Mambo ya Zitto Kabwe haya

Mambo ya Zitto Kabwe haya

gOOD ONE ZITTO.... JE NA KWENYEMAJIMBO YA WABUNGE WENGINE WA CHADEMA HALI NI HIYOHIYO? AU KWAKO TU?
 
Yamegaramiwa na serikali kutoka kodi za wananchi, na kazi yake ilikuwa kuiamsha, kuihamasisha na kuisimamia serikali itekeleze hayo:becky:

Hiyo serikali imetoa pesa Kigoma kwa wapinzani tu, mbona serikali hiyo haionyeshi mambo kama hayo maeneo ambayo chama chake kinalalia? Sababu zingine kuitetea serikali zitoeni baada ya kuondoa sun gogles kwenye macho yenu.
 
watanzania tumejaliwa midomo ya kuchonga hata ukipewa mada itayohusu kunanihii wazazi wako utachonga tu!!!!!!!!!!!
tarehe 31 october siku ya kujua mbivu na mbichi!kura ni siri yako
Mimi Kura yangu siyo siri Diwani, Mbunge na Rais ni Chadema...
 
hiyo serikali imetoa pesa kigoma kwa wapinzani tu, mbona serikali hiyo haionyeshi mambo kama hayo maeneo ambayo chama chake kinalalia? Sababu zingine kuitetea serikali zitoeni baada ya kuondoa sun gogles kwenye macho yenu.
na hata kama serikali ndo imegharamia ye kazi yake ni kufuatilia mbona waliomtangulia hawakufanya kama itakiwavyo?go zitto kazi nzuri bwana mdogo.
 
Hongera sana Zitto, nimefurahi sana kukuona kwenye kampeni za Slaa, umefanya kazi nzuri natumai utarudi Bungeni tena.

Kitendo chako cha kuwa kwenye kampeni za Slaa umetufunga mdomo tuliokuwa tuna hofu utakatiza CCM. Tuliongea mengi kwa vile tunakuthamini sana na tunapenda uendelee kuwa upinzani hatutaki upotee. You have probably proved us wrong-angalau kwa muda huu.
 
Nimeshangaa sana majimbo yaliyowatupa wabunge walioitishia sana serikali kwa madai kuwa hawakufanya lolote kwao na kuwatafuta watu ambao ni "marafiki" wa serikali ili wawe wabunge wao.

Kazi ya Mbunge siyo kusimamia au kuanzisha miradi ya maendeleo jimboni kwake, bali ni kuwawakilisha wananchi wake katika kusimimamia na kuikemea serikali ihakikishe kuwa inafanya mambo yake kama ambavyo jamii inavyotaka. Ukishakuwa mbunge mkali unayefanya kazi yako sawasa kiasi cha kuogopwa na serikali, basi serikali hiyo itahakikisha kuwa miradi yote iliyopangwa kufanyika jimboni mwako itatekelezwa kusudi usije ukaikaba koo.

Watanzania tumekuwa na tabia ya utegemezi sana kiasi kuwa tunategemea mbunge eti ndiye atufanyie mambo, kwa mfano niliwahi kusoma ripoti ya mbunge mmoja huko Singida kuwa alitumia pesa zake binafsi kufanya mambo mengi sana pale jimboni mwake. Hiyo ni vizuri lakini alikuwa akifanya hivyo kama sehemu ya philanthropy yake kwa vile ni mtu tajiri, siyo kama mbunge; anaweza kufanya hivyo bila kuwa mbunge, na inaweza kuchukuliwa kuwa hiyo ilikuwa ni hongo.

Niliwahi kusoma ripoti ya mbunge wa Musoma inayoonyesha jinsi gani anavyochangiwa na matajiri duniani ili kujenga miradi ya mendeleo ya hali ya juu sana jimboni kwake, ingawa hilo ni jambo zuri, ni jambo ambalo angeweza kulifanaya bila kuwa mbunge vile vile; kufanya hivyo kama mbunge ni namna ya hongo pia. Iwapo utakuwa na mbunge ambaye ni lobbyist mzuri wa kuleta miradi jimboni hata ambayo haiko kwenye mipango ya serikali, ni vizuri kwa jimbo lakini ni kinyume cha sheria na haitusaidii katika jitihada zetu za kujenga mfumo wa kidemokrasia unaoheshimu sheria; ni hongo pia kwa wapiga kura wake.

Ni vizuri tuwapime wabunge kwa jinsi walivyotekeleza wajibu wao kama wabunge wetu kuliko kuwapima kwa jinsi walivyotuhonga.
 
Hongera sana Zitto, nimefurahi sana kukuona kwenye kampeni za Slaa, umefanya kazi nzuri natumai utarudi Bungeni tena.

Kitendo chako cha kuwa kwenye kampeni za Slaa umetufunga mdomo tuliokuwa tuna hofu utakatiza CCM. Tuliongea mengi kwa vile tunakuthamini sana na tunapenda uendelee kuwa upinzani hatutaki upotee. You have probably proved us wrong-angalau kwa muda huu.[/QUOTE

Kweli ilikuwa kwa kitambo kidogo tu
 
Hivi huyu jamaa hana mpango wa kugombea urais kupitia NCCR kweli? Kama ni kijana wa jembe na nyundo lazima watamtumia kugawa kura za mashabiki wa chadema 2015. Usiniulize hiyo nccr!
 
Hivi huyu jamaa hana mpango wa kugombea urais kupitia NCCR kweli? Kama ni kijana wa jembe na nyundo lazima watamtumia kugawa kura za mashabiki wa chadema 2015. Usiniulize hiyo nccr!
Atagombea kupitia CHAUMMA
 
Back
Top Bottom