Mambo 10 tuliyofanikiwa katika kilimo chini ya Rais Samia Suluhu

Nyabukika

JF-Expert Member
Jun 15, 2022
1,402
942
Tanzania ina eneo linalofaa kwa kilimo Hekta milioni 44 na linalofaa kwa umwagiliaji Hekta milioni 29, mpaka sasa zaidi ya 60% ya watanzania wameajiriwa katika kilimo. Biashara ya kilimo katika soko la Afrika inatarajiwa kuwa na Dola Trilioni 1 hadi kufika mwaka 2030. Mapinduzi yanayofanywa na Rais Samia katika sekta hii;

1.Serikali imefanikiwa kufungua masoko mapya ya mazao nje ya nchi hususan zao la parachichi katika nchi za India na Afrika Kusini baada ya kukidhi viwango vya ubora.

2.Serikali imefanikiwa kupata maghala ya kukodi nje ya nchi kwa ajili ya kuhifadhi nafaka yenye uwezo wa kubeba tani 5,000 nchini Sudan Kusini, tani 2,000 nchini Congo na jitihada hizi zinaendelea ili kufungua maghala mengine China, Vietnam na UAE.

3.Serikali imeweza kuongeza bajeti ya utafiti kutoka shilingi bilioni 7.35 hadi bilioni 11. Pia, serikali imeona umuhimu wa kugawa vipima udongo kwenye Halmashauri 143, simu janja pamoja na visanduku vya kutolea huduma 3,300.

4.Serikali imeweka nia ya kuwezesha upatikanaji wa Ithibati ya Ubora kwa ajili ya maabara yenye viwango vya ubora vya kimataifa kwa ajili ya Mamlaka ya mimea na viuatilifu, hatua hii itasaidia kuhakiki ubora wa mazao ya Tanzania.

5. Mwaka 2020, serikali ilifanya majaribio ya kutoa ruzuku za pembejeo kwa wakulima ambapo jaribiohilo limetoa matokeo mazuri hivyo Serikali chini ya uongozi wa Rais Samia imeamua kuwepo na Mfuko Maalum wa Pembejeo ili kuwasaidia wakulima.

6. Serikali imeweza kuongeza bajeti ya huduma za Ugani kutoka TZS bilioni 17.7 hadi TZS bilioni 51.45, kuongeza fedha za uzalishaji wa mbegu kutoka TZS bilioni 5.42 hadi TZS bilioni 10.58, sambamba na kuongeza bajeti hiyo, tumewezesha NFRA na Bodi ya Mazao Mchanganyiko kwa jumla ya TZS bilioni 129 ili waweze kufanya kazi zao vizuri.

7. Serikali kupitia Benki ya kilimo Tanzania Agricultural Development Bank (TADB) imeweza kuwa mdau mkubwa kuwezesha mabenki kutoa mikopo kwa wakulima, Hadi sasa benki zinazotoa mikopo kwa wakulima zimefikia 14. 8. Serikali imeelekeza kuanza kujengwa maghala maeneo ya vijijiji walipo wakulima ili wanapovuna waweze kuweka mazao yao ndani ya maghala ili kuondoa tatizo la upotevu wa mazao na ili mnunuaji anapokuja ayakute katika hali nzuri.

9. Serikali pia inalenga kuongeza thamani ya mazao yanayouzwa nje kutoka Dola za Marekani bilioni 1.2 hadi Dola za Marekani bilioni 5. Aidha, serikali ililenga kuongeza idadi ya mashamba makubwa kutoka 110 hadi 1,000.

10. Serikali imeendelea kuimarisha huduma za Ugani, ambapo kwa siku ya tarehe 4 April 2022 ziligawiwa pikipiki 6,700 ambapo pikipiki 300 zilishatangulia na kufanya jumla ya pikipiki kufikia 7,000 kwa Maafisa Ugani wote.

