Mama yangu kashindikana jamani, ameokoka, dini inamfanya kusahau majukumu yake

Mkuu anachosema Winnie ni kweli kabisa, mimi ilinikuta kwa mke wangu mpaka niliamua kumuacha kwa sababu nilivumilia kama miaka miwili na kila siku alikuwa ndio anaongeza, hela ya matumizi nusu kanisani nusu mnakula ndani, hela ya watoto nguo ukithubutu ukamuachia itaenda kanisani. na kila kitu tulichokuwa tunataka kufanya mpaka baba mchungaji atoe baraka. kila ijumaa mkesha unamuona jumapili jioni. kila siku anapitia kanisani anakuja nyumbani saa tatu. Hii kitu isikie kwa mwingine.

Hii ni kweli kabisa...tuliwahi kumuuliza ndugu yetu mmoja, kuwa analifikiriaje suala la uangalizi wa watoto wake ambao walikuwa wadogo..tukajibiwa "Bwana atatenda"....
 
Wakuu naombeni ushauri labda unaeza kumbadilisha mama yangu mzazi

Mama kawa ni mtu asiesikia baada ya kuokoka tangu mwaka 1995 huko nyuma alikua sio sana kiasi kwamba hata biashara alikuwa anafanya.

Cha ajabu baada ya baba kuhamishiwa Dar kikazi amekutana na kanisa tofauti na lile alilokuwa akisali, wakuu mama yangu anaenda kanisani kuanzia saa mbili asubuhi mpaka saa tatu.

Hajui wadogo zangu wawili wamekula nini wameoga na wako wapi, imefikia baba kutoka kazini na kupika. Cha ajabu hata akipewa hela ya mtaji yote anapeleka kanisani hajui mme ni nini amekula. Kashauriwa na kila mtu hadi bibi na babu waliomzaa ila habadiliki mpaka baba kathubutu kusema ana mchepuko na ndio unaompa furaha hapa duniani.

Sasa wakuu je, hata kama ni kumuomba Mungu kweli hata kusahau majukumu yako kama mama kumsahau mume wako hata hela ya matumizi ya kula unapeleka kanisani. Nathubutu kusema mama nahisi anapepo na nina mashaka na hilo kanisa kwani mama kazeeka sana kaisha jamani
.

Huyo mshauri mshua wako apige chini fasta! Maisha yenyewe yako wapi ya kubembelezana? Huyo kesha mchoka mshua anatumia Kanisa kama kisingizio tu, lakini ukweli uko hapo na ukimfwatilia sana utakuta huko unakokuita Kanisani ana jamaa mwingine mpya mwenye mambo mapya, hivyo Ushauri wangu mwambie mshua wako apige chini haraka sana kabla hajakufa kwa shinikizo la Damu kwa kufumania live bila chenga!
 
Hii ni kweli kabisa...tuliwahi kumuuliza ndugu yetu mmoja, kuwa analifikiriaje suala la uangalizi wa watoto wake ambao walikuwa wadogo..tukajibiwa "Bwana atatenda"....

Hahahaha hata yeye husema mungu atatenda yani nivichekesho jaman
 
nawasiwasi na hilo kanisa lisije likawa ni siloam maana wale jamaa ni zaidi ya noma,lakn pia yeye kaamua kumtumikia Mungu labda karama yake ndo hiyo kufanya kazi ya kanisa kwa maana vile vipawa vya roho mtakatifu hata hekima pia ni moja ya kipawa,lakn pia ukikumbuka kipindi cha Yesu na wanafunzi wake kuna mwanafunzi alifiwa na baba yake akamuomba mwalimu wake ambaye ni yesu ili amruhusu kwenda kuzika lakini yesu akamwambia waache wafu wakazike wafu wenzao,kwhyo mwache mama afanye kazi ya Mungu jaman.

