Mkwaruzo
JF-Expert Member
- Feb 21, 2011
- 563
- 98
Ni msemo wa kwanza kati ya miwili nisiyoipenda. Mama wa kambo kama mama (na mlezi) anapaswa kupewa umuhimu wake kutokana na kazi anayoifanya na siyo kumjengea taswira ya ubaya ktk jamii. Mi naona ubaya wa mama wa kambo unaanzia ktk consept zetu mbaya juu yake hivyo kuyapindisha hata yale anayoyafanya kwa nia njema akiwa kama mlezi husika kwa wakati huo, mfano kumrudi mtoto kwa kosa alilofanya.
Msemo wa pili nisiyoupenda ni huu unaosema 'mtoto usiyemzaa ni mkubwa mwenzako'. Baada ya msemo ambao umekuja kumtia ila mama wa kambo, umekuja na huu unaomfanya asiupe umuhimu wajibu wake na pindipo akisibiwa na msemo huu, ndiyo ubaya wa mama wa kambo unapojitokeza. Mfano mtoto anapokosea, atampa adabu isiyoendana na uzito wa kosa na hata isiyo sawa na yule anayepewa.
Kwa maelezo hayo, hebu tuangalie ubaya wa mama wa kambo ulipo na ni sababu zipi zinazompelekea awe hivyo.
Msemo wa pili nisiyoupenda ni huu unaosema 'mtoto usiyemzaa ni mkubwa mwenzako'. Baada ya msemo ambao umekuja kumtia ila mama wa kambo, umekuja na huu unaomfanya asiupe umuhimu wajibu wake na pindipo akisibiwa na msemo huu, ndiyo ubaya wa mama wa kambo unapojitokeza. Mfano mtoto anapokosea, atampa adabu isiyoendana na uzito wa kosa na hata isiyo sawa na yule anayepewa.
Kwa maelezo hayo, hebu tuangalie ubaya wa mama wa kambo ulipo na ni sababu zipi zinazompelekea awe hivyo.