KILIMO NI AJIRA PIA KILIMO NI BIASHARA NA SIO UMASIKINI
 
Good
Tuwekeze Sana kwenye Eneo Hili
Ngano
Sukari ( Jitihada naziona Mkulanzi)
Mafuta ya Alizeti, Mawese,ufuta nk
Hizi ni Baadhi ya Bidhaa ambazo ni aibu kufika 2030 yapasa 100% ziwe zinazalishwa hapa ndani soko lipo ndani na hata kwa jirani
Nawapongeza Bajeti ikatekelezwe kweli na sio maneno
 
Good
Tuwekeze Sana kwenye Eneo Hili
Ngano
Sukari ( Jitihada naziona Mkulanzi)
Mafuta ya Alizeti, Mawese,ufuta nk
Hizi ni Baadhi ya Bidhaa ambazo ni aibu kufika 2030 yapasa 100% ziwe zinazalishwa hapa ndani soko lipo ndani na hata kwa jirani
Nawapongeza Bajeti ikatekelezwe kweli na sio maneno
Kwa upande wa kilimo serikali ya Rais Samia Suluhu inaupiga mwingi sana maana kilimo kimekua rahisi sana
 
Serikali imefanikiwa kudhibiti mfumuko wa bei za bidhaa mbali mbali.

Serikali imefanikiwa kupunguza tozo ya miamala ya pesa mtandao kwa asilimia 30
 
Hiyo Bajeti ya Kilimo Tshs bilioni 700 na ushee inatosha kuendesha ajira kuu ya Watanzania?
Yaani ili angalau tufanye Kilimo cha maana angalau Bajeti ya Kilimo iwe 10-15% ya Bajeti ya nchi.
 
Sure Serikali ya Rais Samia imetubadilisha mitazamo before watu walikiona kilimo kama umasikini lakini sasa tumejua kilimo ni biashara pia ni ajira ndio maana wamekifanya kiwe rahisi zaidi
Na sasa vijana wajiandae kulamba asali kwenye kilimo 👇
 

Attachments

  • Screenshot_20220805-093409.png
    Screenshot_20220805-093409.png
    279.6 KB · Views: 6
  • Screenshot_20220804-140428.png
    Screenshot_20220804-140428.png
    242.8 KB · Views: 6
  • Screenshot_20220804-135040.png
    Screenshot_20220804-135040.png
    53.7 KB · Views: 6
Mengi yanasemwa kufanyika kwenye eneo la kilimo lakini nadhani bado upatikanaji wa pembejeo umekuwa mgumu sana miongoni mwa wakulima wadogo wadogo. Bado kuna mambo yanahitajika kufanyika kivitendo ili kufikia adhma ya serikali ya awamu ya 5 kwenye eneo la kilimo
 
Serikali imefanikiwa kudhibiti mfumuko wa bei za bidhaa mbali mbali.

Serikali imefanikiwa kupunguza tozo ya miamala ya pesa mtandao kwa asilimia 30
Exactly imesaidia pia kukipa kilimo kipaumbele na kukiwezesha kua kilimo cha biashara na ajira pia imetoa ruzuku ya mbolea, pia imeandaa mashamba kwaajili ya vijana
 
Mengi yanasemwa kufanyika kwenye eneo la kilimo lakini nadhani bado upatikanaji wa pembejeo umekuwa mgumu sana miongoni mwa wakulima wadogo wadogo. Bado kuna mambo yanahitajika kufanyika kivitendo ili kufikia adhma ya serikali ya awamu ya 5 kwenye eneo la kilimo
Serikali ya awamu ya sita ipo makini sana inatimiza kila ahadi kwa vitendo kama unafatilia vizuri Sekta ya kilimo sasa imepewa kipaumbele na kilimo kimelahisishwa ata pembejeo za kilimo zinapatikana kwa bei nafuu kabisa
 
Tanzania ina eneo linalofaa kwa kilimo Hekta milioni 44 na linalofaa kwa umwagiliaji Hekta milioni 29, mpaka sasa zaidi ya 60% ya watanzania wameajiriwa katika kilimo. Biashara ya kilimo katika soko la Afrika inatarajiwa kuwa na Dola Trilioni 1 hadi kufika mwaka 2030. Mapinduzi yanayofanywa na Rais Samia katika sekta hii;

1.Serikali imefanikiwa kufungua masoko mapya ya mazao nje ya nchi hususan zao la parachichi katika nchi za India na Afrika Kusini baada ya kukidhi viwango vya ubora.