So watoto wake ni wafu
 
Hahahaha hata yeye husema mungu atatenda yani nivichekesho jaman

Yaani naelewa situation yako, nishakumbana na wa hivi wengi tu.....Kuna mmoja nilisimama kidete mlangoni mwa kanisa kumsubiri mchungaji tuandikishiane achukue dhamana ya ndugu aliyekuwa mgonjwa (principle yao wagonjwa haendi hospitali)...

Sipingani na kusali, ila yatokanayo ndio yanayokuwa kero...
 
Yaani naelewa situation yako, nishakumbana na wa hivi wengi tu.....Kuna mmoja nilisimama kidete mlangoni mwa kanisa kumsubiri mchungaji tuandikishiane achukue dhamana ya ndugu aliyekuwa mgonjwa (principle yao wagonjwa haendi hospitali)...

Sipingani na kusali, ila yatokanayo ndio yanayokuwa kero...

Inatesa sana inahuzunisha
 
Hilo kanisa limemvuta zaidi sababu kila anachoambiwa wanampata, pesa ndio muhimu kwa kanisa hilo.

ni kutafuta njia ya kuongea na hao wa kanisani bila yeye kujuana kuwabana waanze kumshauri aangalie familia yake. Ila sababu pesa zinahusika itakuwa tabu kidogo wao watakosa hizo

Mtapata njia kutokana na majibu yao

Poleni inaudhi, ila makanisa mengi ni biashara na wengine wanatumia voodoi pia kunasa waumini wawasikilize na kuwaabudu
 
winme

Kanisa gani? Kama ni pool of siloam ujue kesha potea mhamisheni haraka.

inhi... nilikuwa na wazo kama lako maana kuna mama namjua naye alisababisha mtafaruku mkubwa ndoani. Kuna wakati alikuwa anaingia kwenye mfungo wa siku 40. Mfungo wake ulikuwa hatari maana hata unyumba alikuwa hatoi mpaka mfungo uishe. Akitoka kazini ni kanisani. Baba wa watu akaamua kujipunguzia mawazo kwenye pombe tu. Madhehebu hasa yanayojiita ya kiroho yana cases nyingi za aina hii.

Kwa ujumla watu wengi wanaokumbwa na uteja wa dini wanakuwa na matatizo ya akili kwa mfano sononi. Wanakwenda kwenye dini kutafuta faraja. Wapo ambao dini inawasidia wanarudi kwenye hali zao za kawaida. Wengine wanazama humo kwenye dini mpaka wanapotelea huko. Dini ndo inakuwa kila kitu kwao. Tatizo la watu wa aina hii wanakuwa wameshajifungia kwenye ulimwengu wao kiasi kwamba hawasikii la mtu kiasi kwamba inakuwa shida kuweza kuwasaidia.

Hakuna mwanamke mwenye akili timamu anayeweza kuwaacha watoto wake na mumewe bila ulinzi na chakula. Kwa hiyo ni wazi huyu mama anaumwa akili. Kinachouma ni pale mchungaji wake anachuma faida kwenye tatizo la mama kama huyu. Cha kufanya ni kutafuta mtu ambaye huyu mama anamheshimu na kumsikiliza, aongee na huyu mama mpaka mama akubali ana tatizo. Akikubali mnaweza kumpeleka hospitali yenye kitengo cha magonjwa ya akili.
 
Mkuu Bujibuji, hope ushamwelewa huyu mtu wako...
winme we si mkristo... Kwa majibu yako tu inaonyesha nia yako ni kuchafua imani za watu kwa style ya indirect... Kama kweli na una uhakika kwa nn usiwe na ujasiri wa kusema?

