Mambo 10 kuhusu hotuba ya Rais Samia leo, Septemba 12, 2023

Feld Marshal Tantawi

JF-Expert Member
Dec 24, 2014
609
1,007
Mambo 10 kuhusu hotuba ya Rais Samia leo;

1. Ametumia muda mwingi kuzungumzia Chadema kuliko kilichompeleka kwenye mkutano. As the result Chadema imekua agenda kubwa kuliko mkutano wenyewe. Hapa Chadema 3, Msajili 0.

2. Hana taarifa sahihi jinsi jamii inavyomchukulia. Namshauri aache kukumbatia "chawa" atumie vyombo vyake kujua hali halisi ilivyo mtaani. Ni tofauti kabisa na anavyojiaminisha. Watu wamemkinai mno. Kama "watu wake" wanampenda watamwambia ukweli ili wamsaidie kubadilika.

3. Anadai kuunda kikosi maalumu cha kufuatilia maoni mtandaoni na kuyafanyia kazi. Awamu ya 5 kilikuwepo kikosi kama hicho na tulishuhudia wakosoaji wakipotea, kukamatwa na wengine kuumizwa. Je anataka kuturudisha zama hizo za giza?

4. Anadai anapenda kukosolewa, lakini ukimsikiliza dhamiri inakataa. Angekua anapenda kukosolewa leo TEC wangealikwa. Lakini kwa sababu ya kukosoa mkataba wa bandari TEC wamepuuzwa. Unawezaje kupuuza Kanisa takatifu Katoliki la Mitume, lenye nusu ya Wakristo wote nchini?

5. Chawa wamemwaminisha kwamba wanaomkosoa wanamtukana. Hawawezi kutofautisha ukosoaji na matusi. Kupinga mkataba wa bandari sio matusi. Kutetea Wamasai wa Ngorongoro sio matusi. Kudai Katiba mpya sio matusi. Wapuuze wanaokuaminisha hivyo

6. Anasema uhuru wa maoni una mipaka, lakini anaamini yeye ndio mwenye kipimo cha kuweka hiyo mipaka. Kwahiyo wanaotoa maoni yasiyomfurahisha anadhani wanatumia uhuru wao vibaya 🤣. Funny but not funny.!

7. Waliomwambia JPM kuwa Katiba haileti maendeleo, huenda ni haohao wanaomwambia Samia kuwa Katiba inaweza kuwepo na isifuatwe. Ni aibu kiongozi aliyeapa kwa Katiba kutamka maneno haya hadharani. Kimsingi alitakiwa kuitetea sana Katiba maana hata Urais wake umetokana

8. Watanzania wanataka Katiba mpya sio elimu ya Katiba. Katiba ni vile jamii inavyotaka kujiongoza yenyewe. Watanzania wanajua wanataka waongozwe vipi. Walishatoa maoni yao kupitia Tume ya Warioba. Hawahitaji kufundishwa tena kuhusu hilo.

9. Mabalozi walioalikwa leo kuna jinsi wamebadili mtizamo wao kwa Rais Samia. Wengi wamekua "disappointed" na hotuba yake. Huenda hii ikawa hotuba mbovu zaidi tangu aingie madarakani.!.

10. Polisi wataitumia hotuba hii kama kigezo cha kuzuia mikutano ya kisiasa. So tusubirie zile ramli za MaRPC kwamba "Taarifa za kiitelijensia zinaonesha uvunjifu wa amani, hivyo mkutano wenu umezuiwa".

Kwa kifupi SSH ameturudisha zama za "jiwe" kwa muda mfupi sana. Hakuwa na pumzi ndefu kama tulivyodhani. Mwaka mmoja tu wa mikutano ya kisiasa tayari amechoka na anatamani kuifuta. Tuna safari ndefu kufikia demokrasia ya kweli.!.
 
Katiba haitokaa itoke mpaka ulafi wamadaraka uje uishe, hiki kitu sijuagj kwa nini akitiliwi maanani.

Lakini tusimlaumu maza maana wote tunajua hii ni danganya toto tu ili kupooza maswala ya bandari,,

Tukija kuamka, watalala wao hii ni TIME TICKING BOOM
 
Mtu yeyote anayetumia hadaa na udanganyifu katika shughuli zake hawezi kamwe kuzifuatilia hadaa hizo na udanganyifu kwa muda mrefu, bila ya kujisahau na kuonyesha sura yake halisi.

Lakini Samia si sifa hizo tu zinazompa upungufu na kuonyesha udhaifu mkubwa sana katika mambo yote anayoyafanya.

Samia siyo kiongozi, na wala hana uwezo wa kifikra kuongoza nchi.

Kwa hiyo, hili lilikuwa ni swala la muda tu kujitambulisha kwa wananchi kuhusu madhaifu yake yote haya.
 
Inabidi niulize haya maswali, kutokana na haya aliyosema Rais Samia katika hotuba yake kuhusu katiba.