2.Serikali imefanikiwa kupata maghala ya kukodi nje ya nchi kwa ajili ya kuhifadhi nafaka yenye uwezo wa kubeba tani 5,000 nchini Sudan Kusini, tani 2,000 nchini Congo na jitihada hizi zinaendelea ili kufungua maghala mengine China, Vietnam na UAE.

3.Serikali imeweza kuongeza bajeti ya utafiti kutoka shilingi bilioni 7.35 hadi bilioni 11. Pia, serikali imeona umuhimu wa kugawa vipima udongo kwenye Halmashauri 143, simu janja pamoja na visanduku vya kutolea huduma 3,300.

4.Serikali imeweka nia ya kuwezesha upatikanaji wa Ithibati ya Ubora kwa ajili ya maabara yenye viwango vya ubora vya kimataifa kwa ajili ya Mamlaka ya mimea na viuatilifu, hatua hii itasaidia kuhakiki ubora wa mazao ya Tanzania.

5. Mwaka 2020, serikali ilifanya majaribio ya kutoa ruzuku za pembejeo kwa wakulima ambapo jaribiohilo limetoa matokeo mazuri hivyo Serikali chini ya uongozi wa Rais Samia imeamua kuwepo na Mfuko Maalum wa Pembejeo ili kuwasaidia wakulima.

6. Serikali imeweza kuongeza bajeti ya huduma za Ugani kutoka TZS bilioni 17.7 hadi TZS bilioni 51.45, kuongeza fedha za uzalishaji wa mbegu kutoka TZS bilioni 5.42 hadi TZS bilioni 10.58, sambamba na kuongeza bajeti hiyo, tumewezesha NFRA na Bodi ya Mazao Mchanganyiko kwa jumla ya TZS bilioni 129 ili waweze kufanya kazi zao vizuri.

7. Serikali kupitia Benki ya kilimo Tanzania Agricultural Development Bank (TADB) imeweza kuwa mdau mkubwa kuwezesha mabenki kutoa mikopo kwa wakulima, Hadi sasa benki zinazotoa mikopo kwa wakulima zimefikia 14. 8. Serikali imeelekeza kuanza kujengwa maghala maeneo ya vijijiji walipo wakulima ili wanapovuna waweze kuweka mazao yao ndani ya maghala ili kuondoa tatizo la upotevu wa mazao na ili mnunuaji anapokuja ayakute katika hali nzuri.

9. Serikali pia inalenga kuongeza thamani ya mazao yanayouzwa nje kutoka Dola za Marekani bilioni 1.2 hadi Dola za Marekani bilioni 5. Aidha, serikali ililenga kuongeza idadi ya mashamba makubwa kutoka 110 hadi 1,000.

10. Serikali imeendelea kuimarisha huduma za Ugani, ambapo kwa siku ya tarehe 4 April 2022 ziligawiwa pikipiki 6,700 ambapo pikipiki 300 zilishatangulia na kufanya jumla ya pikipiki kufikia 7,000 kwa Maafisa Ugani wote.

KILIMO NI AJIRA PIA KILIMO NI BIASHARA NA SIO UMASIKINI
Hakuna kitu, hapa sema tu Serikali ishukuru kuongoza Taifa la wapumbavu, Hivyo unavyo vitaja havipo Nchi yoyote ile ilio piga mapinduzi ya Kilimo.

Nikuambia mataifa yote yalio fanya mapinduzi ya Kilimo yaliwekeza vilivyo yaanu bajeti zao za kilimo ni kubwa kuliko hata za Ulinzi.

Unazungumzia kuongeza sijui nini fullu usaniii mtupu.

