Mambo muhimu ya kufahamu unapojiandaa kubeba Ujauzito

Miss Zomboko

JF-Expert Member
May 18, 2014
4,501
9,279
Vipimo na tafiti muhimu kufanya kabla ya kupata ujauzito

Ikiwa umeamua kufanya vipimo vya awali kabla ya kupata ujauzito, mtaalamu wako wa afya au nesi anaweza kukuliza kuhusu:

Kazi yako-atakuuliza kama kazi yako inahusisha kufanya kazi na vitu hatari
Kama una tatizo na siku zako za hedhi
Hali yako ya afya na maisha kiujumla
Mazoezi unayofanya na kiasi gani
Unajisikiaje-kihisia (emotional wellbeing)
Utaratibu wako wa kula
Daktari wako atapenda kujua hali yoyote ya kiafya ulionayo kama:

Kisukari
Pumu
Shinikizo la damu
Kifafa
Matizo ya tezi
Matatizo ya moyo
Magonjwa ya akili
Mambo mengine yakujadili katika vipimo hivi vya awali kabla ya kupata ujauzito ni kama:

Kama katika familia yenu kuna magonjwa ya kurithi. Mueleze mshauri wako wa afya kama kuna historia ya magonjwa ya kurithi katika familia yenu kama selimundu, magonjwa ya mfumo wa upumuaji(uvimbe wa viriba hewa) au anemia.

Matumizi ya uzazi wa mpango. Mara nyingi, njia za uzazi wa mpango ulizotumia haziwezi kuathiri mda gani umekaa bila kupata ujauzito. Lakini kama ulikua unatumia sindano, inaweza kuchukua mpaka mwaka mmoja baada ya sindano yako ya mwisho, taratibu za uzazi wako kurudi hali ya awali.

Daktari wako anaweza kuuliza kuhusu mimba ulizotoa, zilizoharibika au kutungwa nje ya mji wa uzazi(ectopic pregnancy), kuongelea matukio haya inaweza kurudisha huzuni, hivyo ni vizuri kumwambia daktari wako ili aweze kukupa ushauri na huduma nzuri sasa.

Je, nifanye vipimo na matibabu kabla ya kujaribu kupata mtoto?

Ndio, ni muhimu kufanya vipimo, ila inategemea na hali yako na afya kwa ujumla. Muulize mshauri wako wa afya au muuguzi kama unahitaji kufanya vipimo kabla ya kupata ujauzito. Uchunguzi wa kawaida na vipimo kabla ya ujauzito ni pamoja na:

Vipimo vya magonjwa ya zinaa:

Kama uliwahi kufanya ngono isio salama, ni vema kufanya uchunguzi wa magonjwa ya kuambukizwa ya ngono, hatakama hakuna dalili. Ni vema kufanyiwa vipimo vya:

Homa ya ini
Klamidia
Kaswende
Virusi vya Ukimwi (HIV) . Kufanya matibabu ya magonjwa ya ngono mapema kabla ya kupata mimba kunaongeza nafasi ya kuwa na mafanikio kwenye ujauzito.
Vipimo vya kizazi:

Ikiwa unatoka kufanya uchunguzi wa kizazi fanya mwaka mmoja kabla ya kujaribu kupata ujauzito. Hii ni kwa sababu uchunguzi wa kizazi haufanyiki wakati wa ujauzito, kwani mabadiliko ya asili ya kizazi chako hufanya matokeo kuwa magumu kutafsiri.

Vipimo vya damu:

Ikiwa unafanya vipimo vya awali kabla ya ujauzito, na mshauri wako wa afya au muuguzi wako akawa na wasiwasi una anemia, atakushauri ufanye vipimo hivi. Hii ni kwasababu wanawake wenye anemia mara nyingi wanahitaji kutumia madini ya chuma ya ziada kipindi cha ujauzito.

Kulingana na asili ya kabila na historia yako ya matibabu, kuna uhitaji wa kufanya vipimo vya magonjwa ya kurithi kama siko seli na anemia. Vipimo hivi vitakupatia uhakika na ufahamu wa kujua ni kiasi gani utamrithisha mwanao hali hii ya kiafya.

Ikiwa hauna uhakika kama umepatiwa chanjo ya rubella, unaweza kufanyiwa vipimo vya damu kuangalia.

Je, nipate chanjo kabla ya kujaribu kupata mtoto?

Maambukizi mengi yanaweza sababisha uharibifu wa ujauzito au kasoro baada ya kuzaliwa, hakikisha unapata chanjo kwa mda. Kama unahitaji chanjo ya magonjwa ya virusi kama rubella, inabidi kusubiri mwezi mmoja kabla ya kujaribu kupata mtoto. Chukua tahadhari, kwani inasadikika mwili wako unahitaji muda wa kuangamiza kirusi kabla ya kubeba mimba.

Kama uko katika hatari za ugonjwa wa homa ya ini, unaweza kuamua kupata chanjo dhidi ya ugonjwa huu. Hivyo basi kama hii ni chanjo pekee ulionayo, unaweza kuanza kujaribu kupata mtoto mara moja.

Mkunga wako atatumia taarifa uliyompatia kuamua kama unahitaji huduma zaidi kutoka kwa mtaalamu wa afya ya uzazi au vinginevyo.

Pia atakushauri:

Kufanya mazoezi wakati wa ujauzito hasa mazoezi ya sakafu ya nyonga
Kutumia virutubisho kama foliki asidi na vitamin D
Kula kwa afya
 
Mada Nzuri sana hii!

Emdelea mleta mada kuandika mfano namna ya kuweza ku conveive kwa haraka ni nini kifanyike ijapokuwa mimba nyingi huja bila kupangwa

Na hiyo Ndiyo Africa inakuwa na athari hasi.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom