Mamlaka ya Anga Tanzania yakabidhiwa Bawa la Ndege lililookotwa Pemba kwa Uchunguzi

Kurzweil

JF-Expert Member
May 25, 2011
6,622
8,397
Mamlaka ya Anga Tanzania imekabidhiwa rasmi Bawa la Ndege lililookotwa hivi karibuni kisiwa kidogo cha Kojani kwa ajili ya uchunguzi zaidi.

image (1).jpeg


Akikabidhi bawa hilo mkuu wa wilaya Wete Rashid Hadidi Rashid mara baada ya kulipokea bawa hilo kutoka kwa wavuvi walioliokota na kumkabidhi kaimu mkurugenzi wa mamlaka ya Anga Tanzinia Vallery Luanda Chamlungu huko likoni Kojani kisiwani pemba.

Mkuu wa wilaya Wete amewataka wananchi wanaoishi amawanao jishughulisha na uvuvi wanapookota au kuona kitu kisicho cha kawaida au wasicho kifahamu kutoa tarifa serikalini.


image.jpeg


Kwa upande wake kaimu mkurugenzi wa mamlaka ya Anga Tanzania amesema afisi yake imeridhishwa na wavuvi hao kuokota bawa hilo wakalitunza jamba ambalo limewapa faraja nakuamua kuwatunza cheti pamoja na fedha taslimu sh milioni mbili wavuvi hao kama zawadi ya kazi nzuri ya uaminifu wao.

Nao wavuvi hao wameishukuru mamlaka hiyo ya Anga kwa kuwazawadia fedha hizo kwani nijambo wasilo litarajia.

Chanzo: ITV
 
Back
Top Bottom