Mambo ya Kuzingatia kabla ya kufuga mbwa

Mambo ya Kuzingatia kabla ya kufuga mbwa

Uwe na upendo pia kwa mbwa.La sivyo utamtupa
 
Pure german shephard ukimpata kwa bei nafuu ni 3 mpka 4+ tena hapo unaweza kuuziwa mtoto kwa bei hyo,huyo rot weiller mkubwa ni bajet ya kununua ki ist kabisaa
Mbona ndoto yangu ya kumiliki mbwa inafifia mdogomdogo
 
Yupo german shephard bajet yake 4.5milion,na yupo rotweiller yeye anakwenda kwa 6milion
Nimekuuliza upo wapi eneo mpaka ukatae ile bei? mimi nnao Rottweiler pureeeee.. hiyo Bei wauzie ambao ndo wanaanza kufuga na Hawajui kitu. halaf et unasema rottweiler mkubwa? huyu mkubwa unampeleka wapi au ukisema mkubwa unamaanisha nini
 
Nimekuuliza upo wapi eneo mpaka ukatae ile bei? mimi nnao Rottweiler pureeeee.. hiyo Bei wauzie ambao ndo wanaanza kufuga na Hawajui kitu. halaf et unasema rottweiler mkubwa? huyu mkubwa unampeleka wapi au ukisema mkubwa unamaanisha nini
Huyo ulonae ana umri gani?ntumie picha yake tuyajenge pm
 
Fuga Mbwa wa kawaida hao sijui marotiweiler au pitibuli ni hatari sana,hawa wetu wa uswahilini ukimfuga vizuri kumfungia na kumwachia usiku anakuwa mkali sana ila sio hatarishi kama hiyo midude ya juu.
 
Hiv hawa german sherphd unaweza ukawazoesha kwa wanafamilia??
 
swala la kwanza uwe na uwakika wa chakula cha mbwa kila siku pamoja na chanjo
Kama ni mbwa zetu za kizungu nakushauri kabla ya yote uchanje dawa ya Parvovirus. Usipochanja mbwa akifikisha miaka 3 lazima afe kwa uo ugonjwa.
Mbwa Germany Shepherd(Mbwa wa polisi) wanakufa sana kwa huo ugonjwa, mara ya kwanza, naanza kufuga mbwa wangu alikufa
 
Kwanza ! Hakikisha unalo banda la kumhifadhia huyo mbwa kama ni Wa ulinzi.

Banda inashauriwa lielekezwe upande unaochomoza jua, kwa ajili ya kukauka kwa haraka unapokuwa umelifanyia usafi kwa maana nyingine husaidia kuua wadudu( simple disinfectant)

Weka Chombo cha maji na maji muda wote, weka ubao ulio juu,juu kwa ajili ya kulalia ,kama unaeneo la kutosha mjengee chumba na sebule.

Floor yake isiwe laini saana kuepuka kuteleza, na wala isiwe rough kurahisisha usafi.na iwe na slope kidogo.

Ikiwa ni chumba na sebule ,eneo la sebule weka wavu.eneo la chumba ndo unaweza kulifunika .jenga liwe imara mbwa ana nguvu .

Ukifanikiwa hayo, tafuta mbegu bora ya mbwa, kumbuka mbwa ni aghali, na anataka matunzo.
Jiulize tena unamtaka mbwa kwa ajili ya nini?
 
Mkuuu nikushauri kama huna matumizi nae makubwa sana fuga tu mbwa wa kawaida



Hamini nakwambia, mbwa yoyote ni matunzo tu. Wewe hujawahi kukutana na mbwa wa kawaida na ni mkali hatari.

Uzuri wa wanyama kama mbwa ni matunzo tu. Amini nakwambia mbwa ni matunzo tu, unavomzoea nduvyo atakavyoenda. Hata hao unaoona sijui wa kijerumani mara korea ni kuzoezwa na mafunzo wapewayo na wana ada hulipiwa.

Kama unafuga mbwa kama burudani na ulinzi tafta mbwa yoyote mzuri mbegu nzuri sio ili mradi mbwa.
Mambo unafuga mnyama hata ukichelewesha chakula usalama wako uko matatani acha mkuu.
 
Tafuta fimbo ya muanzi au mpera akijifanya jeuri unatandika hadi anajua yeye ni mgeni tu hapo nyumbani
 
Nimekuuliza upo wapi eneo mpaka ukatae ile bei? mimi nnao Rottweiler pureeeee.. hiyo Bei wauzie ambao ndo wanaanza kufuga na Hawajui kitu. halaf et unasema rottweiler mkubwa? huyu mkubwa unampeleka wapi au ukisema mkubwa unamaanisha nini
Mkuu mm nina mbwa jike mama yake nilimnunua polisi kule Kurasini. Lkn akazaa ktk generation ya 2 hv ya mchanganyiko wa mbwa fulani hv kiuhalisia sijui ni breed gani, hvy kumzaa mbwa nilienae hapa kwangu kwa sasa. Hivyo hy si pure German shepherd. Nataka apandwe ikibidi na pure G. S au mbegu bora zaidi. Je kupandisha mbwa jike kwa mbwa hao ulionao inawezekana? Na je una mbwa aina gani? Na Dar hapa wapatikana wapi? Mimi nipo Chadibwa beach hk Kigamboni.
 
Back
Top Bottom