Hivi huyu mama hana 'handlers', au wamemwacha tu ajimalize mwenyewe. Lakini watamwacha ajimalize mwenyewe, bila ya kuwamaliza hata hao wanaokula toka mikononi mwake?

CCM, kama chama, wamemwacha Mwenyekiti wao akapambanie chama kwa mambo kama haya aliyoeleza leo; au tayari wameamua kumpa kamba ndefu ya kutosha (hapana siyo ile ya kula), bali ya kujitundika mwenyewe?
Mwenyekiti atajimaliza vipi bila kukimaliza chama pia?

Lakini jambo linalojitokeza hapa linatisha zaidi. Kama kiongozi mkuu kama huyu anakosa kutumia ushauri wa watu walio karibu naye, na wengine waliopewa kazi ya kumsaidia, hata katika uandishi wa taarifa tu anazotakiwa kwenda kuwasilisha mbele za watu, kaachwa ananing'inia mwenyewe kiasi hiki, kuna jambo lipi la kushangaza sasa tunapogundua kwamba hata mikataba ya IGA na DP World kaachwa tu ashikiliwe na genge lisilokuwa na nia njema kwa nchi hii?

Kuna maswali mengi ya kujiuliza kuhusu mpangilio wa uendeshaj na uongozii wa nchi yetu.

Sasa tumebaki tu na timu inayotuuliza: "Ni Nani Kama Mama"?
 
Inabidi niulize haya maswali, kutokana na haya aliyosema Rais Samia katika hotuba yake kuhusu katiba.

Hivi huyu mama hana 'handlers', au wamemwacha tu ajimalize mwenyewe. Lakini watamwacha ajimalize mwenyewe, bila ya kuwamaliza hata hao wanaokula toka mikononi mwake?

CCM, kama chama, wamemwacha Mwenyekiti wao akapambanie chama kwa mambo kama haya aliyoeleza leo; au tayari wameamua kumpa kamba ndefu ya kutosha (hapana siyo ile ya kula), bali ya kujitundika mwenyewe?
Mwenyekiti atajimaliza vipi bila kukimaliza chama pia?

Lakini jambo linalojitokeza hapa linatisha zaidi. Kama kiongozi mkuu kama huyu anakosa kutumia ushauri wa watu walio karibu naye, na wengine waliopewa kazi ya kumsaidia, hata katika uandishi wa taarifa tu anazotakiwa kwenda kuwasilisha mbele za watu, kaachwa ananing'inia mwenyewe kiasi hiki, kuna jambo lipi la kushangaza sasa tunapogundua kwamba hata mikataba ya IGA na DP World kaachwa tu ashikiliwe na genge lisilokuwa na nia njema kwa nchi hii?

Kuna maswali mengi ya kujiuliza kuhusu mpangilio wa uendeshaj na uongozii wa nchi yetu.

Sasa tumebaki tu na timu inayotuuliza: "Ni Nani Kama Mama"?
Haaa mimi najiuliza maprofessor waliona nini wakamtundukia pHD ya heshima maana naona wanakidhalilisha chuo kwa kweli
 
Moja kuuubwa lakuogofya.....
Kiongozi anayedharau "KATIBA" hadharani nikiongozi hatari saanaa kwa taifa lake!!
Maana yake unadharau hata kiapo ulichoapa huku umeshika kitabu chadini... Kitabu chadini nacho kimedharaulika sio au namnagani?
Nyerere angekuwepo asingekubali fedheha hii lkn wazee tulionao sasahivi sijui wa namna gani!?!!???
Nikumbushe Vitabu vya dini vinatufunza hiviii......
UONAPO MABAYA ONDOA KWA MIKONO YAKO,KAMA HUWEZI KEMEA,KAMA HUWEZI ONESHA UMECHUKIA....
Wazee wanachekelea kisa wanapokea pensheni yakutosha!!! Shame
 
Moja kuuubwa lakuogofya.....
Kiongozi anayedharau "KATIBA" hadharani nikiongozi hatari saanaa kwa taifa lake!!
Maana yake unadharau hata kiapo ulichoapa huku umeshika kitabu chadini... Kitabu chadini nacho kimedharaulika sio au namnagani?
Nyerere angekuwepo asingekubali fedheha hii lkn wazee tulionao sasahivi sijui wa namna gani!?!!???
Nikumbushe Vitabu vya dini vinatufunza hiviii......
UONAPO MABAYA ONDOA KWA MIKONO YAKO,KAMA HUWEZI KEMEA,KAMA HUWEZI ONESHA UMECHUKIA....
Wazee wanachekelea kisa wanapokea pensheni yakutosha!!! Shame
.
 
Mambo 10 kuhusu hotuba ya Rais Samia leo;

1. Ametumia muda mwingi kuzungumzia Chadema kuliko kilichompeleka kwenye mkutano. As the result Chadema imekua agenda kubwa kuliko mkutano wenyewe. Hapa Chadema 3, Msajili 0.

