila hajui kizungu?
 
Kwa hiyo John Garang was warmly received by the country where Islam was not tolerated in whatsoever because was the country where Christianity was not tolerated in whatsoever?
All in all,your have not rejected by evidence if part of Tanganyika land was not being sold to Arabs during the Mwinyi presidency!
 
Rais Mtukufu Ally Hassan Mwinyi a.k.a Ruksa alipochukua madaraka ya nchi yetu japo alikuwa mzanzibari kwa malengo kuimarisha umoja na mshikamano wa Muungano, kosa kubwa alilofanya Mwl. Julius Kambarage Nyerere kutuacha na KATIBA iliyotoa fursa ya ukuu na utukufu kwa watalawa. Kuanzia hapo yale mazoea ya kuitana Ndugu yaliondoka sababu tayari amiri jeshi mkuu aliitwa mtukufu.

Mwl.Nyerere hakunyamaza pale alipoona au alipopewa taarifa na watendaji wa serikali juu ya udhaifu wa serikali ya Mwinyi na daima alikemea hadharani. Moja ya kero kubwa ilikuwa Bi Sitti Mwinyi kufanya biashara na kuingilia maamuzi ya serikali kiasi cha baadhi ya maamuzi ya Rais Mwinyi kuendana na matakwa ya Bi Sitti. Hilo ilipelekea Mwl.Nyerere kumchana hadharani IKULU SIO PANGO LA WALANGUZI na HATUWEZI KUENDESHA SERIKALI HADI AULIZWE MKE WAKO.

Augustine Lyatonga Mrema aliibuka na kuwa maarufu kutokana na kasi yake ya kunyoosha mabonde lakini aliondolewa na kundi lililokuwa linanufaika na mfumo au madaraka ya Mtukufu.
Madhaifu aliyofanya Mwinyi akiwa rais wa nchi yetu hayakuhakisi au hayakisi mafunzo na maamrisho ya dini ya kiislamu, labda kwa mpumbavu tu anaweza kujisikia raha nchi kuongozwa na fisadi la kikristo au kiislamu.

Hatujawahi kupata kiongozi aliyesimama kwa ajili ya watanzania, ndio maana tunashindwa japo kununua BVR tu kwa ajili ya kuandikisha wapiga kura.

SHAME ON YOU ALL mnaobishana ujinga
 
Huyu mtu anayeitwa Mohamed Said ni mpuuzi kuliko elimu anayojivunia.

sasa kati ya mtikila anayepinga katiba ya watanzania wenye dini na imani tofauti isijitabanaishe na dini yoyote na Huyu Mohamed anayetaka katiba itambuwe na kutekeleza ya dini moja nani mchochezi?

Huyu alikuwa wa kufunga kunusulu umoja na mshikamano wa watanzania. Kumuacha akiiindelea kuchochea vijana kuwajaza jaziba na hasira kwa hoja za kizushi, muda sio mrefu tutajikuta tunakuwa kama central Africa au Somalia au Syria.

Kila dini ifanye ibada zake kwenye nyumba za ibada wanakopatikana waumini wake, kuingiza mahitaji ya din moja kwenye katiba nikushirikisha wengine kwenye ibada isiyowahusu.

Kila dini ikifanya yake bila kuchanganya wengine nakuheshim mipaka ya wengine tutakuwa salama lakin huko tunakopelekwa sasa hivi hakuna future ya Taifa.
 
Abu Jahal,
Umekasirika pasi na sababu.

Soma nilichoandika ikiwa hukubaliani nami nijibu kwa hoja.

Ukinitukana unakuwa unaufunga mlango wa majadiliano.

Elewa hayo niloandika nimeyatoa kutoka kwenye mswada wangu ambao In Sha Allah utakuwa kitabu.

Mwisho imekuwaje umejipa jina hili la Abu Jahal?

Unajua maana yake?
 
Adolay,
Soma tena bandiko langu.

Hakuna mahali popote nilipoandika kuhusu katiba.
Ikiwa unapenda tujadili katiba fungua uzi mpya.
 
Adolay,
Soma tena bandiko langu.

Hakuna mahali popote nilipoandika kuhusu katiba.

Ikiwa unapenda tujadili katiba fungua uzi mpya.


Unamjadili Mtikila kwa sababu gani kama sio mgogoro wa Katiba na mkanganyiko wa Mahakama ya Kadhi?

au hujui kiini cha hoja yako!
 
