JituMirabaMinne
JF-Expert Member
- May 4, 2020
- 3,383
- 9,835
Nimejaribu kuweka baadhi ya vitu vichache ambavyo huenda watu wanavifanya na vinaleta shida. Natambua kwamba vipo vingi ila nimeandika vichache tu. Kama kuna mtu anaweza kuongezea, karibu.
Okay sasa tuendelee,
1. Usiwashe gari na kuanza kupiga resi
Ukiwasha gari yako ni vizuri kuiacha ifikie joto lake kabla ya kuanza kuresi. Pia kama unaondoka ni vizuri ukakanyaga accelerator taratibu, Kama utakanyaga kwa nguvu unaweza kufanya clutch bands kwenye gearbox yako kuisha haraka na hivyo gearbox yako haitaishi maisha marefu.
2. Usizidishe mzigo kwenye gari lako
Mizigo mikubwa inaweza kupelekea gearbox kufanya kazi katika joto kubwa kuliko joto lake la kawaida. Hii inaweza kupelekea vitu kusagana harakaharaka ndani ya gearbox yako na hivyo kupunguza urefu wa maisha ya hiyo gearbox. Kama unataka kuvuta tela au kubeba mzigo mkubwa ni vizuri ukarejejea kwenye owners manual ya gari lako.
3. Usiendeshe gari muda mrefu huku ukiwa umefunga spea tairi(temporary spear tyre)
Kuna mtu unakuta amefunga kile kispea tairi kidogo, halafu ndio anaendesha hilo gari kila siku. Kutumia tairi dogo la spea kwa muda mrefu inaweza kuwa na athari kubwa mbili. Moja, inapelekea kubadilika kwa alignment kwenye mfumo wa suspension wa gari yako. Mbili, Unakuwa unaistress gearbox yako na hivyo kuipunguzia urefu wa maisha yake.
4. Usibadili gear gari inapokuwa inatembea
Gearbox za automatic huwa zinakuwa na bands za clutches. Kutegemeana na aina gearbox unaweza kukuta gearbox ina hata bands 8 za clutches. Kila band huwa inakuwa na lock pin. Hivyo kama unabadili gear huku gari inatembea inaweza kupelekea lock pin kuhama kwenye njia yake au hata kuvunjika. Hili likitokea inaweza kupelekea gearbox yako kukosa gear kabisa au kupata gear fulani kwa shida.