jMali
JF-Expert Member
- Nov 9, 2010
- 8,412
- 5,013
Kunaonekana kusitasita kwa jumuiya ya kimataifa kuchukua hatua baada ya deadline ya kuweka silaha chini kupita, badala ya FDLR kupigwa kama walivyopigwa M23 na wengineo, SADC imeamua kukaa kikao kingine kujadili hatua itakayochukuliwa. Kwa nini FDLR haipigwi moja kwa moja kama M23 kwa kukaidi deadline?
Ni vizuri tukaangalia kwa kina FDLR ni nini (kwa maneno yao wenyewe sio maneno ya Rwanda) na nini kinawatofautisha na vikundi vingine vya waasi nchini DRC.
UASI WA FDLR:
Waasi by definition ni watu wanaoipinga serikali halali kwa silaha. M23 ni waasi kwa kuwa serikali ya kabila ni halali, na M23 ni kundi la askari wa kitutsi toka jeshi la wananchi wa DRC, FARDC, waliojitenga ili kupambana na serikali.
Lakini FDRL ni masalia ya wanajeshi halali wa serikali halali ya Rwanda chini ya juvenal Habyarimana, iliyoangushwa na waasi wa RPA/RPF wakiongozwa na Paul kagame. Wanajeshi hawa walikimbilia DRC baada ya kuzidiwa mapambano. Askari hawa kama wanajeshi wa nchi yoyote duniani walikula kiapo cha kuilinda nchi yao na raia wao (all hutus, tutsis, twa) dhidi ya chochote especially maadui kama waasi RPA/RPF wa Paul Kagame.
Sijui kwa nini baadhi ya watu wanaona kama vile FDLR ni wahuni fulani hivi.
Hebu tufikirie mfano: Tanzania tuvamiwe na waasi, serikali ipinduliwe, jeshi letu lipigwe na kukimbilia msumbiji, hivi jenerali mwamunyange akikusanya kikundi cha wanajeshi wake masalia ya JWTZ huko msumbiji, ili kulinda wakimbizi walioko huko dhidi ya mashambulizi ya hawa waasi walioteka nchi, na kufanya jitihada ya kukomboa Tanzania toka kwa wale waasi, ataonekana wa ajabu? si ndivyo kiapo chake kinavyomtaka afanye au ninakosea?
Mwaka 2005 baada ya kuona ukweli kuwa kutokana na hila/pressure za marekani kwa jumuiya ya kimataifa kama vile misaada ya kifedha, silaha na ufundi, paul kagame amekubalika machoni mwa dunia kuwa kiongozi "halali" wa Rwanda, FDLR iliamua kuachana na mapigano ya silaha, kuweka silaha chini na kukazania upande wa kisiasa.
Waliona kuwa haiwezekani kupigana na Rwanda kijeshi tena, sio tu watashindwa bali hata jumuiya ya kimataifa itawakuwa dhidi yao (kama ambavyo hata humu JF wengi walio dhidi ya FDLR hawajui FDLR ni nini, ila kwa vile wanaitwa "waasi" basi ndio hivyo tena....). So FDLR wakaweka silaha chini na kukazania upande wa siasa ili warudi Rwanda.
Paul kagame kwa kujua uhalali wa madai ya FDLR kisiasa, ndipo akamfadhili Laurent Nkunda kupitia vikundi mbali mbali vya "waasi wa kitutsi" toka jeshi la DRC. Hawa kina Nkunda kazi yao kubwa ilikuwa kuwapiga FDLR ambao walishasema hawataki vita! na kinachoshangaza zaidi, FDLR tatizo lao ni Rwanda sio DRC, hawana matatizo na DRC, sasa iweje 'wacongomani' waasi serikali yao halafu wawapige wao FDLR ambao sio adui?
Kingine ambacho hata chizi alikiona ni kuwa viongozi wote wa hawa "waasi wa kitutsi toka jeshi la DRC", WOTE WALIKUWA WANAJESHI WA RPA ILE ILE ILIYOPINDUA SERIKALI HALALI YA RWANDA AMBAYO FDLR WALIKUWA NDIO WANAJESHI! kwa maana nyingine ni kuwa vita ile ile ya 1994 ilikuwa inaendela DRC kwa majina mengine, FAR ya Rwanda sasa ilikuwa FDLR, na waasi wa RPA kina Nkunda ndio hao CNDP, RCD, M23 etc.
