Mama na Mwana: Nini Kinaendelea Zanzibar?

Mama na Mwana: Nini Kinaendelea Zanzibar?

mwana wa kweli huyaenzi yale aliyoanzisha baba yake.

Inamaana baba yako akianza ushoga na wewe utaenzi tabia ya ushoga?
 
Wanatofautiana political views.. ni jambo la kawaida sana sio lazima mzazi na Mwana wawe na common stand..
 
Huyu mama amewahi kuelezwa kama mmoja wa wafadhili wa Uamsho ambao ndo hasa wapiganiaji wa mamlaka kamili Zanzibar. CCM wanayo tabia na mazoea ya kuwachukua watu kama huyu mama kwenye mikutano hii kwa vitisho. Hilo wala si siri.
 
mwana wa kweli huyaenzi yale aliyoanzisha baba yake.

Inamaana baba yako akianza ushoga na wewe utaenzi tabia ya ushoga?

Katika yote uliyoyaona ni ushoga tu?? mbona mashoga hamuachi kuchafua mabaraza??
 
Anawaondoa njiani akina Nape na genge lake.,hebu wamuulize kwanini Karume alisema Muungano mwisho Chumbe ,ei si wamuhoji ili tuzidi kunufaika ? waarabu wa Pemba wajuana kwa vilemba na mambo ya WaZanzibari hutoyaweza.Waachiwe wapumue ,jingine kule kanisani wamesemaje ,Tanganyika ni lazima ni jambo la wakati tu ,msiyafinyange ya Zanzibar mkayaacha ya kwenu ,mtu kwao !!!
 
Mzee Mwanakijiji
waulize waunguja watakupa majibu; mwana wa kweli huyaenzi yale aliyoanzisha baba yake!
"Muungano kama Koti, Likikubana Shurti Ulivue - Karume Sr" ...Kwa kuzingatia kuwa Kitanda hakizai Haramu, Yupi wa Kweli katka hao wawili? ... Huwa sipendi sana kujadili issues ambazo ziko wazi ila kila mmoja wetu tunajifanya hat
uoni; Kero za Wananchi ziko kwenye Kero za Muungano ambazo hazi tatuliki kwa Muundo wa serikali 2 au 3! Ila zinaweza kupata majibu chini ya Serikali moja yenye kutenda haki kwa wananchi wake wa Bara na Visiwani ...
 
Karume alijitangaza Mfalme wa Zanzibar kwenye vikao mbalimbali Ulaya, ushahidi upo CCM kisiwandui, na alitaka kufanya kweli, ila alijua atafanikisha tu akimshirikisha Maalim Seif wa CUF anaewatetea waliomwajiri yaani Waarabu waliofukuzwa na waliomo. Amani Karume nae yupo tayari kumpa chochote ili asimikwe Ubaba wa Zanzibar forever, ndio wakakutana mwaka 2009 manake miaka ya Amani ilikuwa imeisha na wengi wakitarajia atashikishwa adabu akitoka nje ya Ikulu kwa utapeli na unyang'anyi mkubwa alofanya, ila kwa usanii wa khali ya juu, aliteka nyayo za wazenji baada ya eti kujifanya anawaunganisha ili waidai nchi yao, kaamuru shirika la mapato za zanzibar yaani ZRB ilipie gharama zote za mihadhara ya Uamsho pamoja na kupeleka watu bure kutoka pande zote za zanzibar.
Mama mwanzo alimuunga mkono, sasa katangulia kurudi nyuma baada ya kuona Zanzibar huru haiwezekani, mwanawe kwakweli kajuta ila kurudi nyuma hajui apitie mlango gani?????
 
ni yupi mwenye nguvu ya ushawishi kwa wazanzibar ?