Well ushawaingiza wakristo wengi mkenge kwa kuamini blaa blaa zako za uongo ila nia yako tushaijua sisi ma GREAT THINKERS.. Pole

we kweli unahitaji huduma ya dharura kama lilivyo jina lako. Inaelekea na wewe ni teja la dini (religion fanatic) kama huyu mama sema wewe bado hujakolea. Kama maelezo ya huyu dada umeyaona kuwa ni kinyume na ukristo wako basi na wewe unaelekea huko huko. Hata mtume paulo alikuwa na muda wa kutengeneza maturubali ili apate chakula. Tena huyo huyo alisema asiyeangalia watu wa nyumbani mwake ni mwovu. Huyo huyo alisema watu wawe na kiasi. Huyo huyo alisema wake wawatii waume zao. Pia asiyefanya kazi na asile.
 
Jamani, mimi ninavyojua, huduma huwa na muda maalumu. Hata sisi tunahuduma kanisani. Kila mtu ana nafasi yake na anapangiwa kulingana na muda alionao. Sijawahi kuona mtu anapangiwa huduma kila siku na muda wote kama huo. Lakini siku hizi kuna dini nyingi na nyingine ni za kishetani. Ni bora umuweke katika maombi anaweza kukombolewa. Tafuta kanisa lililosimama katika maombi hasa Charismatiki Katoliki mama yetu atakombolewa. Unaweza kutoa mawasiliano yako kupitia "mathiaskabyemera@gmail.com" ili nikuunganishe na wahudumu wa kukuombea ili kumkomboa mama.
 
Pole sana winme kwa mnayoyapata ,wokovu hauko hivyo kabisa nimezaliwa kwenye familia ya wokovu naujua vizuri wala hamna ujinga na ushetani kama huo.

Nimesoma post zako zote naona mshajitahidi sana kadri ya uwezo wenu mm naona sasa muingie kivitendo zaidi kwanza kabisa kateni matumizi kwa mama yoyote yale hamna kumpatia pesa hata utaratibu wa chakula ubadilike kwa muda potelea mbali familia iteseke kwa muda.

Pili mdili na mchungaji mfuateni na sura za kazi kweli kweli hasa ikibidi na kasilaha ka gheresha kawepo.

Tatu msafirisheni mama yenu aende mahali pazuri kupumzika huko mtatafuta mtu mzuri wa kumfanyia counseling.

Pole sana kwa yote.
 
Last edited by a moderator:
Ni kweli dini ni kama bangi, hasa haya makanisa ya walokole wana mambo mengi sishangai hilo, nafahamu kwenda kanisani asubuhi kurudi sa 3 usiku ni kawaida, mf; J2 ibada inaanza sa 3 asubuhi inaisha sa 8 - 9, au pengine sa 10, mkitoka mara wamama wabaki kidogo, mara viongozi sijui wanini wanahitajika, au kuna wageni itabidi wapikiwe, au kuna semina masaa 2 - 3, au kikao cha viongozi wa maombi, nk: believe mama yako hana michepuko, isipokuwa amejisahau na ameamini kwamba Mungu atamuona zaidi atakapoiacha familia na kujitoa kwake, kitu ambacho anakosea na hata Mungu naamini hawezi kufurahishwa nacho.

Mpe ushauri tu, kama anaishi kijijini ndio balaa kama ulivyosema hapo juu anaweza kwenda kanisani na akaenda kulima tu, ndio hivyo sasa anaamini akimlimia mchungaji wake atabarikiwa huku hajalima shamba lake, wala kuwalisha watoto na mumewe, amesahau Biblia inamwambia amuheshimu mumewe, pia amesahau kama Biblia inamwambia kwamba "mwanamke aliye na hekima hujenga nyumba yake, bali ......" Mithali 14:1
 
ana ugonjwa wa akili unaoitwa.... 'religious grandiose' na ni vigumu sana ya yeye kukubali kuwa anaumwa, so sidhani hata kama atakubali kumuona daktari.
 
