I am Groot
JF-Expert Member
- Jul 20, 2018
- 3,730
- 10,033
Unakumbuka haya enzi za shule?
Kama umesoma shule za msingi za serikali miaka ya '80 mpaka '90 utakuwa unayajua haya…
1. Unaenda shule umechelewa unakuta mwalimu anakamata wachelewaji unaamua urudi nyumbani.
2. Unachukua kimbegu cha ubuyu unasugua sakafuni halafu unamuunguza mwenzio.
3. Mkiruhusiwa tu unakimbia unataka uwe wa kwanza kwenye njia yenu ya kurudia nyumbani.
4. MTU akikukera unamfungia shule (mnapigana baada ya kufunga shule)
5. MTU akikunyima kitu chake unamwambia "Ahaa eeh utaona saa nne" siku ukipata chako hakika atajuta kwa nini alikunyima.
6. Wadada wembamba ndo wanaongoza kwa kusuta wenzao
7. Ukiibiwa daftari jipya unalia kuliko hata uliloandika.
8. Unajaza mapeni kwenye mkebe (compass) na mengine hayaandiki.
9. Vifaa vingine kwenye mkebe hujawahi hata kuvitumia mfano bikari labda utolee mwiba😂
10. Hakuna habari nzuri kama kuambiwa Leo hamna shule mwalimu hayupo.
11. Habari mbaya zaidi ni kurudi nyumbani kutoka shule una njaa halafu unaambiwa chakula mgeni kaja tumempa
12. Mtoto wa mwalimu utamgundua tu kwanzia sweta, begi na viatu vyake.
13. Usiombee umpige mtoto wa mwalimu utatamani uache shule
14. Unatengeneza kifutio cha ndala halafu unatishia eti kinafuta hadi peni😂
15. Ukaguzi na huna ufagio.. unaomba chelewa kwa watu halafu unaongeza kijiti katikati.
16. Siku ukienda na ufagio wanakagua maji, ukienda na maji wanakagua kuni au mbolea😆
😂
17. Kuweka Kioo chini ya Sketi...!!
Dah shule zetu hizi kiboko!!
Ipi umeipitia wewe...??
Kama umesoma shule za msingi za serikali miaka ya '80 mpaka '90 utakuwa unayajua haya…
1. Unaenda shule umechelewa unakuta mwalimu anakamata wachelewaji unaamua urudi nyumbani.
2. Unachukua kimbegu cha ubuyu unasugua sakafuni halafu unamuunguza mwenzio.
3. Mkiruhusiwa tu unakimbia unataka uwe wa kwanza kwenye njia yenu ya kurudia nyumbani.
4. MTU akikukera unamfungia shule (mnapigana baada ya kufunga shule)
5. MTU akikunyima kitu chake unamwambia "Ahaa eeh utaona saa nne" siku ukipata chako hakika atajuta kwa nini alikunyima.
6. Wadada wembamba ndo wanaongoza kwa kusuta wenzao
7. Ukiibiwa daftari jipya unalia kuliko hata uliloandika.
8. Unajaza mapeni kwenye mkebe (compass) na mengine hayaandiki.
9. Vifaa vingine kwenye mkebe hujawahi hata kuvitumia mfano bikari labda utolee mwiba😂
10. Hakuna habari nzuri kama kuambiwa Leo hamna shule mwalimu hayupo.
11. Habari mbaya zaidi ni kurudi nyumbani kutoka shule una njaa halafu unaambiwa chakula mgeni kaja tumempa
12. Mtoto wa mwalimu utamgundua tu kwanzia sweta, begi na viatu vyake.
13. Usiombee umpige mtoto wa mwalimu utatamani uache shule
14. Unatengeneza kifutio cha ndala halafu unatishia eti kinafuta hadi peni😂
15. Ukaguzi na huna ufagio.. unaomba chelewa kwa watu halafu unaongeza kijiti katikati.
16. Siku ukienda na ufagio wanakagua maji, ukienda na maji wanakagua kuni au mbolea😆
😂
17. Kuweka Kioo chini ya Sketi...!!
Dah shule zetu hizi kiboko!!
Ipi umeipitia wewe...??