Hassan Nassor Moyo,, bila ya Moyo Seif asingelikuwa na nguvu Zanzibar(Unguja),,,Moyo ndie aliemkututanisha Karume na Maalim Seif,kumbuka Karume na Maalim Seif walikuwa na matatizo yao ya kibinafsi ukiachana na siasa lakini Moyo ameweza kuziondoa tafauti zao na kuwakutanisha pamoja

Katika siasa za zanzibar kwa hivi sasa King maker ni Hassan Nassor Moyo
 
Hassan Nassor Moyo,, bila ya Moyo Seif asingelikuwa na nguvu Zanzibar(Unguja),,,Moyo ndie aliemkututanisha Karume na Maalim Seif,kumbuka Karume na Maalim Seif walikuwa na matatizo yao ya kibinafsi ukiachana na siasa lakini Moyo ameweza kuziondoa tafauti zao na kuwakutanisha pamoja

Katika siasa za zanzibar kwa hivi sasa King maker ni Hassan Nassor Moyo

Kwanini Hassan Nassoro Moyo?
 
Karume alijitangaza Mfalme wa Zanzibar kwenye vikao mbalimbali Ulaya, ushahidi upo CCM kisiwandui, na alitaka kufanya kweli, ila alijua atafanikisha tu akimshirikisha Maalim Seif wa CUF anaewatetea waliomwajiri yaani Waarabu waliofukuzwa na waliomo. Amani Karume nae yupo tayari kumpa chochote ili asimikwe Ubaba wa Zanzibar forever, ndio wakakutana mwaka 2009 manake miaka ya Amani ilikuwa imeisha na wengi wakitarajia atashikishwa adabu akitoka nje ya Ikulu kwa utapeli na unyang'anyi mkubwa alofanya, ila kwa usanii wa khali ya juu, aliteka nyayo za wazenji baada ya eti kujifanya anawaunganisha ili waidai nchi yao, kaamuru shirika la mapato za zanzibar yaani ZRB ilipie gharama zote za mihadhara ya Uamsho pamoja na kupeleka watu bure kutoka pande zote za zanzibar.
Mama mwanzo alimuunga mkono, sasa katangulia kurudi nyuma baada ya kuona Zanzibar huru haiwezekani, mwanawe kwakweli kajuta ila kurudi nyuma hajui apitie mlango gani?????

Unataka kusema kuwa inawezekana Amani Karume anatumia nafasi hii kutafuta mahali pa kujikingia huko mbeleni...? alifall out na viongozi wa CCM huko bara? Nakumbuka ile hotuba yake wakati wa Mkutano Mkuu wa CCM mwaka 2012...
 
Huyu mama amewahi kuelezwa kama mmoja wa wafadhili wa Uamsho ambao ndo hasa wapiganiaji wa mamlaka kamili Zanzibar. CCM wanayo tabia na mazoea ya kuwachukua watu kama huyu mama kwenye mikutano hii kwa vitisho. Hilo wala si siri.

SAsa mama mtu mzima hivi na heshima yake yote kwanini ajikute analazimika kwenda kwenye mikutano kama hii...
 
Kwanini Hassan Nassoro Moyo?

sababu nimeziandika hapo,,,,lakini vile vile Moyo ndie memba wa baraza la mapinduzi aliebakia hiyo inampa ushawishi "influence" ya kukubaliwa na wazanzibari hasa kuhusu hizi siasa za mungano zinazoendelea hivi sasa

Kwani wewe Mzee Mwanakijiji unafikiria nani ana nguvu za kisiasa zanzibar hivi sasa
 
Hapo ndipo nashindwa kuelewa siasa za Tanzania na wanasiasa kwa ujumla.
Swala la katiba sio swala la mashindano maana hatutafuti nani mshindi na nani kashindwa, Katiba ni maridhiano, katiba ni lazima ikubalike pande zote mbili, katiba ni lazima ibebe maoni ya wananchi na si ya watawala. Katiba sio ya Mama Karume wa si ya watoto wa Karume..
Ningependa katika swala nzima la katiba wanasiasa wangejiweka mbali kabisa. Katiba bora itatoka kwa wananchi
Umeona mbali , Unajua wanasiasa wameshajipa dhamana ya Katiba, wanaona wao ndio wanabeba matakwa ya wananchi kumbe wanakosea, niliwasikia baadhi ya wanasiasa wanasema kuwa wamewahooji watu wao juu ya katiba! Nilishangaa kwa kuwa jukumu hilo ilipewa tume, sasa sijui wao walioji hoji kivipi?
 
Back
Top Bottom