Kutokana na hayo, FDLR ikashindwa kuweka silaha chini, kwani kila wakihadaiwa kuweka silaha chini, Rwanda anafanya hila zake wanajikuta ndio kwanza wanapigwa. Mashitaka yaliyopo sasa dhidi ya viongozi wa FDLR yanatokana na wao kuwachapa UN, Rwanda na DRC waliopigana nao miaka ya 2008-2009, pamoja na kwamba wao hawana mpango wa kupigana na yoyote yule.
MADAI YA FDLR:
FDLR kwa jinsi ninavyojua kwanza walikuwa wanapinga uhalali wa kagame kuwa kiongozi wa Rwanda, uhalali wa RPA n.k, kwa sababu kagame alikuwa muasi aliyepindua nchi, hakuchaguliwa kidemokrasia, ingawa baada ya kuingia kibabe akabadili mifumo inayomuwezesha kuwa sasa awe "anachaguliwa kidemokrasia". Kimsingi wanataka yaliyoamuliwa kwenye mazungumzo ya Arusha yatekelezwe.
Baada ya kupindua nchi, kagame alifuta yale maazimio na kufanya anavyotaka yeye akitumia kisingizio cha kuzuia "genocide against tutsis". Nchi zisizo na unafiki kama Tanzania tunajua kuwa kulikuwa na vita vya miaka minne toka 1990 mpaka 1994 tulipoamua kuweka mazungumzo ili kuvimaliza, lakini kagame anataka genocide ya siku 100 iwe ndio tukio pekee linalomtambulisha yeye nchini rwanda na sio uasi wake.
MADAI YA RWANDA DHIDI YA FDLR:
Rwanda inadai kuwa FDLR ni wauaji wa kimbari. Cha kushangaza haina mashitaka yoyote dhidi ya hao wauaji wa kimbari ambao ni wanachama wa FDLR. FDLR imeundwa mwaka 2000, miaka sita baada ya mauaji ya kimbari ya 1994. kwa nini toka siku zote hizo hawakuwa na orodha ya hao wauaji? Ilitakiwa waseme "fulani na fulani" tulikuwa tunawatafuta toka 1994 sasa wako FDLR. Lakini hawana hilo.
Rwanda vile vile haina tatizo lolote la wanachama wa FDLR kurudi Rwanda endapo tu wataacha kuwa wanachama wa FDLR. In fact Rwanda imeweka programu maalum kwa ajili ya wanachama wa FDLR wanaotaka kuasi chama chao na kurudi Rwanda, watakaporudi watapewa viwanja, nyumba, mafunzo ya ujasiriamali, fedha za kuanzia maisha etc, yote hayo mwananachama atayapata akiachana na FDLR na kukubali propaganda zote za serikali ya kagame. Kwa viongozi wakubwa wa FDLR ndio neema zaidi.
Mwanzilishi wa FDLR, na askari wa zamani wa jeshi la Habyarimana, Paul rwakarabije baada ya kusaliti FDLR na kurudi Rwanda, leo hii ni mkuu wa magereza wa Rwanda! Hivi FDLR inawezaje kuwa kundi la interahamwe na wauaji wa kimbari halafu muanzilishi wake akawa sio tu hana hatia bali anafaa kupewa cheo serikalini?
Wanachama wengi wa FDLR hususani vijana ambao walizaliwa DRC baada ya 1994 wamerudi Rwanda na kufaidi hizo neema zote, lakini wengine waliobaki DRC wenye umri wa kukumbuka nadhani wameshindwa kusaliti nafsi zao. Watakubalije kupewa nyumba na shamba halafu sasa waseme kuwa wazazi na ndugu zao waliouawa na kagame na kuwafanya wakimbilie DRC in the first place walikuwa ni "interahamwe" tu wasiopaswa kukumbukwa (kama alivyowakumbuka victoire ingabire), wakati wao wenyewe wanakumbuka walivyokimbia risasi za kagame kwa neema ya mungu wakiwa na miaka 10? Ni vigumu kwa mwananchama wa FDLR kurudi Rwanda chini ya kagame wakati bado sababu iliyomfanya amkimbie huyo kagame iko pale pale.
Sasa iweje FDLR akirudi Rwanda kwa sharti la kuachana na FDLR apewe nyumba na shamba, lakini FDLR huyo huyo akiwa DRC, ameweka silaha chini anataka mazungumzo ya kisiasa, aambiwe yeye ni interahamwe, na apigwe kijeshi?
UGUMU WA KUIPIGA FDLR:
Ugumu unatokana na hili: FDLR hawapigani! Ni vigumu kwa jumuiya ya kimataifa kama SADC, kuwapiga watu ambao hawapigani. M23 na vikundi vingine vilikuwa vinapigana na serikali na mamlaka zozote ambazo zingewapinga hivyo deadlines ziwepo au zisiwepo wao walikuwa wanafanya mashambulizi hivyo walitakiwa kupigwa.
Kwa upande wa FDLR, wao hawapigani na yoyote yule, hizo silaha zao zilikuwa ni kwa ajili ya kujilinda na mashambulizi ya Rwanda na baadae kwa kiasi fulani DRC ambao walishirikana na Rwanda kuwapiga, na sio vinginevyo. FDLR sio aggressive force toka mwaka 2005. Nimemsikia msemaji wa FDLR akizungumza na ITV wiki iliyopita akisema "kama wanataka kuja kutuua waje tu".
Leo hii majeshi yakienda kule vijijini yatasema yanapigana na nani?
Pili, mataifa yasiyo na unafiki kama Tanzania yanajua kuwa FDLR wana uhalali katika madai yao, hivyo morally hawawezi kukubali FDLR warudishwe kinguvu Rwanda kana kwamba all is now well. Kulikuwa na sababu ya wahutu kukimbia majeshi ya kagame then, na sababu hizo hazijatatuliwa kwa sasa. Ndio maana wenye akili wakasema silaha zikae chini watu waongee. Lakini wasio na akili ndio kwanza wakatishia kumpiga hata aliyetoa wazo hilo!
Ingawa nategemea kuna watu watanipinga katika hili :yell:, lakini FDLR kwa kiasi fulani ni kama ANC ya afrika kusini enzi zile za kupigana na makaburu. ANC yenye silaha na wanajeshi ilikuwa nje ya afrika kusini ikiongozwa na watu kama Nelson Mandela, kina Mbeki n.k ambao walikuwa na kambi zao mpaka huku Tanzania, lakini kimsingi watu wote weusi ndani ya afrika kusini walikuwa wanaunga mkono ANC.
Lakini kutokana na hali ilivyokuwa hawakuweza kujipambanua kuwa na wao ni ANC wakiwa ndani ya afrika kusini, kwa sababu makaburu wangewapiga. "jumuiya ya kimataifa" kama kawaida ikiongozwa na marekani iliweka ANC chini ya definition ya "kikundi cha magaidi", Nelson Mandela aliondolewa kwenye orodha ya magaidi nchini marekani mwaka 2008!, mpaka 2013 bado mpigania uhuru mashuhuri wa ANC, komredi Tokyo sexwale alikamatwa Airport kwa vile jina lake bado lilikuwamo kwenye "orodha ya magaidi wa ANC"!
Katika hali hiyo hiyo, FDLR yenye silaha na inayojulikana ndio iko nje ya Rwanda, DRC, ulaya n.k na kama kawaida imepachikwa nembo ya "negative force", na baadhi ya viongozi wake wana mashitaka mbalimbali. Lakini kama ilivyokuwa kwa ANC, ndani ya Rwanda majority ya watu ni FDLR ingawa ni "mabubu" kama ambavyo ANC ndani ya afrika kusini walikuwa mabubu. FDLR ni kubwa zaidi ndani ya Rwanda kuliko ilivyo DRC. Ndio maana hata watutsi wanaokwenda kinyume na kagame wanashitakiwa kwa kujiunga na FDLR, FDLR ile ile ambayo supposedly ndio iliyowaua wao kwenye mauaji ya kimbari!
UNAFIKI:
Kwa unafiki marekani na wenzie walishinikiza DRC iongee na M23 kule Uganda (of all places!), wakijua fika kuwa M23 hawakuwa na uhalali wowote ule wa kuishinikiza DRC, lengo la M23 lilikuwa ku-destabilize DRC kwa manufaa ya Rwanda. Cha ajabu marekani hao hao, uingereza hao hao walisimamisha misaada Rwanda wakishinikiza Rwanda iachane na M23, lakini hao hao mbona hawashinikizi mazungumzo kati ya FDRL na Rwanda kama walivyofanya kwa M23?, badala yake wanataka FDLR wapigwe tena ikibidi hata kwa makomandoo toka marekani! Kabla M23 hajapigwa aliitwa kampala, akaleta hoja zake mezani zikawa zinajadiliwa kifungu mpaka kifungu, lakini shida yake ikawa wakati mazungumzo yanaendelea na yeye huku anaendelea na vita anasogea sogea ndani ya DRC, ndipo DRC ikaona huu ujinga tukawachapa. Lakini kwa upande wa FDLR na Rwanda hilo halijatokea badala yake wanatakiwa kupigwa tu, why?
Tuzingatie yafuatayo:
Kwa upande wa pili:
Mazungumzo yalifanikiwa kuleta amani South Africa na leo wanaishi kama watu wamoja, sioni kwa nini hilo lisiwezekane Rwanda. Naunga mkono msimamo wa Tanzania wa mazungumzo badala ya vita kwenye suala la FDLR vs Rwanda.
Ni vizuri tukaangalia kwa kina FDLR ni nini (kwa maneno yao wenyewe sio maneno ya Rwanda) na nini kinawatofautisha na vikundi vingine vya waasi nchini DRC.
UASI WA FDLR:
Waasi by definition ni watu wanaoipinga serikali halali kwa silaha. M23 ni waasi kwa kuwa serikali ya kabila ni halali, na M23 ni kundi la askari wa kitutsi toka jeshi la wananchi wa DRC, FARDC, waliojitenga ili kupambana na serikali.
Lakini FDRL ni masalia ya wanajeshi halali wa serikali halali ya Rwanda chini ya juvenal Habyarimana, iliyoangushwa na waasi wa RPA/RPF wakiongozwa na Paul kagame. Wanajeshi hawa walikimbilia DRC baada ya kuzidiwa mapambano. Askari hawa kama wanajeshi wa nchi yoyote duniani walikula kiapo cha kuilinda nchi yao na raia wao (all hutus, tutsis, twa) dhidi ya chochote especially maadui kama waasi RPA/RPF wa Paul Kagame.
Sijui kwa nini baadhi ya watu wanaona kama vile FDLR ni wahuni fulani hivi.
Hebu tufikirie mfano: Tanzania tuvamiwe na waasi, serikali ipinduliwe, jeshi letu lipigwe na kukimbilia msumbiji, hivi jenerali mwamunyange akikusanya kikundi cha wanajeshi wake masalia ya JWTZ huko msumbiji, ili kulinda wakimbizi walioko huko dhidi ya mashambulizi ya hawa waasi walioteka nchi, na kufanya jitihada ya kukomboa Tanzania toka kwa wale waasi, ataonekana wa ajabu? si ndivyo kiapo chake kinavyomtaka afanye au ninakosea?
Mwaka 2005 baada ya kuona ukweli kuwa kutokana na hila/pressure za marekani kwa jumuiya ya kimataifa kama vile misaada ya kifedha, silaha na ufundi, paul kagame amekubalika machoni mwa dunia kuwa kiongozi "halali" wa Rwanda, FDLR iliamua kuachana na mapigano ya silaha, kuweka silaha chini na kukazania upande wa kisiasa.
Waliona kuwa haiwezekani kupigana na Rwanda kijeshi tena, sio tu watashindwa bali hata jumuiya ya kimataifa itawakuwa dhidi yao (kama ambavyo hata humu JF wengi walio dhidi ya FDLR hawajui FDLR ni nini, ila kwa vile wanaitwa "waasi" basi ndio hivyo tena....). So FDLR wakaweka silaha chini na kukazania upande wa siasa ili warudi Rwanda.