Huwezi taja mapinduzi ya Kilimo wakati zilizo kuwa shule za Michepuo ya Kilimo zimekufa,

Huwezi taja mapinduzi ya Kilimo wakati vyuo vya kilimo vingi viko taabani na yamrvakia magofu tu.

Eti maghara nje ya nchi ya kuhifadhi tani 5000, hizo ni tani zinaweza hifadhiwa na mfanya bishara wa kati.

Shukuruni tu mnaongoza taifa la wapumbavu
 
Serikali ya awamu ya sita ipo makini sana inatimiza kila ahadi kwa vitendo kama unafatilia vizuri Sekta ya kilimo sasa imepewa kipaumbele na kilimo kimelahisishwa ata pembejeo za kilimo zinapatikana kwa bei nafuu kabisa
Kipaumbele kipi? Nyie ndi walamba miguu mnadandia bila hata kutafakari, hakuba kitu hapa
 
Sure Serikali ya Rais Samia imetubadilisha mitazamo before watu walikiona kilimo kama umasikini lakini sasa tumejua kilimo ni biashara pia ni ajira ndio maana wamekifanya kiwe rahisi zaidi

Hizi porojo bana, cha ajabu unakuta ndugu zake huyo mama wanataka wapewe mtaji wakaanzishe petroli station na sio kwenda kwenye kilimo!
 
Serikali ya awamu ya sita ipo makini sana inatimiza kila ahadi kwa vitendo kama unafatilia vizuri Sekta ya kilimo sasa imepewa kipaumbele na kilimo kimelahisishwa ata pembejeo za kilimo zinapatikana kwa bei nafuu kabisa
Kaka nakubaliana na wewe, mikakati inaonekana lakini kwenye upatikanaji wa pembejeo bado hali ni mbaya sana. Naongea haya kwa nia njema sana na nipo kwenye kilimo na hapa naandika nikiwa katikati ya shamba langu la vitunguu Igawa, Mbarali, Mbeya. Mbolea hazishikiki, madawa ndio husiseme na vifaa vingine ndio balaa zaidi.
 
Mifumo ya kimgharibi inatuathiri sana...hivi ninyi mnojiita wasomi na wanasiasa mnaweza kuonyesha direct impact ya hayo yote?

Mkulima wa Njombe kijijini anaelima heka 1 mpaka 2 anayajua na anaweza kuguswa na hayo?

Serikali haina watu makini wanaoweza buni na kufanya vitu vyenye mguso wa moja kwa moja chanya kwa mkulima wa Tanzania

Ndio maana sio ajabu kusikia serikali imewanunulia mabwana shamba tabulates,bodaboda na kuongeza magari ya kifahari kwenye wizara ya kilimo pamoja na bajeti kubwa ya pesa ya utafiti lakini mkulima bado ni duni na wala hayo hayampi mabadiliko yoyote

Tatizo watu waliofuzu kwa kuandikiwa au kukopi riporti na mfumo wa kukariri elimu ya mgharibi na wengine tukiwaita maprofesa ndio wanatuongoza

Katika yote hayo hakuna hata moja linalogusa bei ya mbolea...wala ruzuku ya mbegu...muulize waziri au watenda kazi wake kama anajua hata bei ya mbegu za mahindi rejareja ni sh. ngapi?atakuonesha chati ya takwimu zilizopikwa ofisini

Hao watu waulizwe ni idadi kiasi gani wanaenda ofisi za kilimo kwa huduma mbali mbali kama ushauri nk...kama hamna au ni wachache kwanini hawajiulizi kwanini?

Zaidi mashirika ya kigeni hongera sana kama OXFAM...yamekua na direct impact kwa sababu yanafika mpaka chini

Kenya wanafanya vizuri kwa ajili ya haya pia...lakini serikali za kiafrika ni ufisadi ufisadi na siasa period

Toka huko na mafanikio yako ya kilimo kwenye karatasi you mean nothing in reality and ofcourse on field

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom