Mambo poa...

Mambo poa...

ZeMarcopolo

Platinum Member
Joined
May 11, 2008
Posts
14,279
Reaction score
7,681
Mambo poa.jpg


Mambo poa...

Hivyo ndivyo wanavyoonekana kusema vijana machachari katika siasa.

Vijana hawa walikuwa Mbulu katika harakati za kujenga nchi.

Tanzania ina kila sababu ya kujivunia vijana wazalendo na jasiri kama hawa.

Mambo poa, na wataendelea kufanya bidii yawe poa zaidi.

Kama ilivyo kwingine duniani, taifa letu pia lina changamoto ya uwepo wa vijana wachache waoga, wasiojiamini. Vijana wa namna hiyo mara nyingi huwa wamejikunyata tu wakingoja kupewa maelekezo ya nini cha kufanya. Hawana ubunifu na ni dhaifa wa fikra.

Vijana wa namna hiyo ni WASALITI wa nafsi zao. Wanatamani wawe na sababu ya kusema mambo poa, lakini hawapati sababu hiyo. Wameshikiwa akili na watu wengine kwa kulaghaiwa kuwa wao ni informers au spies. Kumbe hakuna chochote zaidi ya kushikiwa akili.

Wanapoona wenzao wako mambo poa, wao roho zinawauma. Wanatamani kuwa mambo poa, lakini wamefungwa minyororo kifikra. Hawana fikra huru!

Jifungue kwenye minyororo,kijana jiunge na mambo poa...
 
Zombies! poleni sana. one thing for certain, the grounds beneath your feet have shifted, tafuteni haraka mahali pa kujificha...
 
Zombies! poleni sana. one thing for certain, the grounds beneath your feet have shifted, tafuteni haraka mahali pa kujificha...

Wewe unajitafutia sababu ya kupata vidonda vya tumbo bure, lakini wenzako kama vipi MAMBO POA...
 
hizo rangi ukitaka kichapo pitanazo mtaa mmoja pale mwanza unaitwa makoroboi .ndo utajua ccm inaudhi
 
Wewe unajitafutia sababu ya kupata vidonda vya tumbo bure, lakini wenzako kama vipi MAMBO POA...

Hawa vijana ni kiboko mpaka wamekugeuza umekuwa teja lao, one word have turned you into nothing walikwambia wana habari zako nyingi maisha yako yako mikononi mwao,wakakwambia ukikohoa tu watamwaga mchele kwenye kuku wengi ,kilichotokea kuwa kipeperushi chao ,very sorry for you the expected PhD holder
 
Vijana tulikuwa wakati wa TANU na mwanzoni mwa miaka ya 80 sasa hivi hakuna kitu, hakuna anayefahamu siasa ambazo za maana bali ni kuropoka na kuwasema watu, ndiyo maana sisi waanzilishi wa umoja wa vijana enzi za TANU tunawashangaa sana maana badala ya kunadi chama sasa watu wanajinadi na ku-attack personalities, hakika siasa uchwara kabisa, enzi zetu Lumumba na hapo njia panda ya UWT tulikaa vichwa vya chama na tulifanya kazi hasa inayoeleweka, tuliuujua uzalendo na tuliutekeleza kwa vitendo na siyo kuwa na kadi tu. Inasikitisha sana, sioni cha kusifu hapo.
 
Nahisi siasa ya Tanzania huwa inatengua oblongata

Nilipata kuangalia TV Show moja inaitwa CSI:Las Vegas, kuna bwana mmoja anaitwa "William Petersen"...

Huyu bwana alisema, "ukichukua wanyama kadhaa(akawataja kwa majina) ukapima uwezo wa akili zao, utashangaa kukuta akili ya mwanasiasa imezidiwa na hao wanyama aliowataja na mbaya zaidi hata nguruwe ana akili kuliko wanasiasa"
 
Nilipata kuangalia TV Show moja inaitwa CSI:Las Vegas, kuna bwana mmoja anaitwa "William Petersen"...

Huyu bwana alisema, "ukichukua wanyama kadhaa(akawataja kwa majina) ukapima uwezo wa akili zao, utashangaa kukuta akili ya mwanasiasa imezidiwa na hao wanyama aliowataja na mbaya zaidi hata nguruwe ana akili kuliko wanasiasa"
Mo mu mo
 
942515_617153594963121_1994579558_n.jpg


Lini mtapitisha tena mgao wa ugua pole?
 
Inawezekana kabisa

Maana kuna mambo mengine ni vigumu kuyaelewa kwa akili ya kawaida

Nilipata kuangalia TV Show moja inaitwa CSI:Las Vegas, kuna bwana mmoja anaitwa "William Petersen"...

Huyu bwana alisema, "ukichukua wanyama kadhaa(akawataja kwa majina) ukapima uwezo wa akili zao, utashangaa kukuta akili ya mwanasiasa imezidiwa na hao wanyama aliowataja na mbaya zaidi hata nguruwe ana akili kuliko wanasiasa"
 
Mambo poa...

Hivyo ndivyo wanavyoonekana kusema vijana machachari katika siasa.

Vijana hawa walikuwa Mbulu katika harakati za kujenga nchi.

Tanzania ina kila sababu ya kujivunia vijana wazalendo na jasiri kama hawa.

Mambo poa, na wataendelea kufanya bidii yawe poa zaidi.

Siku hizi katika moja ya vitu vinavyojenga nchi ni watu kuonyesha wakinywa vinywaji!!!, Hiyo iko kitabu gani tukaperusi nasi.
Pia siku hizi uzalendo ni kuongoza kwa kula misosi!!!!
Nadhani muda si mwingi utakuwa sociologist wetu mzuri.
 
Kukubali kutumika hadharani kama hawa? Lazima blongata haziko sawa
Na nikifikiria yanayoendelea bungeni??!!!!!

Yanayoendelea bungeni ni kwasababu mbili tu za msingi;
Mosi, Spika ameshindwa kulimudu bunge kwahiyo anayumbayumba hadi atakapopata pa kushika ndipo mambo yanakwenda.
Pili wabunge wamebuni mbinu mpya ya kujiongezea posho kwa kufanya mambo ya kihuni ili tu bunge liahirishwe na by default siku za mijadala zinaongezeka na hivyo wataendelea kuhudhuria chako ni chako.
 
Wasubiri ukuu wa wilaya

Sent from my BlackBerry 8520 using JamiiForums
 
Vijana wamependeza kwel ccm oyeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeee
 
Ingekuwa ni vijana wa CHADEMA wachangiaji wangefikia idadi ya 132000!!!!
 
Back
Top Bottom