Paul kagame kwa kujua uhalali wa madai ya FDLR kisiasa, ndipo akamfadhili Laurent Nkunda kupitia vikundi mbali mbali vya "waasi wa kitutsi" toka jeshi la DRC. Hawa kina Nkunda kazi yao kubwa ilikuwa kuwapiga FDLR ambao walishasema hawataki vita! na kinachoshangaza zaidi, FDLR tatizo lao ni Rwanda sio DRC, hawana matatizo na DRC, sasa iweje 'wacongomani' waasi serikali yao halafu wawapige wao FDLR ambao sio adui?
Kingine ambacho hata chizi alikiona ni kuwa viongozi wote wa hawa "waasi wa kitutsi toka jeshi la DRC", WOTE WALIKUWA WANAJESHI WA RPA ILE ILE ILIYOPINDUA SERIKALI HALALI YA RWANDA AMBAYO FDLR WALIKUWA NDIO WANAJESHI! kwa maana nyingine ni kuwa vita ile ile ya 1994 ilikuwa inaendela DRC kwa majina mengine, FAR ya Rwanda sasa ilikuwa FDLR, na waasi wa RPA kina Nkunda ndio hao CNDP, RCD, M23 etc.
Kutokana na hayo, FDLR ikashindwa kuweka silaha chini, kwani kila wakihadaiwa kuweka silaha chini, Rwanda anafanya hila zake wanajikuta ndio kwanza wanapigwa. Mashitaka yaliyopo sasa dhidi ya viongozi wa FDLR yanatokana na wao kuwachapa UN, Rwanda na DRC waliopigana nao miaka ya 2008-2009, pamoja na kwamba wao hawana mpango wa kupigana na yoyote yule.
MADAI YA FDLR:
FDLR kwa jinsi ninavyojua kwanza walikuwa wanapinga uhalali wa kagame kuwa kiongozi wa Rwanda, uhalali wa RPA n.k, kwa sababu kagame alikuwa muasi aliyepindua nchi, hakuchaguliwa kidemokrasia, ingawa baada ya kuingia kibabe akabadili mifumo inayomuwezesha kuwa sasa awe "anachaguliwa kidemokrasia". Kimsingi wanataka yaliyoamuliwa kwenye mazungumzo ya Arusha yatekelezwe.
Baada ya kupindua nchi, kagame alifuta yale maazimio na kufanya anavyotaka yeye akitumia kisingizio cha kuzuia "genocide against tutsis". Nchi zisizo na unafiki kama Tanzania tunajua kuwa kulikuwa na vita vya miaka minne toka 1990 mpaka 1994 tulipoamua kuweka mazungumzo ili kuvimaliza, lakini kagame anataka genocide ya siku 100 iwe ndio tukio pekee linalomtambulisha yeye nchini rwanda na sio uasi wake.
MADAI YA RWANDA DHIDI YA FDLR:
Rwanda inadai kuwa FDLR ni wauaji wa kimbari. Cha kushangaza haina mashitaka yoyote dhidi ya hao wauaji wa kimbari ambao ni wanachama wa FDLR. FDLR imeundwa mwaka 2000, miaka sita baada ya mauaji ya kimbari ya 1994. kwa nini toka siku zote hizo hawakuwa na orodha ya hao wauaji? Ilitakiwa waseme "fulani na fulani" tulikuwa tunawatafuta toka 1994 sasa wako FDLR. Lakini hawana hilo.
Rwanda vile vile haina tatizo lolote la wanachama wa FDLR kurudi Rwanda endapo tu wataacha kuwa wanachama wa FDLR. In fact Rwanda imeweka programu maalum kwa ajili ya wanachama wa FDLR wanaotaka kuasi chama chao na kurudi Rwanda, watakaporudi watapewa viwanja, nyumba, mafunzo ya ujasiriamali, fedha za kuanzia maisha etc, yote hayo mwananachama atayapata akiachana na FDLR na kukubali propaganda zote za serikali ya kagame. Kwa viongozi wakubwa wa FDLR ndio neema zaidi.
Mwanzilishi wa FDLR, na askari wa zamani wa jeshi la Habyarimana, Paul rwakarabije baada ya kusaliti FDLR na kurudi Rwanda, leo hii ni mkuu wa magereza wa Rwanda! Hivi FDLR inawezaje kuwa kundi la interahamwe na wauaji wa kimbari halafu muanzilishi wake akawa sio tu hana hatia bali anafaa kupewa cheo serikalini?