2. Hana taarifa sahihi jinsi jamii inavyomchukulia. Namshauri aache kukumbatia "chawa" atumie vyombo vyake kujua hali halisi ilivyo mtaani. Ni tofauti kabisa na anavyojiaminisha. Watu wamemkinai mno. Kama "watu wake" wanampenda watamwambia ukweli ili wamsaidie kubadilika.

3. Anadai kuunda kikosi maalumu cha kufuatilia maoni mtandaoni na kuyafanyia kazi. Awamu ya 5 kilikuwepo kikosi kama hicho na tulishuhudia wakosoaji wakipotea, kukamatwa na wengine kuumizwa. Je anataka kuturudisha zama hizo za giza?

4. Anadai anapenda kukosolewa, lakini ukimsikiliza dhamiri inakataa. Angekua anapenda kukosolewa leo TEC wangealikwa. Lakini kwa sababu ya kukosoa mkataba wa bandari TEC wamepuuzwa. Unawezaje kupuuza Kanisa takatifu Katoliki la Mitume, lenye nusu ya Wakristo wote nchini?

5. Chawa wamemwaminisha kwamba wanaomkosoa wanamtukana. Hawawezi kutofautisha ukosoaji na matusi. Kupinga mkataba wa bandari sio matusi. Kutetea Wamasai wa Ngorongoro sio matusi. Kudai Katiba mpya sio matusi. Wapuuze wanaokuaminisha hivyo

6. Anasema uhuru wa maoni una mipaka, lakini anaamini yeye ndio mwenye kipimo cha kuweka hiyo mipaka. Kwahiyo wanaotoa maoni yasiyomfurahisha anadhani wanatumia uhuru wao vibaya . Funny but not funny.!

7. Waliomwambia JPM kuwa Katiba haileti maendeleo, huenda ni haohao wanaomwambia Samia kuwa Katiba inaweza kuwepo na isifuatwe. Ni aibu kiongozi aliyeapa kwa Katiba kutamka maneno haya hadharani. Kimsingi alitakiwa kuitetea sana Katiba maana hata Urais wake umetokana

8. Watanzania wanataka Katiba mpya sio elimu ya Katiba. Katiba ni vile jamii inavyotaka kujiongoza yenyewe. Watanzania wanajua wanataka waongozwe vipi. Walishatoa maoni yao kupitia Tume ya Warioba. Hawahitaji kufundishwa tena kuhusu hilo.

9. Mabalozi walioalikwa leo kuna jinsi wamebadili mtizamo wao kwa Rais Samia. Wengi wamekua "disappointed" na hotuba yake. Huenda hii ikawa hotuba mbovu zaidi tangu aingie madarakani.!.

10. Polisi wataitumia hotuba hii kama kigezo cha kuzuia mikutano ya kisiasa. So tusubirie zile ramli za MaRPC kwamba "Taarifa za kiitelijensia zinaonesha uvunjifu wa amani, hivyo mkutano wenu umezuiwa".

Kwa kifupi SSH ameturudisha zama za "jiwe" kwa muda mfupi sana. Hakuwa na pumzi ndefu kama tulivyodhani. Mwaka mmoja tu wa mikutano ya kisiasa tayari amechoka na anatamani kuifuta. Tuna safari ndefu kufikia demokrasia ya kweli.!.
Kwa kifupi SSH ameturudisha zama za "jiwe" kwa muda mfupi sana. Hakuwa na pumzi ndefu kama tulivyodhani. Mwaka mmoja tu wa mikutano ya kisiasa tayari amechoka na anatamani kuifuta. Tuna safari ndefu kufikia demokrasia ya kweli.!.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Haaa mimi najiuliza maprofessor waliona nini wakamtundukia pHD ya heshima maana naona wanakidhalilisha chuo kwa kweli
Hiyo Ph.D. ya kutunukiwa kapewa na Kikwete, mkuu wa chuo.
Maprofesa hawana mchango wowote waliotoa katika uamzi huo.

Na hata kama wangeshirikishwa, kwani mkuu 'Zithro' (kidogo nikuite zithromycin kumbe wewe ni Zithromax) umesahau maprofesa wetu wengi wa CCM, kuanzia enzi za akina Juma Kapuya, enda hadi kwa akina Kabuti Kalamagamba na wengine wengi hapo katikati?

Maprofesa wetu karibu wote walishaamua kukabidhi hadhi yao ya usomi kwa CCM, waitumie wanavyotaka wenyewe.
 
Hiyo Ph.D. ya kutunukiwa kapewa na Kikwete, mkuu wa chuo.
Maprofesa hawana mchango wowote waliotoa katika uamzi huo.

Na hata kama wangeshirikishwa, kwani mkuu 'Zithro' (kidogo nikuite zithromycin kumbe wewe ni Zithromax) umesahau maprofesa wetu wengi wa CCM, kuanzia enzi za akina Juma Kapuya, enda hadi kwa akina Kabuti Kalamagamba na wengine wengi hapo katikati?

Maprofesa wetu karibu wote walishaamua kukabidhi hadhi yao ya usomi kwa CCM, waitumie wanavyotaka wenyewe.
very sad
 
Back
Top Bottom