Mambo 20 yaliyotusumbua shule za msingi

Mambo 20 yaliyotusumbua shule za msingi

Rasokauzu

JF-Expert Member
Joined
Apr 27, 2014
Posts
518
Reaction score
303
MAMBO 20 YALIYOTUSUMBUA SHULE ZA MSINGI.

1.Unaenda shule umechelewa unakuta mwalimu anakamata wachelewaj unaamua urudi nyumbani tu.

2.Unachukua kimbegu cha ubuyu unasugua sakafuni afu unamuunguza mwenzio

3.mkiruhusiwa tu unakimbia unataka uwe wa kwanza kwenye njia yenu y kurudia nyumban

4.MTU akikukera unamfungia shule (mnapigana baada ya kufunga shule)

5.MTU akikunyima kitu chake unamwambia "Ahaa eeh utaona sa nne"

6.wadada wembamba ndo wanaongoza kwa kusuta wenzao

7.ukiibiwa daftar jipya unalia kuliko hata uliloandika

8.unajaza mapeni kwenye mkebe(compass) na mengine hayaandiki

9.vifaa vingine kwenye mkebe hujawahi hata kuvitumia mfano bikari labda utolee mwiba

10.hakuna habari nzuri kama kuambiwa Leo hamna shule au mwalimu hayupo

11.habari mbaya zaidi ni kurudi nyumbani kutoka shule una njaa alafu unaambiwa chakula mgeni kaja tumempa

12.mtoto wa mwalimu utamgundua tu kwanzia sweta begi na viatu vyake

13.usiombee umpige mtoto wa mwalimu utatamani uache shule

14.unatengeneza kifutio cha ndala alafu unatishia eti kinafuta hadi peni

15.ukaguzi na huna ufagio.. unaomba chelewa kwa watu af unaongeza kijiti katikati

16.siku ukienda na ufagio wanakagua maji, ukienda na naji wanakagua kuni au mbolea


17.Siku ya jumpili usiku unalala mapema kuanzia saa 2

18. Unaweka Nguo za shule chini ya godoro ili zijinyooshe ( kama pasi vile).

19. Unawahi usku km saa kumi na moja kuwahi mamba endapo wiki iyo mwalimu Wa zamu ni mkali ( kama Mwl katarina).

20. Kumuogopa kiranja kuliko mwalimu Wa kawaida.

Ongezea mengine tujue kweli na wewe ni mhenga
 
Hii thread umeileta wakati mbaya. Mtani sa ivi ndio anapiga domo kishenzi. Naomba nitarudi baadae. Maana
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom