Powel Mizengo
Senior Member
- Jan 20, 2014
- 126
- 24
Nakumbuka ni muda mrefu toka nilipoleta thread yenye Title "MAMA MKWE ANANING'ANG'ANIA". Kama wengi wenu mlivyonishauri,niliupokea ushauri nikachanganya na akili zangu na matokeo yake mi nikaamua kuchukua mdogo mtu!!!kwa sasa nipo naishi na huyo mdogo mtu!!!!Tatizo kubwa ambalo limenifanya nirudi tena kwenu wadau ni hili; Huyu binti imekuwa ni kawaida yake pindi naporudi toka kwenye matembezi yangu na hasa napokuwa nimerudi nimepombeka,yeye anazama kwenye Wallet yangu na kuchota kiasi cha pesa akidhani mi sina kumbukumbu ya kiasi nilichoacha!!!Ameshanifanyia mchezo huu muda sasa!!Si kwamba simwachii pesa za matumizi bali sielewi tatizo lake ni nini kunipekua mifukoni!!! Jamani wadau,huyu binti bado sijalipa mahali(Bride Price) Nilipewa ili kureplace dada mtu ambaye kisa chake nilishawaeleza!!!Na tayari tulikuwa na mipango ya kuoana mwishoni mwa mwaka huu yaani Desemba!!b. Sasa haka katabia kananitatiza!!!!Naomba mchango wenu wa ushauri manake sielewi kama anaweza badilika kweli!!!