Elections 2010 Mama Sitta aeleza alivyokamatwa na TAKUKURU

Mazingira ya Mama sitta yanatia shaka kidogo hasa muda na mahali.Lakini pia ningependa kujua huyo mtoto ana uhusianano gani na Mama Sitta.Kwanini mtoto mgonjwa asiwe amelazwa hosipital kwaajili ya matibabu na badala yake awe gest house ?.

upo pia uwezekano mkubwa hasa kipindi hiki cha kampeni mgombea kujikuta anakwenda sehemu za ajabu ajabu pengine kujijengea mazingira mazuri kwa wapiga kura.Inawezekana Mama Sitta aliamua kweli kwenda kumwangalia mgonjwa lakini yakaandaliwa mazingira yakumchafua ili aenguliwe kwenye vikao vya mchujo kamati kuu.

Ifahamike wazi Mama Sitta ni miongoni mwa wabunge wa CCM wanaojipambanua kama wapiganaji dhidi ya lile kundi la waathirika wa kashfa za kifasadi ambao sasa wanafanya kila juhudi kuhakikisha wanakuwa na nguvu ndani ya Bunge.Ukifuatilia kwa makini harakati zote za ufisadi katika chaguzi za ndani za CCM utagundua kwamba wanaCCM wanaokumbana na mkono wa TAKUKURU ni wale wanaojiita wapiganaji !.

Na kama umejitenga na wenzio kwamba hutaki kupokea wala kutoa rushwa kwa nini uwashawishi wapiga kura kwa pesa na zawadi ili wakuchague?
 
Sasa na hao takukuru mbona huo mtego wenye wameutega 'kijinga' hivyo? Kwa maelezo yao na haya ya mama 6, sioni ni vipi takukuru wanaweza kupeleka kesi hiyo mahakamani na kushinda. Wangemwacha mpaka akamwone huyo 'mgonjwa' aliyeitiwa na ndipo wamkamate pamoja na 'mgonjwa' wake! Mbali na hapo ni kuchafuana tu kusipokuwa na manufaa yoyote na kuharibu credibility ya takukuru.

Kama katika scandal zote hizi hakuna hata moja wanayoweza kuipeleka mahakamani na kushinda nadhani Dr Hosea itabidi awajibishwe. Hivi hawa takukuru wanashindwa hata kupose kama wajumbe ili washuhudie hizo rushwa zikitolewa moja kwa moja. Ukifuatilia chaguzi hizi kwa kiasi kikubwa rushwa haijajificha kiasi cha takukuru kushindwa kupata ushahidi usio acha shaka!

Au wametumwa kufanya kazi nyingine tofauti?

Takukuru walio isafisha Richmond wakisema kila kitu kilikwenda sawa hadi kamati ya Mwakyembe iliposema vinginevyo: wataweza kweli kuona mantiki ya kuwajibika hadi Hosea ajiuzu. kama ni kujiuzulu au kulazimishwa kuwajibika sasa angekuwa tayari yuko nyumbani. Nji hii hakuna anayewajibika bwana kwa makosa ya kutokutimiza wajibu wake.
Suala la kuwajibika lingekuwa lina mantiki, unadhani CCm ingepitisha jina la Kikwete kugombea urais?

DR. SLAA IS MY HERO
 
CCM hakuna msafi, wote hiyo ndiyo staili yao ya kupata uongozi. Kama JK aliliruhusu "vitochi" kwenye kukusanya watu unategemea kuna msafi hapo! Sasa hivi rushwa inanuka kuliko kipindi kingine chochote tangu nchi hii ipate uhuru. Mgonjwa na Guest House wapi na wapi, tu bahasha je? Kama ni nduguyo mgojwa hao wana CCM wanini?
 
Kwa mtazamo wangu maelezo ya mama 6 yanaeleweka sana.....
Amejaribu tu kupindisha ukweli...

Mgonjwa gest anafanya nini? Changa la macho hilo....

Wapi Malaria sugu....!
 
TAKUKURU Ingekuwa na credibility kama Hoseah angejiuzulu au kufukuzwa kazi. Public trust is very important kwa vyombo vya dola. TAKUKURU wanatumika tena sana tu. Japo huneda lengo lilikuwa ni kutisha hasa kwa chaguzi zijazo kama Bosi wao alivyosema jana kwenye hotuba na ninahisi alitarget 2015. Tutarajie wengi kukamatw kuelekea october na hasa wale ambao pembeni ya majina yao hakuna(CCM)
 
Mh. Mama sitta maelezo yako tumeyapata ila jambo hili limejaa maswali mengi kuliko majibu. kwanza mama wewe ni mheshimiwa, umebeba dhamana kubwa kwa Taifa, kwangu mimi naona usalama wako ni muhimu sana kwako na kwataifa kwa ujumla, kutoka usiku wa manane kiasi hicho mama ilikuwa ni hatari sana aidha sikuona umuhimu wa wewe kwenda kumuona huyo mgonjwa kwani naamini mama wewe sio daktari, na fikiri kwa mamlaka uliyokuwa nayo ungeweza hata kumpigia simu mganga mkuu wa mkoa au yeyote akasaidia katika hilo. Pamoja na kuwa huenda moyo wa upendo ndiyo uliokusukuma kwenda kumuona mgojwa lakini kutokana na tukio la uchaguzi linalofanyika kesho yake lazima mitego ya kuwakamata watoa rushwa ilikuwa imetegwa sasa nakuomba usilaumu moja kwa moja TAKUKURU kwani hiyo ndiyo kazi yao ambayo wanatakiwa waifanye, na ndiyo maana kwa muda mrefu watu wamekuwa wanailalamikia sana TAKUKURU kwa kutowajibika hivyo tuache wafanye kazi yao. kutoa maelezo ya utetezi hapa nafikiri haitasaidia sana ila kama kweli unahakika kuwa umeonewa basi ni vizuri ukachukua hatua za kisheria ambazo naamini unazifahamu vizuri.Pia kumbuka hili jambo limekuwa baya kwakuwa limetokea kwako ila kama lingetokea kwa mgombea mwingine nafikiri ungewapa zawadi TAKUKURU. kama TAKUKURU wameweza kushughulika na watu kama wewe nafikiri tunapokwenda sasa ni kuzuri. bado nakukumbusha kuwa kama umeonewa njia iko wazi kuelekea mahakamani. naomba kuwasilisha!!!!!!!:A S 39::A S 39::A S 39::A S 39::A S 39:
 
Back
Top Bottom