mm naona kuna tatizo ndani ya familia yenu ambayo imemsababishia mama yako kushinda kwa kanisa tu wala hasijali familia yake
cha kufanya kaa chini angalia tatizo ni nini kisha ndo uanze kuchukua hatua za kufanya
kingine sio busara kuja hapa kumuanika mama ayako au familia yako ungeenda kwa wakubwa yaani mababu au wazee wangemshauri na kujua chanzo ni nini au kingine ungempeleka kwa wanasaikolojia ili wajue tatizo la ubongo wa mama yako umekaaje uenda ameshaathirika kichwani ninyi hamjui

kingine usifanye ulokole uchukiwe na kila mtu kwa kutangaza hapa ulokole ni mzuri ila tatizo wale walioupokea wamepokeaje na siku hizi kuna madhehebu mingi yanafunguliwa mengine ni dini za uongo tu hakuna chochote
kuna mapepo kwenye dini hzo ambazo zinapelekea kuharibu familia nyingi na kuzisambaratisha hvyo jua na kuwa mtu mwenye kutambua roho iangamizayo ndani ya familia yenu kuwa mwombaji kutakufanya kuiokoa famiilia yako
 
Pole sana winme kwa mnayoyapata ,wokovu hauko hivyo kabisa nimezaliwa kwenye familia ya wokovu naujua vizuri wala hamna ujinga na ushetani kama huo.

Nimesoma post zako zote naona mshajitahidi sana kadri ya uwezo wenu mm naona sasa muingie kivitendo zaidi kwanza kabisa kateni matumizi kwa mama yoyote yale hamna kumpatia pesa hata utaratibu wa chakula ubadilike kwa muda potelea mbali familia iteseke kwa muda.

Pili mdili na mchungaji mfuateni na sura za kazi kweli kweli hasa ikibidi na kasilaha ka gheresha kawepo.

Tatu msafirisheni mama yenu aende mahali pazuri kupumzika huko mtatafuta mtu mzuri wa kumfanyia counseling.

Pole sana kwa yote.

Nakubaliana na wewe katika yote isipokuwa hapo kwenye kumkatishia huduma kama chakula. Mtu akishafikia hatua hii unafikiri huwa anajali? Kwanza jiulize tangu asubuhi mpaka usiku anapokuwa huko kanisani anakula? Huyu ukimkatishia huduma anakupa neno la biblia "majaribu hayana budi kuja....." "....nao watawatesa na kuwaua....." "...kuishi ni kristo kufa ni faida......". Huoni mumewe alishamfungia mpaka nje lakini hakuacha? Matatizo ya afya ya akili tanzania ni makubwa ila hayaongelewi. Tumeng'ang'ania ukimwi na kansa za matiti. Nina rafiki ambaye dadake alipata depression ila mwanzoni hatukujua kama ana tatizo. Akaanza tabia ya ulevi na umalaya. umalaya ulianza kutokana na hitaji la pombe maana alishaacha kazi kwa hiyo akawa anaenda baa kuhemea. mamake alipoona ameshindwa kumuachisha pombe ikabidi awe anampa hela ya pombe lakini ikafika mahali anashindwa. Wameenda kwenye maombi sana lakini wapi. Dada akafikia kupotea nyumbani hata siku 3. Kuna kipindi akapotea miezi miwili. Kurudi akarudi na mimba. akiulizwa baba wa mtoto hata hajui. akazaa lakini akawa haangalii mtoto. ghafla akaacha kutoka akawa ni mtu wa kujifungia ndani. kasheshe akaanza kula kama mchwa. muda wote ana kitu mdomoni. usiku wa manane anaenda kwenye friji anakula vikiwa vya baridi hivyo hivyo. Hapo ndo kupata wazo la kumpeleka muhimbili na sasa ana nafuu kubwa. Fikiria ni watu wa ngapi tunawahukumu bila kujua ni wagonjwa.

Huo ushauri wa kumhamisha kwa mapumziko na counseling ni mzuri lakini watahitaji ushauri wa madaktari wa akili wawape mbinu za kufanya hivyo maana kumhamisha ghafla ni kama kumuachisha teja unga au mlevi pombe ghafla. Anaweza kupata madhara makubwa zaidi.
 
Back
Top Bottom