Wanachama wengi wa FDLR hususani vijana ambao walizaliwa DRC baada ya 1994 wamerudi Rwanda na kufaidi hizo neema zote, lakini wengine waliobaki DRC wenye umri wa kukumbuka nadhani wameshindwa kusaliti nafsi zao. Watakubalije kupewa nyumba na shamba halafu sasa waseme kuwa wazazi na ndugu zao waliouawa na kagame na kuwafanya wakimbilie DRC in the first place walikuwa ni "interahamwe" tu wasiopaswa kukumbukwa (kama alivyowakumbuka victoire ingabire), wakati wao wenyewe wanakumbuka walivyokimbia risasi za kagame kwa neema ya mungu wakiwa na miaka 10? Ni vigumu kwa mwananchama wa FDLR kurudi Rwanda chini ya kagame wakati bado sababu iliyomfanya amkimbie huyo kagame iko pale pale.
Sasa iweje FDLR akirudi Rwanda kwa sharti la kuachana na FDLR apewe nyumba na shamba, lakini FDLR huyo huyo akiwa DRC, ameweka silaha chini anataka mazungumzo ya kisiasa, aambiwe yeye ni interahamwe, na apigwe kijeshi?
UGUMU WA KUIPIGA FDLR:
Ugumu unatokana na hili: FDLR hawapigani! Ni vigumu kwa jumuiya ya kimataifa kama SADC, kuwapiga watu ambao hawapigani. M23 na vikundi vingine vilikuwa vinapigana na serikali na mamlaka zozote ambazo zingewapinga hivyo deadlines ziwepo au zisiwepo wao walikuwa wanafanya mashambulizi hivyo walitakiwa kupigwa.
Kwa upande wa FDLR, wao hawapigani na yoyote yule, hizo silaha zao zilikuwa ni kwa ajili ya kujilinda na mashambulizi ya Rwanda na baadae kwa kiasi fulani DRC ambao walishirikana na Rwanda kuwapiga, na sio vinginevyo. FDLR sio aggressive force toka mwaka 2005. Nimemsikia msemaji wa FDLR akizungumza na ITV wiki iliyopita akisema "kama wanataka kuja kutuua waje tu".
Leo hii majeshi yakienda kule vijijini yatasema yanapigana na nani?
Pili, mataifa yasiyo na unafiki kama Tanzania yanajua kuwa FDLR wana uhalali katika madai yao, hivyo morally hawawezi kukubali FDLR warudishwe kinguvu Rwanda kana kwamba all is now well. Kulikuwa na sababu ya wahutu kukimbia majeshi ya kagame then, na sababu hizo hazijatatuliwa kwa sasa. Ndio maana wenye akili wakasema silaha zikae chini watu waongee. Lakini wasio na akili ndio kwanza wakatishia kumpiga hata aliyetoa wazo hilo!
Ingawa nategemea kuna watu watanipinga katika hili :yell:, lakini FDLR kwa kiasi fulani ni kama ANC ya afrika kusini enzi zile za kupigana na makaburu. ANC yenye silaha na wanajeshi ilikuwa nje ya afrika kusini ikiongozwa na watu kama Nelson Mandela, kina Mbeki n.k ambao walikuwa na kambi zao mpaka huku Tanzania, lakini kimsingi watu wote weusi ndani ya afrika kusini walikuwa wanaunga mkono ANC.
Lakini kutokana na hali ilivyokuwa hawakuweza kujipambanua kuwa na wao ni ANC wakiwa ndani ya afrika kusini, kwa sababu makaburu wangewapiga. "jumuiya ya kimataifa" kama kawaida ikiongozwa na marekani iliweka ANC chini ya definition ya "kikundi cha magaidi", Nelson Mandela aliondolewa kwenye orodha ya magaidi nchini marekani mwaka 2008!, mpaka 2013 bado mpigania uhuru mashuhuri wa ANC, komredi Tokyo sexwale alikamatwa Airport kwa vile jina lake bado lilikuwamo kwenye "orodha ya magaidi wa ANC"!
