Mamba mkubwa auwawa (Congo-DRC)

Mamba mkubwa auwawa (Congo-DRC)

Brother sijakurupuka kuandika nilicho andika na yawezekana nina fikra pana kuliko wewe.. Umewahi kuangalia vipindi vya wanyama? kama ndio basi utakubaliana na mimi kuwa kuna sindano maalumu mithili ya bunduki ambayo hurushwa kwa mbali na mtambo huo baada ya muda kidogo basi mnyama huyo analala na kukamatwa bila madhara yoyote

Hata mi naona kuwa hujakurupuka iko hivi asee sasa sjui ukikurupuka itakuwaje nimejaribu kufkiria wala spati jibu.

Ila yote kwa yote shukran sana kwa majibu yako mazuri kiongozi wangu.
 
Ungekuwa karibu nakunasa kerebu moja.

Unajua umenifanya nimecheka kiasi flani kwa hii comment yako asee.

Sio kosa lake mkuu ni mtazamo wa fikra zake mkuu.
 
Nchi za kiafrika za ajabu sana, mnyama akijichanganya kwenye makazi wa watu anauwawa na kufanywa kitoweo kama juzi kiboko mdogo aliyeingia kwenye dimbwai la mtu. Kwa nini wasingempiga ile sinadano ya nusu kaputi na kumchukua na kumrudisha kwenye mazingira yake ya aslili?

Anakutana na hiyo hali ili wajifunze wasirdi tena maeneo ya watu wew mbna simba akikutana n wew upigwi hiyo sindano anakugeuza kitoweo safiii😋
 
Brother sijakurupuka kuandika nilicho andika na yawezekana nina fikra pana kuliko wewe.. Umewahi kuangalia vipindi vya wanyama? kama ndio basi utakubaliana na mimi kuwa kuna sindano maalumu mithili ya bunduki ambayo hurushwa kwa mbali na mtambo huo baada ya muda kidogo basi mnyama huyo analala na kukamatwa bila madhara yoyote

Brother, usidanganyike na programs za vipindi vya TV ambavyo vinakuwa vimeandaliwa.
 
Nchi za kiafrika za ajabu sana, mnyama akijichanganya kwenye makazi wa watu anauwawa na kufanywa kitoweo kama juzi kiboko mdogo aliyeingia kwenye dimbwai la mtu. Kwa nini wasingempiga ile sinadano ya nusu kaputi na kumchukua na kumrudisha kwenye mazingira yake ya aslili?

Hii ya kiboko niliiona kwenye tv, yaani alitandikwa risasi kadhaa mbele ya camera za tv. Kisha wakaanza mkata kata kama kitoweo. Na walioua inasemekana ni mali asili eti alikuwa anakula mazao. Kiukweli, kama kiboko yupo eneo fulani (msituni) maeneo ya kumzunguka ni himaya yake. Yule kiboko yeye ndo alivamiwa na watu eneo lake. Kama huyu mamba angekuwa hazina kwa taifa la DRC endapo wangetambua upekee wake.
 
Mkuu wakati unamchoma hiyo sindano yee awe anakuangalia tu kiongozi hebu nipe upeo wa fikra kidogo ndugu.

Nimewahi ona kwenye animal planet, kama mnyama ni mkali, mnataka kumpiga sindano ya nusu kaputi, kuna kama vibunduki fulani vinakuwa na 'risasi-sindano' ambayo ina dawa. Hivyo analengewa mbali tu kama kati ya umbali wa mita 5-12 hivi.
 
Mkuu wakati unamchoma hiyo sindano yee awe anakuangalia tu kiongozi hebu nipe upeo wa fikra kidogo ndugu.

Siyo kuchoma sindano Kama binadamu , kuna bunduki ya kurusha hiyo sindano,
 
mh alikufa mwenyewe huyo!
Watamuueje?
Halafu huyo mamba nimkubwa kuliko udhaniavyo Rweza79 ni kwamba tu unashindwa kuimagine. Unajua kama wewe ni mwanaume mrefu na uliejaza vizuri unakua sawa na mguu wa mbele wa huyo mamba?
Zile picha tunazopigaga mwisho wa semina zetu si unazifahamu sasa imagine ndio hizo hapo halafu pawe na kiumbe mmoja ana funika mwanzo mwisho. Hehehe we jamaa huyu ukimwona laivu lazima utumbo ubane!

Hajafa mwenyewe, kichwa cha uzi kinasema 'auawa'. Kuna uwezekano afrika tulivyo wendawazimu, kahusishwa na nguvu za giza. Pia kwa jinsi watu walivyokusanyana kwa kujipanga nae, yaonesha ni mkubwa sana. Ila kusema urefu wa mwanaume ni sawa na mguu wake??? Labda, ila sidhani. Urefu wa mguu wake wa mbele labda futi tatu hivi.
 
Last edited by a moderator:
Brother, usidanganyike na programs za vipindi vya TV ambavyo vinakuwa vimeandaliwa.
Hivyo unataka kuniambia hakuna hiyo ganzi ya kudunga wanyama pale ambapo anatakiwa kusafiriswa au kutibiwa au unataka kubisha tuu kwa sababu ndio asili ya utanzania?
 
Nimewahi ona kwenye animal planet, kama mnyama ni mkali, mnataka kumpiga sindano ya nusu kaputi, kuna kama vibunduki fulani vinakuwa na 'risasi-sindano' ambayo ina dawa. Hivyo analengewa mbali tu kama kati ya umbali wa mita 5-12 hivi.

Siyo kuchoma sindano Kama binadamu , kuna bunduki ya kurusha hiyo sindano,
Bora mmeeleza ukweli kwani kuna watu wanabisha tu vitu vya kawaida. Ukienda ofisi zote za maliasili utakuta hizo sindano na wala sio za garama sana ila ni uzembe wetu tuu wa kuzitumia. Hutumika pale mmnyama mkali anataka kusafirishwa kutoka sehemu moja hadi nyingine au anataka kufanyiwa matibabu
 
Hivyo unataka kuniambia hakuna hiyo ganzi ya kudunga wanyama pale ambapo anatakiwa kusafiriswa au kutibiwa au unataka kubisha tuu kwa sababu ndio asili ya utanzania?

Rejea context ya mada husika pamoja na comment yako. Hakuna aliyekataa kwamba ganzi ya kucoma wanyama haipo, kilichobishaniwa ni wewe kusema kwamba ilitakiwa wananchi wasimuue huyo mamba bali wamchukue na kumpeleka mahali husika. hivi kwa mazingira halisi ya vijijini, mamba walivyo hatari pamoja na uchache/uhaba wa wataalamu wa wanyama, huo muda na maandalizi unatoka wapi?
 
Kumuangalia tu ningesimama mita 250 maana nawaogopa sana
 
Back
Top Bottom