Afrika kulikuwa hamna dini. Wazee waliamini mizimu, waliamini miti, waliamini milima, waliamini wazee wao waliotangulia wanawalinda. Kuna wengine waliamini jua na hata moto.
Soma kitabu cha Chinua Achebe, Things Fall Apart, ameeleza vizuri Maisha ya kijiji cha Kiafrika kabla na baada ya dini / Wakoloni kuja Afrika.
Baadhi ya Wamarekani weusi pia wanaamini " Kwanzaa" badala ya Krisimasi. Profesa wao alikuja Afrika na kuona wanakijiji wanatoa mazao kwa mizimu yao ili wabarikiwe tena msimu mwingine. Profesa akawaambia Wamarekani wenzake aliporudi kuwa washerehekee mila zao ( kama vile Afrika ni nchi moja) na leo wanaita Kwanzaa Day. Alitumia lugha ya Kiswahili kuwaambia wenzake washeherekee umoja na upendo wao, nia na imani kuendeleza utamaduni na jamii yao. Kwanzaa imetoka katika zao la "kwanza" la wanakijiji. Kwa kifupi amejitungia sikukuu na kuweka mazao katika mkeka ili mradi na wao wawe na sikukuu kama wazungu.
Dini za leo pia zinaambatana na utamaduni wa nchi. Ndio maana Mtu anaamini Mungu na uchawi, kwa kuwa uchawi ni utamaduni wake. Au anaamini Mungu na pia uwezo wa Binadamu mwenzake kuwa na super power za kutibu kitamaduni n.k.
Katika Dini za Kikristo utaona kule Ufilipino , Hispania au Mexico (wakatoliki) wanaamini Yesu na pia sanamu za watakatifu (saints), kitu ambacho hatuoni Afrika sana. Kuna saints wa kubariki biashara, wagonjwa, watoto, kijiji na kadhalika. Ni sherehe kubwa na sijawahi kuziona Katika jumuiya ya Kikristo Tanzania. Wananchi wanakimbiza masanamu ya watakatifu wao barabarani kwa sherehe kubwa.
Pia katika nchi za kitajiri za ulaya na marekani, utamaduni wao unawaruhusi watu wa jinsia Moja kuoana kanisani. Vitu hivi vinapingwa Afrika kwa kuwa utamaduni wetu ni tofauti. Sina uhakika kama kuna mapadri wa kike Tanzania kama ulaya.
Katika dini ya Kiislamu pia dini na utamaduni upo vile vile. Kuna mashehe wanajifanya wana uwezo wa kutibu kuliko daktari. Mimi binafsi nilimwona mmoja akisoma Quran tukufu huku akitema mate Katika glasi. Akamwambia mgonjwa anywe hayo mate yamsaidia kutibika. Mwengine atasema ni dawa, mimi nilifikiri itampa madhara zaidi mgonjwa kama sheikh ana TB au magonjwa mingine ya kuambukiza. Pia kuna wale wa dini zote wanawaua wazee au zeruzeru kwa sababu za kichawi.
Pia kuna tofauti ya kufuata dini kutokana na desturi ya wananchi. Kuna nchi kama Indonesia ambapo pia wana tabia ya kuomba kwa wazee wao na mizimu , mazao bora. Wananchi wao wengi ni waislamu lakini wanawake wengi hawavai baibui na wamesoma sana na wako huru kimawazo, kimaisha na kimapenzi. Haya Maisha katika nchi yenye waislamu wengi kuliko wote duniani ( milioni 250) ni tofauti na nchi za kiarabu kama Saudi Arabia ambapo mwanamke hana Haki sawa na mwanamme na haruhusiwi kuendesha gari wala kutoka bila baibui au kusafiri peke Yake. Hapo dini imeambatana na utamaduni wa kibedui.
Nawasilisha.