Katika hali hiyo hiyo, FDLR yenye silaha na inayojulikana ndio iko nje ya Rwanda, DRC, ulaya n.k na kama kawaida imepachikwa nembo ya "negative force", na baadhi ya viongozi wake wana mashitaka mbalimbali. Lakini kama ilivyokuwa kwa ANC, ndani ya Rwanda majority ya watu ni FDLR ingawa ni "mabubu" kama ambavyo ANC ndani ya afrika kusini walikuwa mabubu. FDLR ni kubwa zaidi ndani ya Rwanda kuliko ilivyo DRC. Ndio maana hata watutsi wanaokwenda kinyume na kagame wanashitakiwa kwa kujiunga na FDLR, FDLR ile ile ambayo supposedly ndio iliyowaua wao kwenye mauaji ya kimbari!
UNAFIKI:
Kwa unafiki marekani na wenzie walishinikiza DRC iongee na M23 kule Uganda (of all places!), wakijua fika kuwa M23 hawakuwa na uhalali wowote ule wa kuishinikiza DRC, lengo la M23 lilikuwa ku-destabilize DRC kwa manufaa ya Rwanda. Cha ajabu marekani hao hao, uingereza hao hao walisimamisha misaada Rwanda wakishinikiza Rwanda iachane na M23, lakini hao hao mbona hawashinikizi mazungumzo kati ya FDRL na Rwanda kama walivyofanya kwa M23?, badala yake wanataka FDLR wapigwe tena ikibidi hata kwa makomandoo toka marekani! Kabla M23 hajapigwa aliitwa kampala, akaleta hoja zake mezani zikawa zinajadiliwa kifungu mpaka kifungu, lakini shida yake ikawa wakati mazungumzo yanaendelea na yeye huku anaendelea na vita anasogea sogea ndani ya DRC, ndipo DRC ikaona huu ujinga tukawachapa. Lakini kwa upande wa FDLR na Rwanda hilo halijatokea badala yake wanatakiwa kupigwa tu, why?
Tuzingatie yafuatayo:
- Mahakama ya ICTR ilishurutishwa na marekani kusitisha mashtaka dhidi ya kagame na kundi lake la RPA. Carla del ponte muendesha mashtaka, alifukuzwa kazi mara moja pale alipotaka kumshitaki kagame, na muendesha mashtaka aliyefuatia alikalia faili hili mpaka leo hii ICTR imefungwa!
- kagame anashitakiwa katika mahakama za ufaransa, spain na hata marekani kwenyewe kesi ilizuiwa kwa sababu ya sheria inayozuia marais kushitakiwa marekani, vinginevyo kagame anayo kesi mpaka marekani! kwa kesi hizi hizi za mauaji ya 1994.
- Ripoti za UN zimeweka wazi kuwa kagame na serikali yake wamefanya "genocide against hutus" huko DRC. ripoti hiyo "UN mapping report" imekaliwa na "jumuiya ya kimataifa" (marekani). Haya mauaji ambayo UN wenyewe wanasema ni "genocide against hutus" ndio yanayotengeneza FDLR! Sasa iweje FDLR warudishwe Rwanda bila mazungumzo yoyote yale?
Kwa upande wa pili:
- ICTR haijawahi kumshitaki kiongozi yoyote yule wa FDLR kwa mauaji ya kimbari. Hawa FDLR wanaitwa "interahamwe" kwa vigezo vya mahakama gani? Na kama mwanzilishi wa FDLR yenyewe kapewa ukuu wa magereza Rwanda hawa kweli ni wauaji au wanasiasa wa upinzani?
- Kule ICC nako mashtaka yote dhidi ya viongozi wa FDLR yalifeli wakaachiwa huru, na walivyoachiwa mahakama ya ICC ilisema hivi "no case to answer". Hivi sasa mashtaka yaliyoko dhidi ya viongozi wa FDLR ni kutokana na rufaa ambayo kagame alilazimisha ICC waifungue, ili in exchange awape Bosco Ntaganda. Na bado kagame anamhifadhi Laurent Nkunda ambaye anatakiwa ICC.
Mazungumzo yalifanikiwa kuleta amani South Africa na leo wanaishi kama watu wamoja, sioni kwa nini hilo lisiwezekane Rwanda. Naunga mkono msimamo wa Tanzania wa mazungumzo badala ya vita kwenye suala la FDLR vs Rwanda.