Mama na Mwana: Nini Kinaendelea Zanzibar?

Mama na Mwana: Nini Kinaendelea Zanzibar?

Mzee Mwanakijiji

Platinum Member
Joined
Mar 10, 2006
Posts
34,097
Reaction score
43,309
Kwa watu wanaojua au hata wale ambao wanafuatilia siasa za visiwani humo ni rahisi kuona kuwa mgawanyo huu wa kijamii ambao unatokana na siasa unaweza kuwa na madhara makubwa zaidi visiwano humo labda kuliko mgawanyo mwingine wowote katika historia ya karibuni ya Zanzibar. Binafsi bado nafuatilia kwa karibu katika kusoma na kuelewa kile hasa kinachoendelea ama hadharani au nyuma ya pazia. Hata hivyo hofu yangu ni kuwa mgawanyiko huu mkubwa utakuwa na madhara makubwa sana Zanzibar na kurudisha jamii nyuma. Kinyume na kauli ya baadhi ya watu kuwa Wazanzibari katika kudai "Mamlaka Kamili" au "Serikali Tatu" wako wamoja ushahidi ni wazi kuwa hawana umoja huo... tafakari:

Mwana:

Amani Karume akiwa na viongozi wenzake ambao wanadaiwa ndio wadai wakubwa wa "Mamlaka Kamili" ya Zanzibar na hata kudai "Serikali Tatu" ambapo Zanzibar itakuwa na Mamlaka Kamili - whatever that means.

1959334_746251598742196_4469375882401869990_n.jpg


Siku si nyingi (nne tu) Mama amesimama na Wana CCM wenzake tena huko huko Zanzibar na kusema maneno mazito tu ya kudai mfumo wa Serikali Mbili huku akionya watu wanaotaka Serikali Tatu (in extension akiwemo mwanae)...

64.jpg


Nauliza tu: Nini kinaendelea?
 
Kama uliwahi kukaa na Wazanzibar Shuleni, Chuoni, Mtaani basi kinachoendelea huko Zanzibari wote ni S3 ila wakienda Dodoma ni S2 hiyo ndio hali halisi ya ndugu zetu hawa
 
Huyu mama nishapapata kumsikia kwa masikio yangu kuwa watu waachwe wauzungumze muungano. Sasa kutaka kuuboresha kwa serekali tatu si ndo kuuzungumza huko? Au Uzungumzwe kwa namna gani? Zanzibar hakuna siri yeyote, kila kitu kipo fawahisha kwamba wazanzibari wanataka mamlaka kamili yakijamulia mambo yao bila ya kuingiliwa na Tanganyika ambaye kisharia yupo na hadhi sawa na zanzibar katika partnership yao.
Tatizo kubwa nilionalo ni ulafi, unafiki na tamaa ya uluwa waliyonayo viongozi wa ccm zanzibar.
 
Tatizo la Zanzibar ni Ccm wachache waliobaki hakuna siri wala nyuma ya pazia, hao wenyewe wakiweko znz wanakua tofauti wakiweko dodoma

Fuatilia semina zilizokua zikifanyika baraza la Wawakilishi wote walikua wanataka mamlaka kamili ya zanzibar

Warioba ameleta jibu waache waseme baadae turudi kwenye rasimu.
 
hakuna watu wasio na ujasiri km wazanzibar. ila wanavopiga domo!
 
Kwenye kura ya maoni Wanzinzibar wataongea vilivyo, vile vile kwa jinsi upepo unavyo kwenda kuna kila dalili ya kuikomboa Tanganyika yetu kwa kupitia kwa Wanzanzibar....
 
Mwanakijiji ukitaka kufahamu nini kinaendelea zanzibar angalia katika walio kimbelembele kudai mamlaka kamili ndio hao hao walikuwa mbele kuanza pirika za mapinduzi (Moyo na wenzie). Hao hao walipindua serikali halali ya wazanzibar 1963 sasa wanadai mamlaka kamili nadhani utafahamu nini kinaendelea. Haya ni maneno mazito utakuja kuniambia siku za mbeleni.

Binafsi nilikubeza kuhusu serikali moja hapo nyuma ila baada ya kugundua janja ya nyani nimegeuza njia na kusupport hoja ya serikali moja kuna jambo liko nyuma ya pazia yangu macho!!!
 
Mama sahivi yuko upande wa mwanawe Ali,inshallah huenda akarejea tena Ikulu ya Zenj.
 
Nadhani mama anatumiwa ili wapate kugombana na mwanae,na hii haileti picha nzuri ya CCM kutumia familia hiyo kufanya wakitakacho.Cha msingi ni marithiano ya pande zote mbili,wakae wajadili waje na kitu chenye maana.

Na kitu kingiene upande wa pili wa Tanzania Bara una mambo ambayo wananchi wake wangependa yabadilike na bila marithiano hayawezekani.Si halali kila wakitakacho upande wa pili wa Muungano hadi inafikia kuvunja sheria za nchi/Katiba lazima wapewe na hapa ndipo kosa lilipoanzia.

Kubadili chochote ilitakiwa kuwe na marithiano ya pande zote mbili na ziwe zimewekwa kisheria na siyo kwa siri.
 
Kina choendelea Zanzibar ni kudai uhuru mwengne .
 
mama ndiye anayempa kiburi mtoto-rais mstaafu. Yule mwingije, yaani balozi karume anapingana nao sana. Nakubaliana na mwanakijiji kuwa kuna siri nzito hapo.


mkuu mama analala anaota kifo cha mume wake kilivyo kuwa!
anashindwa kuweka wazi nini anataka coz bado ndoto za kifo cha mume wake zinamsumbua sana na kumuogopesha siunajuwa ukingatwa na nyoka ukikanyaga jani nini kinatokea! maoni ya huyo mama yatatolewa na malim seifu pamoja na ya mwanaye
 
Jana katika mdahalo ulikuwa unarushwa na ITV, Mh. Duni alisisitiza zaidi ya mara moja ili mchakato wa Katiba Mpya uendelee ni kwa wazanzibari kuridhiana na kwenda Dodoma na msimamo mmoja. Na jukumu hili aliwapa viongozi wao wakiongozwa na Rais wa Zanzibar Mh Shein wakiwemo makampuni wake wote wawili! Inaweza pia kutoa picha kinachoendelea Zanzibar.
 
Hapo ndipo nashindwa kuelewa siasa za Tanzania na wanasiasa kwa ujumla.
Swala la katiba sio swala la mashindano maana hatutafuti nani mshindi na nani kashindwa, Katiba ni maridhiano, katiba ni lazima ikubalike pande zote mbili, katiba ni lazima ibebe maoni ya wananchi na si ya watawala. Katiba sio ya Mama Karume wa si ya watoto wa Karume..
Ningependa katika swala nzima la katiba wanasiasa wangejiweka mbali kabisa. Katiba bora itatoka kwa wananchi
 
Mama Karume ameahidiwa kutuzwa maisha yake yote kama mke wa Makamu wa kwanza wa Rais na SMT, kama ambavyo mama Nyerere anatunzwa na SMT. Huu Muungano Watanganyika tunaulinda kwa gharama kubwa sana.
 
mwanakijiji amechuja siku hizi, mada zake zinakaa hata wiki haizifiki page moja. watu wamemstukia ni mzushi.
 
Back
Top Bottom