Mohamed

unaweza kurejerea title ya hoja yako kisha fafanuwa, ( Man of the moment) what stay behind the two words

1. Man - why this man in this moment

2. Moment - why moment?
 
Wale wanaoshabikia haya mambo ya Udini wajue tu kuwa balaa la kidini likitokea halitochagua,,watanzania tutatafutana,,,tusome kutoka kwa nchi za wenzetu mfano Nigeria,Central Africa,North Ireland etc
 
adolay

Adolay,
Kuwa mimi ni "mpuuzi," hili nakataa.
Wapi ndugu yangu nimezungumza ya katiba?

Hamaki zinakuondolea umakini.
Tulia nisome kisha lete majibu yako.

Nifungwe kwa kosa lipi?
Kwa kuisahihisha historia pale nilipoona imekosewa.

Nifungwe kwa kulifahamisha taifa langu makosa yake.
Nchi haziendeshwi hivi.
 
Last edited by a moderator:
Mohamed

unaweza kurejerea title ya hoja yako kisha fafanuwa, ( Man of the moment) what stay behind the two words

1. Man - why this man in this moment

2. Moment - why moment?

Adolay,
Niandikie Kiswahili tutaelewana vizuri.
 
Nakushangaa unamshambulia Mtikila wakati wewe na Mtikila lenu moja wote ni vinara wa udini Tanzania.Tofauti pekee ni wewe unautetea na kuupigania uislam wakati Mtikila anautetea na kuupigania ukristo.

Ngongo,
Hakuna mashambulizi.

Nimeihifadhi historia ya wakti ule na matokeo yake.
Soma tena kwa makini uone hali ilikuwaje wakati ule wa 1980.
 
Mijitu yote inayoendekeza UDINI ni ya kutoweshwa tu kwanza yenyewe ili yajue uchungu wa vita vya udini...mwenye timamu zake hawezi shabikia haya mauchochezi
 
adolay

Adolay,
Sasa mbona unanitukana?

Wewe ndiye uloniuliza na mie kwa kurahisisha ili tuelewane vizuri ndipo
nikakushauri uandike Kiswahili lugha ambayo sote haitupi shida ili tufahamiane
na nikujibu.

Ndugu yangu badala yake unanitukana.
Si kitu na tuishie hapa hadi hapo ghadhabu zako zitakapotulia.
 
Last edited by a moderator:
Ms,

kwa nini dini inakuchukulia mda sana? Reading your article you know nothing about Sudan. You translate the whole conflict into religious dimension. By the way Christians in Sudan are minorities. Majority are Muslims and animist-non believers in western inspired faith.

I always believe in ones right to free expression, but I always wonder why everything I mean everything you write is in the prism of Religion. Kwa nini mzee wangu? Yaani kweli unaweza ku andikia kwamba Garang alipokelewa udsm just because he was a Christian? Shamelessly you even quantify the Muslim student as 10 percent? Really where do you get this audacity? Kiukweli, at times sikuelewi. Unashindwa hata ku imagine Watu Kama Akina Garang walikuwa wanaamini nini..walipigania nini? You simply bring your bigot statement za dini? Please...MS you can do better for sure.

MS wewe ni msomi wa kipekee.
 
Mohamed Said

Mkuu nazani haija tosheleza kukujua sioni information zako kama wewe ni nani,unafanya nini,umetokea wapi?...At least tuweze kufahamu ni nani ambaye tuna elimishana kama vile tunavyo mfahamu Mtikala.

Then kingine mkuu ambacho nilitaka kukuuliza...Unajua mwisho wa hii mijadala yako ambayo Mara nyingi ina milengo ya Kidini?

Huwa nawaza endapo nitakuwa source ya kupandikiza chuki za Udini ambao utaleta mauji na machafuko sijui furaha yangu itakuwa ni pale watu,ndugu,jamaa na marafiki zangu watako mwaga damu?

Nazani una marafiki/majirani/ndugu wakristu?

Kama ilivyo kwangu nina marafiki,majirani,na ndugu waislam.Najaribu kuwaza kama kweli unawapenda na pia nawaza wanajisikiaje MTU wanaye zani rafiki yao anakuwa katika milengo uliyo nayo.

BADO NAAMINI SISI SOTE NI NDUGU NA MUNGU NI MMOJA ALIYE TUUMBA NA KUTUPA PUMZI AMBAYO TUNA ITUMIA.

EE MUNGU ULIYE TUUMBA NA KUTUPA PUMZI AMBAYO TUNAITUMIA NAOMBA UTUEPUSHE NA MACHAFUKO YA KIDINI MAANA TUNA AMINI KWAMBA UPO WEWE ULIYE TUUMBA NA KUTUPA PUMZI TUNAE KUJUA KAMA MUNGU/ALLAH......AMEN
 
Last edited by a moderator:
Back
Top Bottom